< Job 33 >

1 Men hør nu Job, paa min Tale og lyt til alle mine Ord!
“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
2 Se, jeg har aabnet min Mund, min Tunge taler i Ganen;
Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
3 mine Ord er talt af oprigtigt Hjerte, mine Læber fører lutret Tale.
Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
4 Guds Aand har skabt mig, den Almægtiges Aande har givet mig Liv.
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
5 Svar mig, i Fald du kan, rust dig imod mig, mød frem!
Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
6 Se, jeg er din Lige for Gud, ogsaa jeg er taget af Ler;
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
7 Rædsel for mig skal ikke skræmme dig, min Haand skal ej ligge tyngende paa dig.
Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
8 Dog, det har du sagt i mit Paahør, jeg hørte saa lydende Ord:
“Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
9 »Jeg er ren og uden Brøde, lydeløs, uden Skyld;
‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
10 men han søger Paaskud imod mig, regner mig for sin Fjende;
Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
11 han lægger mine Fødder i Blokken, vogter paa alle mine Veje.«
Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
12 Se, der har du Uret, det er mit Svar, thi Gud er større end Mennesket.
“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
13 Hvorfor tvistes du med ham, fordi han ej svarer paa dine Ord?
Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
14 Thi paa een Maade taler Gud, ja paa to, men man ænser det ikke:
Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
15 I Drømme, i natligt Syn, naar Dvale falder paa Mennesker, naar de slumrende hviler paa Lejet;
Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
16 da aabner han Menneskers Øre, gør dem angst med Skræmmebilleder
anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
17 for at faa Mennesket bort fra Uret og udrydde Hovmod af Manden,
ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
18 holde hans Sjæl fra Graven, hans Liv fra Vaabendød.
kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
19 Eller han revses med Smerter paa Lejet, uafbrudt staar der Kamp i hans Ben;
Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
20 Livet i ham væmmes ved Brød og hans Sjæl ved lækker Mad;
kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
21 hans Kød svinder hen, saa det ikke ses, hans Knogler, som før ikke saas, bliver blottet;
Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
22 hans Sjæl kommer Graven nær, hans Liv de dræbende Magter.
Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
23 Hvis da en Engel er paa hans Side, een blandt de tusind Talsmænd, som varsler Mennesket Tugt,
“Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
24 og den viser ham Naade og siger: »Fri ham fra at synke i Graven, Løsepenge har jeg faaet!«
kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
25 da svulmer hans Legem af Friskhed, han oplever atter sin Ungdom.
ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
26 Han beder til Gud, og han er ham naadig, han skuer med Jubel hans Aasyn, fortæller Mennesker om sin Frelse.
Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
27 Han synger det ud for Folk: »Jeg synded og krænkede Retten og fik dog ej Løn som forskyldt!
Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
28 Han har friet min Sjæl fra at fare i Grav, mit Liv ser Lyset med Lyst!«
Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
29 Se, alle disse Ting gør Gud to Gange, ja tre med Mennesket
“Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
30 for at redde hans Sjæl fra Graven, saa han skuer Livets Lys!
ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
31 Lyt til og hør mig, Job, ti stille, saa jeg kan tale!
“Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
32 Har du noget at sige, saa svar mig, tal, thi gerne gav jeg dig Ret;
Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
33 hvis ikke, saa høre du paa mig, ti stille, at jeg kan lære dig Visdom!
Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”

< Job 33 >