< Ordsprogene 28 >

1 Den gudløse flyr, skønt ingen er efter ham; tryg som en Løve er den retfærdige.
Mtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza, bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
2 Ved Voldsmands Brøde opstaar Strid, den kvæles af Mand med Forstand.
Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi, bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.
3 En fattig Tyran, der kuer de ringe, er Regn, der hærger og ej giver Brød.
Mtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.
4 Hvo Loven sviger, roser de gudløse, hvo Loven holder, er paa Krigsfod med dem.
Wale waiachao sheria huwasifu waovu, bali wale waishikao sheria huwapinga.
5 Ildesindede fatter ej Ret; alt fatter de, som søger HERREN.
Watu wabaya hawaelewi haki, bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.
6 Hellere en fattig med lydefri Færd end en, som gaar Krogveje, er han end rig.
Afadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.
7 Forstandig Søn tager Vare paa Loven, men Drankeres Fælle gør sin Fader Skam.
Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali rafiki wa walafi humwaibisha baba yake.
8 Hvo Velstand øger ved Aager og Opgæld, samler til en, som er mild mod de ringe.
Yeye aongezaye utajiri wake kwa riba kubwa mno hukusanya kwa ajili ya mwingine, ambaye atawahurumia maskini.
9 Den, der vender sit Øre fra Loven, endog hans Bøn er en Gru.
Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
10 Leder man retsindige vild paa onde Veje, falder man selv i sin Grav; men de lydefri arver Lykke.
Yeye ambaye humwongoza mwenye haki kwenye mapito mabaya, ataanguka kwenye mtego wake mwenyewe, bali wasio na lawama watapokea urithi mwema.
11 Rigmand tykkes sig viis, forstandig Smaamand gennemskuer ham.
Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua.
12 Naar retfærdige jubler, er Herligheden stor, vinder gudløse frem, skal man lede efter Folk.
Mwenye haki ashindapo, kuna furaha kubwa, bali waovu watawalapo, watu hujificha.
13 At dølge sin Synd fører ikke til Held, men bekendes og slippes den, finder man Naade.
Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema.
14 Saligt det Menneske, som altid ængstes, men forhærder man sit Hjerte, falder man i Ulykke.
Amebarikiwa mtu ambaye siku zote humcha Bwana, bali yeye afanyaye moyo wake kuwa mgumu huangukia kwenye taabu.
15 En brølende Løve, en graadig Bjørn er en gudløs, som styrer et ringe Folk.
Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge.
16 Uforstandig Fyrste øver megen Vold, langt Liv faar den, der hader Rov.
Mtawala dhalimu hana akili, bali yeye achukiaye mapato ya udhalimu atafurahia maisha marefu.
17 Et Menneske, der tynges af Blodskyld, er paa Flugt til sin Grav; man hjælpe ham ikke.
Mtu mwenye kusumbuliwa na hatia ya kuua atakuwa mtoro mpaka kufa; mtu yeyote na asimsaidie.
18 Den, som vandrer lydefrit, frelses, men den, som gaar Krogveje, falder i Graven.
Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama hulindwa salama, bali yeye ambaye njia zake ni potovu ataanguka ghafula.
19 Den mættes med brød, som dyrker sin Jord, med Fattigdom den, der jager efter Tomhed.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.
20 Ærlig Mand velsignes rigt, men Jag efter Rigdom undgaar ej Straf.
Mtu mwaminifu atabarikiwa sana, bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka hataacha kuadhibiwa.
21 At være partisk er ikke godt, en Mand kan forse sig for en Bid Brød.
Kuonyesha upendeleo si vizuri, hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate.
22 Misundelig Mand vil i Hast vinde Gods; at Trang kommer over ham, ved han ikke.
Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri, naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.
23 Den, der revser, faar Tak til sidst fremfor den, hvis Tunge er slesk.
Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi, kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili.
24 Stjæle fra Forældre og nægte, at det er Synd, er at være Fælle med hærgende Mand.
Yeye amwibiaye babaye au mamaye na kusema, “Si kosa,” yeye ni mwenzi wa yule aharibuye.
25 Den vindesyge vækker Splid, men den, der stoler paa HERREN, kvæges.
Mtu mwenye tamaa huchochea fitina, bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa.
26 Den, der stoler paa sit Vid, er en Taabe, men den, der vandrer i Visdom, reddes.
Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu, bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama.
27 Hvo Fattigmand giver, skal intet fattes, men mangefold bandes, hvo Øjnene lukker.
Yeye ampaye maskini hatapungukiwa na kitu chochote, bali yeye awafumbiaye maskini macho hupata laana nyingi.
28 Vinder gudløse frem, kryber Folk i Skjul; naar de omkommer, bliver de retfærdige mange.
Wakati waovu watawalapo, watu huenda mafichoni, bali waovu wanapoangamia, wenye haki hufanikiwa.

< Ordsprogene 28 >