< 3 Mosebog 10 >
1 Men Arons Sønner Nadab og Abihu tog hver sin Pande, kom Ild i dem og lagde Røgelse derpaa og frembar for HERRENS Aasyn fremmed Ild, som han ikke havde paalagt dem.
Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua vyetezo vyao, wakaweka moto ndani yake na kuongeza uvumba; kisha wakamtolea Bwana moto usio halali, kinyume na agizo la Mungu.
2 Da for Ild ud fra HERRENS Aasyn og fortærede dem, saa de døde for HERRENS Aasyn.
Hivyo moto ukaja kutoka kwa uwepo wa Bwana na kuwaramba, nao wakafa mbele za Bwana.
3 Moses sagde da til Aron: »Det er det, HERREN talede om, da han sagde: Jeg viser min Hellighed paa dem, der staar mig nær, og min Herlighed for alt Folkets Øjne!« Og Aron tav.
Kisha Mose akamwambia Aroni, “Hili ndilo alilonena Bwana wakati aliposema: “‘Miongoni mwa wale watakaonikaribia nitajionyesha kuwa mtakatifu; machoni pa watu wote nitaheshimiwa.’” Aroni akanyamaza.
4 Da kaldte Moses Misjael og Elzafan, Arons Farbroder, Uzziels Sønner, til sig og sagde til dem: »Kom og bær eders Frænder bort fra Helligdommen uden for Lejren!«
Mose akawaita Mishaeli na Elisafani, wana wa Uzieli mjomba wake Aroni, akawaambia, “Njooni hapa. Ondoeni miili ya binamu zenu mbele ya mahali patakatifu, mkaipeleke nje ya kambi.”
5 Og de kom og bar dem uden for Lejren i deres Kjortler, som Moses havde sagt.
Hivyo wakaja na kuwaondoa, wakiwa bado wamevalia makoti yao ya ibada, wakawapeleka nje ya kambi, kama Mose alivyoamuru.
6 Men Moses sagde til Aron og hans Sønner Eleazar og Itamar: »I maa hverken lade eders Haar vokse frit eller sønderrive eders Klæder, ellers skal I dø og Vrede komme over hele Menigheden; lad eders Brødre, hele Israels Hus, begræde den Brand, HERREN har antændt;
Ndipo Mose akamwambia Aroni pamoja na wanawe, Eleazari na Ithamari, “Msifunue vichwa vyenu wala msirarue mavazi yenu, la sivyo mtakufa na Bwana ataikasirikia jumuiya nzima. Lakini ndugu zenu, nyumba yote ya Israeli, wanaweza kuwaombolezea wale ambao Bwana amewaangamiza kwa moto.
7 og vig ikke fra Aabenbaringsteltets Indgang, ellers skal I dø, thi HERRENS Salveolie er paa eder!« Og de gjorde som Moses sagde.
Msitoke nje ya ingilio la Hema la Kukutania, la sivyo mtakufa, kwa sababu mafuta ya Bwana ya upako yako juu yenu.” Hivyo wakafanya kama vile Mose alivyosema.
8 Og HERREN talede til Aron og sagde:
Kisha Bwana akamwambia Aroni,
9 Vin og stærk Drik maa hverken du eller dine Sønner drikke, naar I gaaet ind i Aabenbaringsteltet, for at I ikke skal dø. Det skal være eder en evig gyldig Anordning fra Slægt til Slægt,
“Wewe na wanao msinywe mvinyo wala kinywaji kingine kilichochachuka wakati mwingiapo katika Hema la Kukutania, la sivyo mtakufa. Hili litakuwa Agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo.
10 for at I kan gøre Skel mellem det hellige og det, der ikke er helligt, og mellem det urene og det rene,
Ni lazima mtenganishe kilicho kitakatifu na kile kilicho cha kawaida, kati ya yaliyo najisi na yaliyo safi,
11 og for at I kan vejlede Israeliterne i alle de Love, HERREN har kundgjort dem ved Moses.
na lazima mwafundishe Waisraeli amri zote ambazo Bwana aliwapa kupitia Mose.”
