< Salme 141 >

1 En Salme af David. HERRE, jeg raaber til dig, il mig til Hjælp, hør min Røst, naar jeg raaber til dig;
Ee Yahwe, ninakulilia wewe; uje upesi kwangu. Unisikilize nikuitapo.
2 som Røgoffer gælde for dig min Bøn, mine løftede Hænder som Aftenoffer!
Maombi yangu na yawe kama uvumba mbele zako; mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama dhabihu ya jioni.
3 HERRE, sæt Vagt ved min Mund, vogt mine Læbers Dør!
Ee Yahwe, uweke mlinzi kinywani mwangu; mngojezi malangoni pa midomo yangu.
4 Bøj ikke mit Hjerte til ondt, til at gøre gudløs Gerning sammen med Udaadsmænd; deres lækre Mad vil jeg ikke smage.
Usiruhusu tamaa ya moyo wangu kutamani uovu wowote wala kushiriki katika matendo ya dhambi na watu waishio maovuni. Nisile vyakula vyao vya anasa.
5 Slaar en retfærdig mig, saa er det Kærlighed; revser han mig, er det Olie for Hovedet, ej skal mit Hoved vise det fra sig, end sætter jeg min Bøn imod deres Ondskab.
Mwenye haki na anipige; nao utakuwa ni wema kwangu. Anirudi; itakuwa kama mafuta kichwani pangu; kichwa changu na kisikatae kupokea. Lakini maombi yangu siku zote yatakuwa dhidi ya matendo yao mauvu.
6 Ned ad Klippens Skrænter skal Dommerne hos dem styrtes, og de skal høre, at mine Ord er liflige.
Viongozi wao watatupwa chini toka juu mlimani; watayasikia maneno yangu kuwa ni matamu.
7 Som naar man pløjer Jorden i Furer, spredes vore Ben ved Dødsrigets Gab. (Sheol h7585)
Watalazimika kusema, “Kama vile jembe moja livunjapo ardhi, hivyo mifupa yetu imesambaratishwa kinywani pa kuzimu.” (Sheol h7585)
8 Dog, mine Øjne er rettet paa dig, o HERRE, Herre, paa dig forlader jeg mig, giv ikke mit Liv til Pris!
Hakika macho yangu yanakutazama wewe, Yahwe, Bwana; katika wewe napata kimbilio; usiiache nafsi yangu.
9 Vogt mig for Fælden, de stiller for mig, og Udaadsmændenes Snarer;
Unilinde dhidi ya mitego waliyoiweka kwa ajili yangu, na matanzi yao watendao maovu.
10 lad de gudløse falde i egne Garn, medens jeg gaar uskadt videre.
Waovu na waangukie kwenye nyavu zao wenywe pindi mimi nitorokapo.

< Salme 141 >