< Salme 148 >
1 Halleluja! Pris HERREN i Himlen, pris ham i det høje!
Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
2 Pris ham, alle hans Engle, pris ham, alle hans Hærskarer,
Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
3 pris ham, Sol og Maane, pris ham, hver lysende Stjerne,
Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
4 pris ham, Himlenes Himle og Vandene over Himlene!
Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
5 De skal prise HERRENS Navn, thi han bød, og de blev skabt;
Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
6 han gav dem deres Plads for evigt, han gav en Lov, som de ej overtræder!
Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
7 Lad Pris stige op til HERREN fra Jorden, I Havdyr og alle Dyb,
Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
8 Ild og Hagl, Sne og Røg, Storm, som gør, hvad han siger,
moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
9 I Bjerge og alle Høje, Frugttræer og alle Cedre,
Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
10 I vilde Dyr og alt Kvæg, Krybdyr og vingede Fugle,
wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
11 I Jordens Konger og alle Folkeslag, Fyrster og alle Jordens Dommere,
Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
12 Ynglinge sammen med Jomfruer, gamle sammen med unge!
wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
13 De skal prise HERRENS Navn, thi ophøjet er hans Navn alene, hans Højhed omspænder Jord og Himmel.
Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
14 Han løfter et Horn for sit Folk, lovprist af alle sine fromme, af Israels Børn, det Folk, der staar ham nær. Halleluja!
Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.