< Ordsprogene 6 >
1 Min Søn: har du borget for din næste og givet en anden Haandslag,
Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
2 er du fanget ved dine Læber og bundet ved Mundens Ord,
kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
3 gør saa dette, min Søn, og red dig, nu du er kommet i Næstens Haand: Gaa hen uden Tøven, træng ind paa din Næste;
basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
4 und ikke dine Øjne Søvn, ej heller dine Øjenlaag Hvile,
Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
5 red dig som en Gazel af Snaren, som en Fugl af Fuglefængerens Haand.
Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
6 Gaa hen til Myren, du lade, se dens Færd og bliv viis.
Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
7 Skønt uden Fyrste, Foged og Styrer,
Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
8 sørger den dog om Somren for Æde og sanker sin Føde i Høst.
lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
9 Hvor længe vil du ligge, du lade, naar staar du op af din Søvn?
Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
10 Lidt Søvn endnu, lidt Blund, lidt Hvile med samlagte Hænder:
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
11 som en Stimand kommer da Fattigdom over dig, Trang som en skjoldvæbnet Mand.
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
12 En Nidding, en ussel Mand er den, som vandrer med Falskhed i Munden,
Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
13 som blinker med Øjet, skraber med Foden og giver Tegn med Fingrene,
ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
14 som smeder Rænker i Hjertet og altid kun ypper Kiv;
ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
15 derfor kommer hans Undergang brat, han knuses paa Stedet, kan ikke læges.
Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
16 Seks Ting hader HERREN, syv er hans Sjæl en Gru:
Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
17 Stolte Øjne, Løgnetunge, Hænder, der udgyder uskyldigt Blod,
macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
18 et Hjerte, der udtænker onde Raad, Fødder, der haster og iler til ondt,
moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
19 falsk Vidne, der farer med Løgn, og den, som sætter Splid mellem Brødre.
shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
20 Min Søn, tag Vare paa din Faders Bud, opgiv ikke din Moders Belæring,
Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
21 bind dem altid paa dit Hjerte, knyt dem fast om din Hals;
Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.
22 paa din Vandring lede den dig, paa dit Leje vogte den dig, den tale dig til, naar du vaagner;
Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.
23 thi Budet er en Lygte, Læren Lys, og Tugtens Revselse Livets Vej
Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,
24 for at vogte dig for Andenmands Hustru, for fremmed Kvindes sleske Tunge!
yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.
25 Attraa ej i dit Hjerte hendes Skønhed, hendes Blik besnære dig ej!
Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,
26 Thi en Skøge faar man blot for et Brød, men Andenmands Hustru fanger dyrebar Sjæl.
kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.
27 Kan nogen bære Ild i sin Brystfold, uden at Klæderne brænder?
Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?
28 Kan man vandre paa glødende Kul, uden at Fødderne svides?
Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?
29 Saa er det at gaa ind til sin Næstes Hustru; ingen, der rører hende, slipper for Straf.
Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.
30 Ringeagter man ikke Tyven, naar han stjæler for at stille sin Sult?
Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.
31 Om han gribes, maa han syvfold bøde og afgive alt sit Huses Gods.
Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.
32 Afsindig er den, der boler med hende, kun en Selvmorder handler saa;
Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
33 han opnaar Hug og Skændsel, og aldrig udslettes hans Skam.
Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;
34 Thi Skinsyge vækker Mandens Vrede, han skaaner ikke paa Hævnens Dag;
kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
35 ingen Bøde tager han god; store Tilbud rører ham ikke.
Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.