< Josua 4 >

1 Da nu hele Folket havde tilendebragt Overgangen over Jordan, sagde HERREN til Josua:
Wakati taifa lote lilipokwisha kuvuka Mto Yordani, Bwana akamwambia Yoshua,
2 »Vælg eder tolv Mænd af Folket, een Mand af hver Stamme,
“Chagua watu kumi na wawili miongoni mwa watu, kila kabila mtu mmoja,
3 og byd dem: Tag eder tolv Sten her, midt i Jordan, hvor Præsterne stod stille, bring dem med over og stil dem paa den Plads, hvor I holder Rast i Nat!«
nawe uwaambie wachukue mawe kumi na mawili katikati ya Mto Yordani, palepale makuhani waliposimama, wayachukue na kuyaweka mahali mtakapokaa usiku huu wa leo.”
4 Saa lod Josua de tolv Mænd kalde, som han havde til Rede af Israeliterne, een Mand af hver Stamme;
Basi Yoshua akawaita watu kumi na wawili ambao alikuwa amewachagua kutoka miongoni mwa Waisraeli, mtu mmoja kutoka kila kabila,
5 og Josua sagde til dem: »Gaa foran HERREN eders Guds Ark midt ud i Jordan, og tag saa hver en Sten paa Skulderen, svarende til Tallet paa Israeliternes Stammer,
naye akawaambia, “Mtangulie mbele ya Sanduku la Bwana Mungu wenu, mwende katikati ya Mto Yordani. Kila mmoja wenu atainua jiwe begani mwake, kufuatana na hesabu ya makabila ya Waisraeli,
6 for at det kan tjene til Tegn iblandt eder. Naar eders Børn i Fremtiden spørger: Hvad Betydning har disse Sten for eder?
kuwa kama ishara katikati yenu. Siku zijazo, wakati watoto wenu watakapowauliza, ‘Ni nini maana ya mawe haya?’
7 saa skal I sige til dem: De betyder, at Jordans Vand standsede foran HERRENS Pagts Ark; da den drog over Jordan, standsede Jordans Vand. Og disse Sten skal være Israeliterne et Mindetegn til evig Tid!«
waambieni kwamba maji ya Mto Yordani yaliyokuwa yakitiririka yalitindika mbele ya Sanduku la Agano la Bwana. Wakati lilipovuka Yordani, maji ya Yordani yalitindika. Mawe haya yatakuwa kumbukumbu kwa watu wa Israeli milele.”
8 Da gjorde Israeliterne, som Josua bød, og tog tolv Sten midt i Jordan, som HERREN havde sagt til Josua, svarende til Tallet paa Israeliternes Stammer, og de bragte dem med over til det Sted, hvor de holdt Rast, og stillede dem der.
Hivyo Waisraeli wakafanya kama Yoshua alivyowaagiza. Wakachukua mawe kumi na mawili kutoka katikati ya Mto Yordani, kulingana na hesabu ya kabila za Waisraeli kama Bwana alivyomwambia Yoshua, nao wakayabeba hadi kambini mwao, mahali walipoyatua chini.
9 Og tolv Sten rejste Josua midt i Jordan paa det Sted, hvor Præsterne, som bar Pagtens Ark, stod stille, og der staar de den Dag i Dag.
Yoshua akayasimamisha yale mawe kumi na mawili ambayo yalikuwa katikati ya Mto Yordani, mahali pale ambapo miguu ya makuhani waliobeba Sanduku la Agano iliposimama. Nayo yako huko mpaka leo.
10 Men Præsterne, som bar Arken, blev staaende midt i Jordan, indtil alt, hvad HERREN havde paalagt Josua at sige til Folket, var udført, i Overensstemmelse med alt, hvad Moses havde paalagt Josua; og Folket gik skyndsomt over.
Makuhani waliobeba lile Sanduku walibakia wakiwa wamesimama katikati ya Mto Yordani mpaka kila kitu Bwana alichomwamuru Yoshua kilipokuwa kimefanywa na watu, sawasawa na vile Mose alivyokuwa amemwamuru Yoshua. Watu wakafanya haraka kuvuka,
11 Da hele Folket saa havde tilendebragt Overgangen, gik HERRENS Ark og Præsterne over og stillede sig foran Folket.
na mara tu watu wote walipokwisha kuvuka, Sanduku la Bwana na makuhani wakavuka watu wakiwa wanatazama.