12 Og Moses sagde til Aron og hans tilbageblevne Sønner Eleazar og Itamar: »Tag Afgrødeofferet, der er levnet fra HERRENS Ildoffer, og spis det usyret ved Siden af Alteret, thi det er højhelligt;
Mose akamwambia Aroni pamoja na wanawe waliosalia, Eleazari na Ithamari, “Chukueni sadaka ya nafaka iliyobaki kutoka sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, muile hapo kando ya madhabahu ikiwa imeandaliwa bila chachu, kwa sababu ni takatifu sana.
13 I skal spise det paa et helligt Sted; det er jo din og dine Sønners retmæssige Del af HERRENS Ildofre; thi saaledes er det mig paabudt.
Mtaila katika mahali patakatifu kwa sababu ni fungu lenu na fungu la wana wenu la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, kwa maana hivyo ndivyo nilivyoamriwa.
14 Og Svingningsbrystet og Offerydelseskøllen skal I spise paa et rent Sted, du, dine Sønner og Døtre, thi de er givet dig tillige med dine Sønner som en retmæssig Del af Israeliternes Takofre;
Lakini wewe na wanao na binti zako mwaweza kula kidari kile kilichoinuliwa na paja lile lililotolewa. Mtavila mahali safi pa kawaida ya ibada; mmepewa wewe na watoto wako kuwa fungu lenu la sadaka za amani za Waisraeli.
15 Offerydelseskøllen og Svingningsbrystet skal man frembære sammen med de til Ildofre bestemte Fedtdele, for at Svingningen kan udføres for HERRENS Aasyn, og de skal tilfalde dig og dine Sønner tillige med dig som en evig gyldig Rettighed, saaledes som HERREN har paabudt!«
Paja lile lililotolewa na kidari kile kilichoinuliwa lazima viletwe pamoja na sehemu za mafuta ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, ili kuinuliwa mbele za Bwana kama sadaka ya kuinuliwa. Hili litakuwa fungu lako la kawaida na wanao, kama Bwana alivyoagiza.”
16 Og Moses spurgte efter Syndofferbukken, men se, den var opbrændt. Da blev han fortørnet paa Eleazar og Itamar, Arons tilbageblevne Sønner, og sagde:
Mose alipouliza kuhusu mbuzi atolewaye kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kukuta kwamba ameteketezwa, aliwakasirikia Eleazari na Ithamari, wana wa Aroni waliobaki, akawauliza,
17 »Hvorfor har I ikke spist Syndofferet paa det hellige Sted? Det er jo dog højhelligt, og han har givet eder det, for at I skal borttage Menighedens Skyld og saaledes skaffe dem Soning for HERRENS Aasyn.
“Kwa nini hamkula sadaka ya dhambi katika eneo la mahali patakatifu? Ni takatifu sana. Mlipewa ninyi ili kuondoa hatia ya jumuiya kwa ajili ya kuwafanyia upatanisho mbele za Bwana.
18 Se, Blodet deraf er ikke blevet bragt ind i Helligdommens Indre, derfor havde det været eders Pligt at spise det paa det hellige Sted, saaledes som jeg har paabudt!«
Kwa kuwa damu yake haikuletwa ndani ya Mahali Patakatifu, mngemla mbuzi huyo katika sehemu ya mahali patakatifu kama nilivyoagiza.”
19 Men Aron svarede Moses: »Se, de har i Dag frembaaret deres Syndoffer og Brændoffer for HERRENS Aasyn, og en saadan Tilskikkelse har ramt mig! Om jeg i Dag havde spist Syndofferkød, vilde HERREN da have billiget det?«
Aroni akamjibu Mose, “Leo wanangu wametoa sadaka zao za dhambi na sadaka zao za kuteketezwa mbele za Bwana, lakini mambo kama haya yamenitokea mimi. Je, Bwana angependezwa kama ningekuwa nimekula sadaka ya dhambi leo?”
20 Da Moses hørte dette, billigede han det.
Mose aliposikia haya, akaridhika.