< Job 8 >
1 Saa tog Sjuhiten Bildad til Orde og sagde:
Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
2 Hvor længe taler du saa, hvor længe skal Mundens Uvejr rase?
“hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
3 Mon Gud vel bøjer Retten, bøjer den Almægtige Retfærd?
Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
4 Har dine Sønner syndet imod ham, og gav han dem deres Brøde i Vold,
Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
5 saa søg du nu hen til Gud og bed hans Almagt om Naade!
Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
6 Saafremt du er ren og oprigtig, ja, da vil han vaage over dig, genrejse din Retfærds Bolig;
Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
7 din fordums Lykke vil synes ringe, saare stor skal din Fremtid blive.
Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
8 Thi spørg dog den henfarne Slægt, læg Mærke til Fædrenes Granskning!
Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
9 Vi er fra i Gaar, og intet ved vi, en Skygge er vore Dage paa Jord.
(Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
10 Mon ej de kan lære dig, sige dig det og give dig Svar af Hjertet:
Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
11 Vokser der Siv, hvor der ikke er Sump, gror Nilgræs frem, hvor der ikke er Vand?
Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
12 Endnu i Grøde, uden at høstes, visner det før alt andet Græs.
Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
13 Saa gaar det enhver, der glemmer Gud, en vanhelligs Haab slaar fejl:
Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
14 som Sommerspind er hans Tilflugt, hans Tillid er Spindelvæv;
Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
15 han støtter sig til sit Hus, det falder, han klynger sig til det, ej staar det fast.
Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
16 I Solskinnet vokser han frodigt, hans Ranker breder sig Haven over,
Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
17 i Stendynger fletter hans Rødder sig ind, han hager sig fast mellem Sten;
Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
18 men rives han bort fra sit Sted, fornægter det ham: »Jeg har ikke set dig!«
Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
19 Se, det er Glæden, han har af sin Vej, og af Jorden fremspirer en anden!
Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
20 Se, Gud agter ej den uskyldige ringe, han holder ej fast ved de ondes Haand.
Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
21 End skal han fylde din Mund med Latter og dine Læber med Jubel;
Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
22 dine Avindsmænd skal klædes i Skam og gudløses Telt ej findes mer!
Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.