< Ordsprogene 14 >
1 Visdom bygger sig Hus, Daarskabs Hænder river det ned.
Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 Hvo redeligt vandrer, frygter HERREN, men den, som gaar Krogveje, agter ham ringe.
Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
3 I Daarens Mund er Ris til hans Ryg, for de vise staar Læberne Vagt.
Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
4 Naar der ikke er Okser, er Laden tom, ved Tyrens Kraft bliver Høsten stor.
Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
5 Sanddru Vidne lyver ikke, det falske Vidne farer med Løgn.
Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
6 Spotter søger Visdom, men finder den ikke, til Kundskab kommer forstandig let.
Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
7 Gaa fra en Mand, som er en Taabe, der mærker du intet til Kundskabs Læber.
Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
8 Den kloge i sin Visdom er klar paa sin Vej, men Taabers Daarskab er Svig.
Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
9 Med Daarer driver Skyldofret Spot, men Velvilje raader iblandt retsindige.
Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
10 Hjertet kender sin egen Kvide, fremmede blander sig ej i dets Glæde.
Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
11 Gudløses Hus lægges øde, retsindiges Telt staar i Blomst.
Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
12 Mangen Vej synes Manden ret, og saa er dens Ende dog Dødens Veje.
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
13 Selv under Latter kan Hjertet lide, og Glædens Ende er Kummer.
Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
14 Af sine Veje mættes den frafaldne, af sine Gerninger den, som er god.
Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
15 Den tankeløse tror hvert Ord, den kloge overtænker sine Skridt.
Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
16 Den vise ængstes og skyr det onde, Taaben buser sorgløs paa.
Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
17 Den hidsige bærer sig taabeligt ad, man hader rænkefuld Mand.
Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
18 De tankeløse giver Daarskab i Arv, de kloge efterlader sig Kundskab.
Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
19 Onde maa bukke for gode, gudløse staa ved retfærdiges Døre.
Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
20 Fattigmand hades endog af sin Ven, men Rigmands Venner er mange.
Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
21 Den, der foragter sin Næste, synder, lykkelig den, der har Medynk med arme.
Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
22 De, som virker ondt, farer visselig vild; de, som virker godt, finder Naade og Trofasthed.
Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
23 Ved al Slags Møje vindes der noget, Mundsvejr volder kun Tab.
Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
24 De vises Krone er Kløgt, Taabers Krans er Daarskab.
Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
25 Sanddru Vidne frelser Sjæle; den, som farer med Løgn, bedrager.
Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
26 Den stærkes Tillid er HERRENS Frygt, hans Sønner skal have en Tilflugt.
Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
27 HERRENS Frygt er en Livsens Kilde, derved undgaas Dødens Snarer.
Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
28 At Folket er stort, er Kongens Hæder, Brist paa Folk er Fyrstens Fald.
Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
29 Den sindige er rig paa Indsigt, den heftige driver det vidt i Daarskab.
Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
30 Sagtmodigt Hjerte er Liv for Legemet, Avind er Edder i Benene.
Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
31 At kue den ringe er Haan mod hans Skaber, han æres ved Medynk med fattige.
Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
32 Ved sin Ondskab styrtes den gudløse, ved lydefri Færd er retfærdige trygge.
Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
33 Visdom bor i forstandiges Hjerte, i Taabers Indre kendes den ikke.
Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
34 Retfærdighed løfter et Folk, men Synd er Folkenes Skændsel.
Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
35 En klog Tjener har Kongens Yndest, en vanartet rammer hans Vrede.
Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.