< Ordsprogene 29 >

1 Hvo Nakken gør stiv, skønt revset tit, han knuses brat uden Lægedom.
Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
2 Er der mange retfærdige, glædes Folket, men raader de gudløse, sukker Folket.
Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
3 Hvo Visdom elsker, glæder sin Fader, hvo Skøger omgaas, bortødsler Gods.
Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
4 Kongen grundfæster Landet med Ret, en Udsuger lægger det øde.
Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
5 Mand, der smigrer sin Næste, breder et Net for hans Fod.
Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
6 I sin Brøde hildes den onde, den retfærdige jubler af Glæde.
Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
7 Den retfærdige kender de ringes Retssag; den gudløse skønner intet.
Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
8 Spottere ophidser Byen, men Vismænd, de stiller Vrede.
Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
9 Gaar Vismand i Rette med Daare, vredes og ler han, alt preller af.
Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
10 De blodtørstige hader lydefri Mand, de retsindige tager sig af ham.
Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
11 En Taabe slipper al sin Voldsomhed løs, Vismand stiller den omsider.
Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
12 En Fyrste, som lytter til Løgnetale, faar lutter gudløse Tjenere.
Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
13 Fattigmand og Blodsuger mødes, HERREN giver begges Øjne Glans.
Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
14 En Konge, der dømmer de ringe med Ret, hans Trone staar fast evindelig.
Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
15 Ris og Revselse, det giver Visdom, uvorn Dreng gør sin Moder Skam.
Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
16 Bliver mange gudløse, tiltager Synd; retfærdige ser med Fryd deres Fald.
Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
17 Tugt din Søn, saa kvæger han dig og bringer din Sjæl, hvad der smager.
Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
18 Uden Syner forvildes et Folk; salig den, der vogter paa Loven.
Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19 Med Ord lader Træl sig ikke tugte, han fatter dem vel, men adlyder ikke.
Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
20 Ser du en Mand, der er hastig til Tale, for en Taabe er der snarere Haab end for ham.
Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
21 Forvænner man sin Træl fra ung, vil han til sidst være Herre.
Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
22 Hidsig Mand vækker Strid, vredladen Mand gør megen Synd.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
23 Et Menneskes Hovmod ydmyger ham, den ydmyge opnaar Ære.
Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
24 Hæleren hader sit Liv, han hører Forbandelsen, men melder intet.
Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
25 Frygt for Mennesker leder i Snare, men den, der stoler paa HERREN, er bjærget.
Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
26 Mange søger en Fyrstes Gunst; Mands Ret er dog fra HERREN.
Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
27 Urettens Mand er retfærdiges Gru, hvo redeligt vandrer, gudløses Gru.
Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.

< Ordsprogene 29 >