12 Og Rubeniterne, Gaditerne og Manasses halve Stamme drog væbnet over i Spidsen for Israeliterne, som Moses havde sagt til dem;
Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakavuka mbele ya Waisraeli, wakiwa wamevaa silaha, kama Mose alivyowaamuru.
13 henved 40 000 Mand i Tal, rustede til Strid, drog de foran HERREN over til Jerikos Sletter til Kamp.
Kiasi cha watu 40,000 waliojiandaa kwa vita walivuka mbele za Bwana hadi nchi tambarare za Yeriko kwa ajili ya vita.
14 Paa den Dag gjorde HERREN Josua stor i hele Israels Øjne, og de frygtede ham alle hans Livs Dage, som de havde frygtet Moses.
Siku ile Bwana akamtukuza Yoshua mbele ya Israeli yote, nao wakamheshimu siku zote za maisha yake, kama vile walivyomheshimu Mose.
15 Da sagde HERREN til Josua:
Basi Bwana akamwambia Yoshua,
16 »Byd Præsterne, som bærer Vidnesbyrdets Ark, at stige op fra Jordan!«
“Waamuru hao makuhani wanaolibeba Sanduku la Ushuhuda, wapande kutoka ndani ya Mto Yordani.”
17 Og Josua bød Præsterne: »Stig op fra Jordan!«
Kwa hiyo Yoshua akawaamuru hao makuhani akisema, “Pandeni kutoka ndani ya Mto Yordani.”
18 Saa steg Præsterne, som bar HERRENS Pagts Ark, op fra Jordan, og næppe havde deres Fødder betraadt det tørre Land, før Jordans Vand vendte tilbage til sit Leje og overalt gik over sine Bredder som før.
Nao makuhani wakapanda kutoka ndani ya Mto Yordani wakilibeba hilo Sanduku la Agano la Bwana. Mara tu walipoiweka miguu yao penye kingo, nje ya mto, maji ya Yordani yakarudi kufurika kama ilivyokuwa kabla.
19 Og Folket steg op fra Jordan den tiende Dag i den første Maaned og slog Lejr i Gilgal ved Østenden af Jerikolandet.
Siku ya kumi ya mwezi wa kwanza watu walipanda kutoka Yordani na kupiga kambi huko Gilgali, kwenye mpaka wa mashariki ya Yeriko.
20 Men de tolv Sten, som de havde taget op fra Jordan, rejste Josua i Gilgal,
Naye Yoshua akayasimamisha huko Gilgali yale mawe kumi na mawili ambayo walikuwa wameyachukua katikati ya Mto Yordani.
21 og han sagde til Israeliterne: »Naar eders Børn i Fremtiden spørger deres Fædre: Hvad betyder disse Sten?
Akawaambia Waisraeli, “Wazao wenu watakapowauliza baba zao siku zijazo wakisema, ‘Mawe haya maana yake ni nini?’
22 saa skal I fortælle eders Børn det og sige: Paa tør Bund gik Israel over Jordan derhenne;
Basi waambieni, ‘Israeli ilivukia mahali pakavu katika Mto Yordani.’
23 thi HERREN eders Gud lod Jordans Vand tørre bort foran eder, indtil I var kommet over, ligesom HERREN eders Gud gjorde med det røde Hav, som han lod tørre bort foran os, indtil vi var kommet over,
Kwa maana Bwana Mungu wenu alikausha maji ya Yordani mbele yenu, hadi mlipomaliza kuvuka. Bwana Mungu wenu alifanya haya kwa Mto Yordani sawasawa na kile alichoifanyia Bahari ya Shamu wakati alipoikausha mbele yetu hadi tulipomaliza kuvuka.
24 for at alle Jordens Folk skal kende, at HERRENS Arm er stærk, at de maa frygte HERREN eders Gud alle Dage.«
Alifanya hivi ili kwamba mataifa yote ya dunia yapate kujua kuwa mkono wa Bwana ni wenye nguvu, na ili kwamba kila wakati mpate kumcha Bwana Mungu wenu.”

< Josua 4 >