< Jeremias 26 >

1 I Josias's Søns, Kong Jojakim af Judas, første Regeringstid kom dette Ord fra HERREN:
Mwanzoni mwa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilikuja kutoka kwa Bwana:
2 Saa siger HERREN: Staa frem i Forgaarden til HERRENS Hus og tal til hele Juda, som kommer for at tilbede i HERRENS Hus, alle de Ord, jeg har paalagt dig at tale til dem; udelad ikke et Ord!
“Hili ndilo Bwana asemalo: Simama katika ua wa nyumba ya Bwana na useme na watu wote wa miji ya Yuda wanaokuja kuabudu katika nyumba ya Bwana. Waambie kila kitu nitakachokuamuru, usipunguze neno.
3 Maaske hører de og omvender sig, hver fra sin onde Vej, saa jeg kan angre det onde, jeg har i Sinde at gøre dem for deres onde Gerningers Skyld.
Huenda watasikiliza, na kila mmoja akageuka kutoka njia yake mbaya. Kisha nitawahurumia na kuacha kuwaletea maafa niliyokuwa ninapanga kwa sababu ya maovu waliyofanya.
4 Sig til dem: Saa siger HERREN: Hvis I ikke hører mig og følger den Lov, jeg har forelagt eder,
Waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ikiwa hamtanisikiliza na kuifuata sheria yangu ambayo nimeiweka mbele yenu,
5 saa I hører mine Tjenere Profeternes Ord, som jeg aarle og silde sendte eder, skønt I ikke vilde høre,
nanyi ikiwa hamtayasikiliza maneno ya watumishi wangu manabii, ambao nimewatuma kwenu tena na tena (ijapokuwa hamkuwasikiliza),
6 saa gør jeg med dette Hus som med Silo og giver alle Jordens Folk denne By at forbande ved.
ndipo nitaifanya nyumba hii kama Shilo na mji huu kuwa kitu cha kulaaniwa na mataifa yote ya dunia.’”
7 Præsterne, Profeterne og alt Folket hørte nu Jeremias tale disse Ord i HERRENS Hus;
Makuhani, manabii na watu wote wakamsikia Yeremia akiyasema maneno haya ndani ya nyumba ya Bwana.
8 og da Jeremias havde sagt alt, hvad HERREN havde paalagt ham at sige til alt Folket, greb Præsterne og Profeterne og alt Folket ham og sagde: »Du skal dø!
Lakini mara tu Yeremia alipomaliza kuwaambia watu kila kitu Bwana alichomwamuru kukisema, basi makuhani, manabii na watu wote walimkamata wakisema, “Ni lazima ufe!
9 Hvor tør du profetere i HERRENS Navn og sige: Det skal gaa dette Hus som Silo, og denne By skal ødelægges, saa ingen bor der!« Og alt Folket stimlede sammen om Jeremias i HERRENS Hus.
Kwa nini unatoa unabii katika jina la Bwana kwamba nyumba hii itakuwa kama Shilo na mji huu utakuwa ukiwa na kuachwa tupu?” Nao watu wote wakamkusanyikia na kumzunguka Yeremia ndani ya nyumba ya Bwana.
10 Da Judas Fyrster hørte det, gik de fra Kongens Palads op til HERRENS Hus og tog Sæde ved Indgangen til HERRENS nye Port.
Maafisa wa Yuda waliposikia kuhusu mambo haya, wakapanda kutoka jumba la kifalme, wakaenda katika nyumba ya Bwana na kushika nafasi zao kwenye ingilio la Lango Jipya la nyumba ya Bwana.
11 Saa sagde Præsterne og Profeterne til Fyrsterne og alt Folket: »Denne Mand har gjort halsløs Gerning, thi han har profeteret mod denne By, som I selv hørte.«
Kisha makuhani na manabii wakawaambia maafisa pamoja na watu wote, “Mtu huyu anastahili ahukumiwe kifo kwa sababu ametoa unabii mbaya dhidi ya mji huu. Mmesikia kwa masikio yenu wenyewe!”
12 Men Jeremias sagde til Fyrsterne og alt Folket: »HERREN sendte mig for at profetere mod dette Hus og denne By alle de Ord, I hørte.
Kisha Yeremia akawaambia maafisa wote na watu wote: “Bwana amenituma kutoa unabii dhidi ya nyumba hii na mji huu mambo yote mliyoyasikia.
13 Bedrer dog eders Veje og eders Gerninger og hør paa HERREN eders Guds Røst, at HERREN maa angre det onde, han har talet imod eder.
Sasa tengenezeni njia zenu na matendo yenu, na kumtii Bwana Mungu wenu. Ndipo Bwana atawahurumia na kuacha kuleta maafa aliyokuwa ameyatamka dhidi yenu.
