< Salme 130 >

1 Sang til Festrejserne. Fra det dybe raaber jeg til dig, HERRE,
Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2 o Herre, hør min Røst! Lad dine Ører lytte til min tryglende Røst!
Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
3 Tog du Vare, HERRE, paa Misgerninger, Herre, hvo kunde da bestaa?
Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4 Men hos dig er der Syndsforladelse, at du maa frygtes.
Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
5 Jeg haaber paa HERREN, min Sjæl haaber paa hans Ord,
Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
6 paa Herren bier min Sjæl mer end Vægter paa Morgen, Vægter paa Morgen.
Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
7 Israel, bi paa HERREN! Thi hos HERREN er Miskundhed, hos ham er Forløsning i Overflod.
Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
8 Og han vil forløse Israel fra alle dets Misgerninger.
Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.

< Salme 130 >