< Mikas 3 >
1 Da sagde jeg: Hør dog, I Jakobs Høvdinger, I Dommere af Israels Hus! Kan Kendskab til Ret ej ventes af eder,
Kisha nikasema, “Sikilizeni enyi viongozi wa Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli. Je, hampaswi kujua hukumu,
2 I, som hader det gode og elsker det onde, I, som flaar Huden af Folk og Kødet af deres Ben,
ninyi mnaochukia mema na kupenda maovu; ninyi mnaowachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao;
3 æder mit Folks Kød og flænger dem Huden af Kroppen, sønderbryder deres Ben og breder dem som Kød i en Gryde, som Suppekød i en Kedel?
ninyi mnaokula nyama ya watu wangu, mnaowachuna ngozi na kuvunja mifupa yao vipande vipande; mnaowakatakata kama nyama ya kuwekwa kwenye sufuria na kama nyama ya kuwekwa kwenye chungu?”
4 Engang skal de raabe til HERREN, han lader dem uden Svar; da skjuler han sit Aasyn for dem, fordi deres Gerninger er onde.
Kisha watamlilia Bwana, lakini hatawajibu. Wakati huo atawaficha uso wake kwa sababu ya uovu waliotenda.
5 Saa siger HERREN om Profeterne, de, som vildleder mit Folk, de, som raaber om Fred, naar kun de faar noget at tygge, men ypper Krig med den, der intet giver dem i Munden:
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu, mtu akiwalisha, wanatangaza ‘amani’; kama hakufanya hivyo, wanaandaa kupigana vita dhidi yake.
6 Derfor skal I opleve Nat uden Syner, Mørke, som ej bringer Spaadom; Solen skal gaa ned for Profeterne, Dagen skal sortne for dem.
Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono, na giza, msiweze kubashiri. Jua litawachwea manabii hao, nao mchana utakuwa giza kwao.
7 Til Skamme skal Seeren blive, blues skal de, som spaar; alle skal tilhylle Skægget, thi Svar er der ikke fra Gud.
Waonaji wataaibika na waaguzi watafedheheka. Wote watafunika nyuso zao kwa sababu hakuna jibu litokalo kwa Mungu.”
8 Jeg derimod er ved HERRENS Aand fuld af Styrke, af Ret og af Kraft til at forkynde Jakob dets Brøde, Israel, hvad det har syndet.
Lakini kuhusu mimi, nimejazwa nguvu, nimejazwa Roho wa Bwana, haki na uweza, kumtangazia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
9 Hør det, I Jakobs Huses Høvdinger, I Dommere af Israels Hus, I, som afskyr Ret og gør alt, som er lige, kroget,
Sikieni hili, enyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli, mnaodharau haki na kupotosha kila lililo sawa;
10 som bygger Zion med Blod og Jerusalem med Uret.
mnaojenga Sayuni kwa kumwaga damu na Yerusalemu kwa uovu.
11 Dets Høvdinger dømmer for Gave, dets Præster kender Ret for Løn; dets Profeter spaar for Sølv og støtter sig dog til HERREN: »Er HERREN ej i vor Midte? Over os kommer intet ondt.«
Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa, na makuhani wake wanafundisha kwa malipo, nao manabii wake wanatabiri kwa fedha. Hata hivyo wanamwegemea Bwana na kusema, “Je, Bwana si yumo miongoni mwetu? Hakuna maafa yatakayotupata.”
12 For eders Skyld skal derfor Zion pløjes som en Mark, Jerusalem blive til Grushobe, Tempelbjerget til Krathøj.
Kwa hiyo kwa sababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.