14 Men se, jeg er i eders Haand; gør med mig, hvad der er godt og billigt i eders Øjne!
Lakini kwa habari yangu mimi, niko mikononi mwenu, nifanyieni lolote mnaloona kuwa ni jema na la haki.
15 Dog skal I vide, at hvis I dræber mig, saa bringer I uskyldigt Blod over eder og denne By og dens Indbyggere; thi sandelig sendte HERREN mig for at tale alle disse Ord til eder.«
Hata hivyo, jueni kwa hakika, ikiwa mtaniua, mtakuwa mmejipatia dhambi kwa damu isiyo na hatia juu yenu wenyewe, na juu ya mji huu na wote wanaoishi ndani yake, kwa maana ni kweli Bwana amenituma kwenu ili niseme maneno haya yote masikioni mwenu.”
16 Da sagde Fyrsterne og alt Folket til Præsterne og Profeterne: »Denne Mand har ikke gjort halsløs Gerning, men talt til os i HERREN vor Guds Navn.«
Kisha maafisa na watu wote wakawaambia makuhani na manabii, “Mtu huyu asihukumiwe kifo! Amesema nasi katika jina la Bwana, Mungu wetu.”
17 Og nogle af Landets Ældste traadte frem og sagde til hele Folkets Forsamling:
Baadhi ya wazee wa nchi wakasogea mbele, wakaliambia kusanyiko lote la watu,
18 »Mika fra Moresjet profeterede paa Kong Ezekias af Judas Tid og sagde til alt Judas Folk: Saa siger Hærskarers HERRE: Zion skal pløjes som en Mark, Jerusalem blive til Grushobe, Tempelbjerget til Krathøj.
“Mika Mmoreshethi alitoa unabii katika siku za Hezekia mfalme wa Yuda. Akawaambia watu wote wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “‘Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.’
19 Mon Kong Ezekias af Juda og hele Juda dræbte ham? Frygtede de ikke HERREN og bad ham om Naade, saa HERREN angrede det onde, han havde truet dem med? Vi er ved at bringe stor Ulykke over vore Sjæle.«
Je, Hezekia mfalme wa Yuda au mtu mwingine yeyote katika Yuda alimhukumu Mika kufa? Je, Hezekia hakumcha Bwana na kuhitaji msaada wake? Je, Bwana hakuwahurumia na akaacha kuleta maafa aliyokuwa ametamka dhidi yao? Tunakaribia sana kujiletea maangamizo ya kutisha sisi wenyewe!”
20 Der var ogsaa en anden Mand, som profeterede i HERRENS Navn, Urija, Sjemajas Søn, fra Kirjat-Jearim; og han profeterede mod denne By og dette Land med de samme Ord som Jeremias.
(Wakati huu, Uria mwana wa Shemaya kutoka mji wa Kiriath-Yearimu alikuwa mtu mwingine aliyetoa unabii kwa jina la Bwana. Alitoa unabii juu ya mambo yaliyofanana na haya dhidi ya mji huu na nchi hii kama alivyofanya Yeremia.
21 Da Kong Jojakim og alle hans Krigsfolk og alle Fyrsterne hørte hans Ord, stod han ham efter Livet; og da Urija hørte det, blev han bange og flygtede og kom til Ægypten.
Mfalme Yehoyakimu na wakuu wake wote na maafisa waliposikia maneno yake, mfalme alitafuta kumuua. Lakini Uria alipata habari, na kwa kuogopa akakimbilia Misri.
22 Men Kong Jojakim sendte Folk til Ægypten; han sendte Elnatan, Akbors Søn, og nogle andre til Ægypten,
Hata hivyo, Mfalme Yehoyakimu alimtuma Elnathani mwana wa Akbori huko Misri, pamoja na watu wengine ili kwenda kumkamata Uria.
23 og de bragte Urija hjem fra Ægypten og førte ham til Kong Jojakim, som lod ham hugge ned med Sværdet og hans Lig kaste hen, hvor Smaafolk havde deres Grave.
Wakamrudisha Uria kutoka Misri na kumpeleka kwa Mfalme Yehoyakimu, ambaye alimuua kwa upanga, na mwili wake kutupwa kwenye eneo la makaburi ya watu wasio na cheo.)
24 Men Ahikam, Sjafans Søn, holdt Haanden over Jeremias, saa han ikke blev overgivet i Folkets Haand og dræbt.
Zaidi ya hayo, Ahikamu mwana wa Shafani akamuunga mkono Yeremia, kwa hiyo hakutiwa tena mikononi mwa watu ili auawe.

< Jeremias 26 >