< Josua 18 >
1 Hele Israeliternes Menighed kom sammen i Silo, og de rejste Aabenbaringsteltet der, da de nu havde underlagt sig Landet.
Kusanyiko lote la Waisraeli likakusanyika huko Shilo na kusimamisha Hema la Kukutania. Nchi ikawa chini ya utawala wao,
2 Men der var endnu syv Stammer tilbage af Israeliterne, som ikke havde faaet deres Arvelod tildelt.
lakini palikuwa bado makabila saba ya Israeli ambayo yalikuwa hayajapokea urithi wao.
3 Josua sagde derfor til Israeliterne: »Hvor længe vil I endnu nøle med at drage hen og tage det Land i Besiddelse, som HERREN, eders Fædres Gud, har givet eder?
Hivyo Yoshua akawaambia Waisraeli, “Je, mtasubiri hata lini ili kuingia kumiliki nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa?
4 Udse eder tre Mænd af hver Stamme, som jeg kan udsende; de skal gøre sig rede og drage Landet rundt og affatte en Beskrivelse derover til Brug ved Fastsættelsen af deres Arvelod og saa komme tilbage til mig.
Chagueni watu watatu kutoka kwenye kila kabila. Nitawatuma hao watu kukagua hiyo nchi na kuniandikia mapendekezo ya mgawanyo wa urithi wa kila kabila. Nao watanirudia.
5 De skal dele det i syv Dele; Juda skal beholde sit Omraade mod Syd og Josefs Slægt sit mod Nord.
Mtaigawanya hiyo nchi katika sehemu saba. Yuda atabaki katika eneo lake upande wa kusini na nyumba ya Yosefu katika nchi yake upande wa kaskazini.
6 Og I skal saa affatte en Beskrivelse over Landet, delt i syv Dele, og bringe mig den; saa vil jeg kaste Lod for eder her for HERREN vor Guds Aasyn.
Baada ya kuandika maelezo ya hizo sehemu saba za nchi, yaleteni kwangu, nami nitawapigia kura kwa kura mbele za Bwana Mungu wetu.
7 Thi Leviterne faar ingen Del iblandt eder, da HERRENS Præstedømme er deres Arvelod; og Gad, Ruben og Manasses halve Stamme har paa Jordans Østside faaet deres Arvelod, som HERRENS Tjener Moses gav dem!«
Hata hivyo, Walawi hawatakuwa na sehemu miongoni mwenu, kwa maana huduma ya ukuhani kwa Bwana ndio urithi wao. Nao Gadi, Reubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapata urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, ambako Mose mtumishi wa Bwana aliwapa.”
8 Da begav Mændene sig paa Vej; og Josua bød de bortdragende affatte en Beskrivelse over Landet, idet han sagde: »Drag Landet rundt, affat en Beskrivelse over det og kom saa tilbage til mig; saa vil jeg kaste Lod for eder her for HERRENS Aasyn i Silo!«
Watu hao walipokuwa wanaondoka kwenda kuandika vizuri kuhusu hiyo nchi, Yoshua akawaagiza, “Nendeni mkakague hiyo nchi na mwandike maelezo kuihusu. Kisha mrudi kwangu, nami nitawapigia kura hapa Shilo mbele za Bwana.”
9 Saa begav, Mændene sig paa Vej og drog igennem Landet og affattede en Beskrivelse derover, By for By, i syv Dele; og derpaa kom de tilbage til Josua i Lejren ved Silo.
Ndipo hao watu walipoondoka na kupita katika ile nchi. Wakaandika maelezo yake kwenye kitabu, mji kwa mji, katika sehemu saba na kurudisha taarifa kwa Yoshua huko kambini Shilo.
10 Men Josua kastede Lod for dem i Silo for HERRENS Aasyn og udskiftede der Landet til Israeliterne, Afdeling, for Afdeling.
Basi Yoshua akawapigia kura huko Shilo mbele za Bwana, na hapo akagawanya ile nchi kwa Waisraeli kufuatana na mgawanyo wa kabila zao.
11 Da faldt Loddet for Benjaminiternes Stamme efter deres Slægter; og det Omraade, der blev deres Lod, kom til at ligge mellem Judas og Josefs Sønner.
Kura iliangukia kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo. Eneo lao walilogawiwa lilikuwa kati ya kabila la Yuda na la Yosefu.
12 Deres Nordgrænse begynder ved Jordan, og Grænsen strækker sig op til Bjergryggen norden for Jeriko og mod Vest op i Bjerglandet, saa den ender i Bet-Avens Ørken;
Upande wa kaskazini mpaka wao ulianzia pale Yordani, kupitia kaskazini ya mteremko wa Yeriko na kuendelea magharibi kuingia katika nchi ya vilima, ukitokea kwenye jangwa la Beth-Aveni.
