< Ordsprogene 13 >
1 Viis Søn elsker tugt, spotter hører ikke paa skænd.
Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
2 Af sin Munds Frugt nyder en Mand kun godt, til Vold staar troløses Hu.
Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
3 Vogter man Munden, bevarer man Sjælen, den aabenmundede falder i Vaade.
Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
4 Den lade attraar uden at faa, men flittiges Sjæl bliver mæt.
Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
5 Den retfærdige hader Løgnetale, den gudløse spreder Skam og Skændsel.
Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
6 Retfærd skærmer, hvo lydefrit vandrer, Synden fælder de gudløse.
Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
7 Mangen lader rig og ejer dog intet, mangen lader fattig og ejer dog meget.
Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
8 Mands Rigdom er Løsepenge for hans Liv, Fattigmand faar ingen Trusel at høre.
Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
9 Retfærdiges Lys bryder frem, gudløses Lampe gaar ud.
Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
10 Ved Hovmod vækkes kun Splid, hos dem, der lader sig raade, er Visdom.
Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
11 Rigdom, vundet i Hast, smuldrer hen, hvad der samles Haandfuld for Haandfuld, øges.
Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
12 At bie længe gør Hjertet sygt, opfyldt Ønske er et Livets Træ.
Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
13 Den, der lader haant om Ordet, slaas ned, den, der frygter Budet, faar Løn.
Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
14 Vismands Lære er en Livsens Kilde, derved undgaas Dødens Snarer.
Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
15 God Forstand vinder Yndest, troløses Vej er deres Undergang.
Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
16 Hver, som er klog, gaar til Værks med Kundskab, Taaben udfolder Daarskab.
Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
17 Gudløs Budbringer gaar det galt, troværdigt Bud bringer Lægedom.
Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
18 Afvises Tugt, faar man Armod og Skam; agtes paa Revselse, bliver man æret.
Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
19 Opfyldt Ønske er sødt for Sjælen, at vige fra ondt er Taaber en Gru.
Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
20 Omgaas Vismænd, saa bliver du viis, ilde faren er Taabers Ven.
Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
21 Vanheld følger Syndere, Lykken naar de retfærdige.
Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
22 Den gode efterlader Børnebørn Arv, til retfærdige gemmes Synderens Gods.
Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
23 Paa Fattigfolks Nyjord er rigelig Føde, mens mangen rives bort ved Uret.
Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
24 Hvo Riset sparer, hader sin Søn, den, der elsker ham, tugter i Tide.
Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
25 Den retfærdige spiser, til Sulten er stillet, gudløses Bug er tom.
Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.