< Nehemias 12 >

1 Følgende er Præsterne og Leviter, der drog op med Zerubbabel, Sjealtiels Søn, og Jesua: Seraja, Jirmeja, Ezra,
Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua: Seraya, Yeremia, Ezra,
2 Amarja, Malluk, Hattusj.
Amaria, Maluki, Hatushi,
3 Sjekanja, Harim, Meremot,
Shekania, Rehumu, Meremothi,
4 Iddo, Ginnetoj, Abija,
Ido, Ginethoni, Abiya,
5 Mijjamin, Ma'adja, Bilga,
Miyamini, Moadia, Bilga,
6 Sjemaja, Jojarib, Jedaja,
Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
7 Sallu, Amok, Hilkija og Jedaja. Det var Overhovederne for Præsterne og deres Brødre paa Jesuas Tid.
Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.
8 Leviterne: Jesua, Binnuj, Kadmiel, Sjerebja, Juda, Mattanja, der sammen med sine Brødre forestod Lovsangen,
Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani.
9 medens Bakbukja og Unni sammen med deres Brødre stod over for dem efter deres Afdelinger.
Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.
10 Jesua avlede Jojakim, Jojakim avlede Eljasjib, Eljasjib avlede Jojada,
Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada,
11 Jojada avlede Johanan, og Johanan avlede Jaddua.
Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.
12 Paa Jojakims Tid var Overhovederne for Præsternes Fædrenehuse følgende: Meraja for Seraja, Hananja for Jirmeja,
Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani: wa jamaa ya Seraya, Meraya; wa jamaa ya Yeremia, Hanania;
13 Mesjullam for Ezra, Johanan for Amarja,
wa jamaa ya Ezra, Meshulamu; wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;
14 Jonatan for Malluk, Josef for Sjebanja,
wa jamaa ya Maluki, Yonathani; wa jamaa ya Shebania, Yosefu;
15 Adna for Harim, Helkaj for Merajot,
wa jamaa ya Harimu, Adna; wa jamaa ya Meremothi, Helkai;
16 Zekarja for Iddo, Mesjullam for Ginneton,
wa jamaa ya Ido, Zekaria; wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;
17 Zikri for Abija, .... for Minjamin, Piltaj for Ma'adja,
wa jamaa ya Abiya, Zikri; wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;
18 Sjammua for Bilga, Jonatan for Sjemaja,
wa jamaa ya Bilgai, Shamua; wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;
19 Mattenaj for Jojarib, Uzzi for Jedaja,
wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai; wa jamaa ya Yedaya, Uzi;
20 Kallaj for Sallu, Eber for Amok,
wa jamaa ya Salu, Kalai; wa jamaa ya Amoki, Eberi;
21 Hasjabja for Hilkija og Netan'el for Jedaja.
wa jamaa ya Hilkia, Hashabia; wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.
22 Leviterne: .... . I Eljasjibs, Jojadas, Johanans og Jadduas Dage optegnedes Overhovederne for Fædrenehusene og Præsterne indtil Perseren Darius's Regering.
Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi.
23 Af Levis Efterkommere optegnedes Overhovederne for Fædrenehusene i Krønikebogen ned til Johanans, Eljasjibs Søns, Dage.
Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu.
24 Og Leviternes Overhoveder var: Hasjabja, Sjerebja, Jesua, Binnuj, Kadmiel og deres Brødre, der stod over for dem for at synge Lovsangen og Takkesangen efter den Guds Mand Davids Bud, den ene Afdeling efter den anden;
Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.
25 og Mattanja, Bakbukja og Obadja, Mesjullam, Talmon og Akkub var Dørvogtere og holdt Vagt ved Portenes Forraadskamre.
Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu.
26 Disse var Overhoveder paa Jojakims Tid, en Søn af Jesua, en Søn af Jozadak, og paa Statholderen Nehemias's og Præsten Ezra den Skriftlærdes Tid.
Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.