13 derfra gaar Grænsen videre til Luz, til Bjergryggen sønden for Luz, det er Betel, og strækker sig ned til Atarot-Addar over Bjerget sønden for Nedre-Bet-Horon.
Kutoka hapo ulikatiza kwenye mteremko wa kusini mwa Luzu (yaani Betheli) na kushuka hadi Ataroth-Adari katika kilima kusini mwa Beth-Horoni ya Chini.
14 Derpaa bøjer Grænsen om og løber som Vestgrænse sydpaa fra Bjerget lige sønden for Bet-Horon og ender ved Kirjat-Ba'al, det er den judæiske By Kirjat-Jearim; det er Vestgrænsen.
Kutoka kilima kinachotazamana na Beth-Horoni upande wa kusini mpaka ule ukazunguka kusini kufuatia upande wa magharibi, na ukatokezea Kiriath-Baali (yaani Kiriath-Yearimu), mji wa watu wa Yuda. Huu ndio uliokuwa upande wa magharibi.
15 Sydgrænsen begynder ved Udkanten af Kirjat-Ba'al, og Grænsen gaar til Neftoas Vandkilde;
Upande wa kusini mpaka ulianzia kwenye viunga vya Kiriath-Yearimu kwa upande wa magharibi, nao ukatokeza kwenye chemchemi ya maji ya Neftoa.
16 derpaa strækker den sig ned til Randen af Bjerget lige over for Hinnoms Søns Dal norden for Refaimdalen og videre til Hinnoms Dal sønden om Jebusiternes Bjergryg og til Rogelkilden;
Mpaka ukateremka hadi shefela inayotazamana na Bonde la Ben-Hinomu, kaskazini mwa Bonde la Refaimu. Ukaendelea chini kwenye Bonde la Hinomu sambamba na mteremko wa kusini mwa mji mkubwa wa Wayebusi na kisha hadi En-Rogeli.
17 saa drejer den nordpaa og fortsætter til Sjemesjkilden og videre til Gelilot lige over for Adummimpasset, derpaa ned til Rubens Søn Bohans Sten
Kisha ukapinda kuelekea kaskazini, ukaenda hadi En-Shemeshi na kuendelea mpaka Gelilothi, inayotazamana na Njia ya Adumimu, ukateremka hadi kwenye Jiwe la Bohani mwana wa Reubeni.
18 og gaar saa videre til Bjergryggen norden for Bet-Araba og ned i Arabalavningen;
Ukaendelea upande wa mteremko wa kaskazini wa Beth-Araba ukateremka hadi Araba.
19 saa gaar den videre til Bjergryggen norden for Bet-Hogla og ender norden for Salthavets Bugt ved Jordans Udløb; det er Sydgrænsen.
Kisha ukaenda mpaka kwenye mteremko wa kaskazini wa Beth-Hogla na kujitokeza kwenye ghuba ya kaskazini ya Bahari ya Chumvi, kwenye maingilio ya Yordani upande wa kusini. Huo ulikuwa mpaka wa kusini.
20 Mod Øst danner Jordan Grænse. Det er Benjaminiternes Arvelod med dens Grænser efter deres Slægter.
Nayo Yordani ikawa ndio mpaka wa upande wa mashariki. Hii ilikuwa ndiyo mipaka iliyoonyesha urithi wa koo za Benyamini pande zote.
21 Og Benjaminiternes Stammes Byer efter deres Slægter er følgende: Jeriko, Bet-Hogla, Emek-Keziz,
Kabila ya Benyamini, ukoo kwa ukoo, ilikuwa na miji mikubwa ifuatayo: Yeriko, Beth-Hogla, Emeki-Kesisi,
22 Bet-Araba, Zemarajim, Betel,
Beth-Araba, Semaraimu, Betheli,
24 Kefar-Ammoni, Ofni og Geba; tilsammen tolv Byer med Landsbyer.
Kefar-Amoni, Ofni, na Geba; miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
25 Gibeon, Rama, Be'erot,
Gibeoni, Rama na Beerothi,
27 Rekem, Jirpe'el, Tar'ala,
Rekemu, Irpeeli, Tarala,
28 Zela, Elef, Jebus, det er Jerusalem, Gibeat og Kirjat-Jearim; tilsammen fjorten Byer med Landsbyer. Det er Benjaminiternes Arvelod efter deres Slægter.
Zela, Elefu, mji wa Wayebusi (yaani Yerusalemu), Gibea na Kiriathi; miji kumi na minne pamoja na vijiji vyake. Huu ndio uliokuwa urithi wa Benyamini kwa ajili ya koo zake.