27 Da Jerusalems Mur skulde indvies, opsøgte man Leviterne alle Vegne, hvor de boede, og bragte dem til Jerusalem, for at de skulde fejre Indvielsen med Fryd og Takkesang, med Sang, Cymbler, Harper og Citre.
Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze.
28 Da samledes Sangerne fra Egnen om Jerusalem og fra Netofatiternes Landsbyer,
Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi,
29 fra Bet-Gilgal, fra Gebas og Azmavets Marker; thi Sangerne havde bygget sig Landsbyer rundt om Jerusalem.
kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu.
30 Da Præsterne og Leviterne havde renset sig, rensede de Folket, Portene og Muren.
Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.
31 Saa lod jeg Judas Øverster stige op paa Muren og opstillede to store Lovprisningstog. Det ene drog til højre oven paa Muren ad Møgporten til,
Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi.
32 og med det fulgte Hosjaja og den ene Halvdel af Judas Øverster;
Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata,
33 dernæst nogle af Præsterne med Trompeter, Azarja, Ezra, Mesjullam,
pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu,
34 Juda, Benjamin, Sjemaja og Jirmeja;
Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia,
35 endvidere Zekarja, en Søn af Jonatan, en Søn af Sjemaja, en Søn af Mattanja, en Søn af Mika, en Søn af Zakkur, en Søn af Asaf,
pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu,
36 og hans Brødre Sjemaja, Azar'el, Milalaj, Gilalaj, Ma'aj, Netan'el, Juda, Hanani med den Guds Mand Davids Musikinstrumenter, med Ezra den Skriftlærde i Spidsen;
pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano.
37 og de gik over Kildeporten; derpaa gik de lige ud op ad Trinene til Davidsbyen, ad Opgangen paa Muren oven for Davids Palads hen til Vandporten mod Øst.
Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.
38 Det andet Lovprisningstog, hvor jeg og den anden Halvdel af Folkets Øverster var med, drog til venstre oven paa Muren, over Ovntaarnet til den brede Mur
Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana,
39 og videre over Efraimsporten, den gamle Port, Fiskeporten, Hanan'eltaarnet og Meataarnet til Faareporten og stillede sig op i Fængselsporten.
juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.
40 Derpaa stillede de to Lovprisningstog sig op i Guds Hus, jeg sammen med Halvdelen af Øversterne
Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa,
41 og Præsterne Eljakim, Ma'aseja, Minjamin, Mika, Eljoenaj, Zekarja, Hananja med Trompeter,
na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao,
42 endvidere Ma'aseja, Sjemaja, El'azar, Uzzi, Johanan, Malkija, Elam og Ezer. Og Sangerne stemte i, ledede af Jizraja.
na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia.
43 Paa den Dag ofrede de store Slagtofre og var glade, thi Gud havde bragt dem stor Glæde; ogsaa Kvinderne og Børnene var glade; og Glæden i Jerusalem hørtes langt bort.
Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.
44 Paa den Dag indsattes der Mænd til at have Tilsyn med de Kamre, der brugtes til Forraadene, Offerydelserne, Førstegrøden og Tienden, for i dem at opsamle de i Loven foreskrevne Afgifter til Præsterne og Leviterne fra de forskellige Bymarker, thi Juda glædede sig over Præsterne og Leviterne, der gjorde Tjeneste;
Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi.
45 og disse tog Vare paa, hvad der var at varetage for deres Gud og ved Renselsen, ligesom ogsaa Sangerne og Dørvogterne gjorde deres Gerning efter Davids og hans Søn Salomos Bud.
Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe.
46 Thi allerede paa Davids Tid var Asaf Leder for Sangerne og for Lov— og Takkesangene til Gud.
Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu.
47 Hele Israel gav paa Zerubbabels og Nehemias's Tid Afgifter til Sangerne og Dørvogterne, efter som det krævedes Dag for Dag; og de gav Leviterne Helliggaver, og Leviterne gav Arons Sønner Helliggaver.
Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.

< Nehemias 12 >