< 1 Mosebog 8 >
1 Da ihukom Gud Noa og alle de vilde Dyr og Kvæget, som var hos ham i Arken; og Gud lod en Storm fare hen over Jorden, saa at Vandet begyndte at falde;
Mungu akamkumbuka Noa na wanyama wote wa porini na wa kufugwa waliokuwa naye ndani ya safina, akatuma upepo ukavuma katika dunia, nayo maji yakaondoka.
2 Verdensdybets Kilder og Himmelens Sluser lukkedes, Regnen fra Himmelen standsede,
Zile chemchemi zilizo chini sana ya ardhi pamoja na malango ya mafuriko ya mbinguni yakawa yamefungwa nayo mvua ikawa imekoma kunyesha kutoka angani.
3 og Vandet veg lidt efter lidt bort fra Jorden, og Vandet tog af efter de 150 Dages Forløb.
Maji yakaendelea kupungua taratibu katika nchi. Kunako mwisho wa siku ya 150, maji yalikuwa yamepungua,
4 Paa den syttende Dag i den syvende Maaned sad Arken fast paa Ararats Bjerge,
katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa saba, safina ikatua katika milima ya Ararati.
5 og Vandet vedblev at synke indtil den tiende Maaned, og paa den første Dag i denne Maaned dukkede Bjergenes Toppe frem.
Maji yakaendelea kupungua hadi mwezi wa kumi, na siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, vilele vya milima vikaonekana.
6 Da der var gaaet fyrretyve Dage: aabnede Noa den Luge, han havde lavet paa Arken,
Baada ya siku arobaini Noa akafungua dirisha alilokuwa amelifanya katika safina
7 og sendte en Ravn ud; den fløj frem og tilbage, indtil Vandet var tørret bort fra Jorden.
na akamtoa kunguru, akawa akiruka kwenda na kurudi mpaka maji yalipokwisha kukauka juu ya nchi.
8 Da sendte han en Due ud for at se, om Vandet var sunket fra Jordens Overflade;
Kisha akamtoa hua ili aone kama maji yameondoka juu ya uso wa ardhi.
9 men Duen fandt intet Sted at sætte sin Fod og vendte tilbage til ham i Arken, fordi der endnu var Vand over hele Jorden; og han rakte Haanden ud og tog den ind i Arken til sig.
Lakini hua hakupata mahali pa kutua kwa kuwa maji yalienea juu ya uso wa dunia yote, kwa hiyo akarudi kwa Noa ndani ya safina. Noa akanyoosha mkono akamchukua yule hua akamrudisha ndani ya safina.
10 Derpaa biede han yderligere syv Dage og sendte saa atter Duen ud fra Arken;
Noa akangojea siku saba zaidi kisha akamtoa tena hua kutoka safina.
11 ved Aftenstid kom Duen tilbage til ham, og se, den havde et friskt Olieblad i Næbbet. Da skønnede Noa, at Vandet var svundet bort fra Jorden.
Wakati hua aliporejea kwa Noa jioni, alikuwa amechukua katika mdomo wake jani bichi la mzeituni, lililochumwa wakati ule ule! Ndipo Noa akajua ya kuwa maji yameondoka juu ya uso wa dunia.
12 Derpaa biede han syv Dage til, og da han saa sendte Duen ud, kom den ikke mere tilbage til ham.
Akangojea siku saba zaidi na akamtuma tena hua, lakini wakati huu hua hakurudi tena kwa Noa.
13 I Noas 601ste Leveaar paa den første Dag i den første Maaned var Vandet tørret bort fra Jorden. Da tog Noa Dækket af Arken, og da han saa sig om, se, da var Jordens Overflade tør.
Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka 601, wa kuishi kwake Noa, maji yalikuwa yamekauka duniani. Kisha Noa akafungua mlango wa safina akaona ya kuwa uso wa ardhi ulikuwa umekauka.
14 Paa den syv og tyvende Dag i den anden Maaned var Jorden tør.
Katika siku ya ishirini na saba ya mwezi wa pili dunia ilikuwa imekauka kabisa.
Ndipo Mungu akamwambia Noa,
16 »Gaa ud af Arken med din Hustru, dine Sønner og dine Sønnekoner
“Toka ndani ya safina, wewe na mkeo na wanao na wake zao.
17 og for alle Dyr, der er hos dig, alt Kød, Fugle, Kvæg og alt Kryb, der kryber paa Jorden, ud med dig, at de kan vrimle paa Jorden og blive frugtbare og mangfoldige paa Jorden!«
Utoe nje kila aina ya kiumbe hai aliye pamoja nawe: Ndege, wanyama na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi, ili wakazae, na kuongezeka na kuijaza tena dunia.”
18 Da gik Noa ud med sine Sønner, sin Hustru og sine Sønnekoner;
Kwa hiyo Noa akatoka nje pamoja na mkewe, wanawe na wake zao.
19 og alle de vildtlevende Dyr, alt Kvæget, alle Fuglene og alt Krybet, der kryber paa Jorden, efter deres Slægter, gik ud af Arken.
Wanyama wote na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi na ndege wote, kila kitu kiendacho juu ya nchi, aina moja baada ya nyingine vikatoka katika safina, kila aina ya kiumbe, kimoja baada ya kingine.
20 Derpaa byggede Noa HERREN et Alter og tog nogle af alle de rene Dyr og Fugle og ofrede Brændofre paa Alteret.
Kisha Noa akamjengea Bwana madhabahu, akachukua baadhi ya wale wanyama na ndege wote walio safi, akatoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.
21 Og da HERREN indaandede den liflige Duft, sagde han til sig selv: »Jeg vil aldrig mere forbande Jorden for Menneskenes Skyld, thi Menneskehjertets Higen er ond fra Ungdommen af, og jeg vil aldrig mere tilintetgøre alt, hvad der lever, saaledes som jeg nu har gjort!
Bwana akasikia harufu nzuri ya kupendeza, naye akasema moyoni mwake, “Kamwe sitailaani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, hata ingawa kila mwelekeo wa moyo wake ni mbaya tangu ujana. Kamwe sitaangamiza tena viumbe hai vyote kama nilivyofanya.
22 Herefter skal, saa længe Jorden staar, Sæd og Høst, Kulde og Hede, Sommer og Vinter, Dag og Nat ikke ophøre!«
“Kwa muda dunia idumupo, wakati wa kupanda na wa kuvuna, wakati wa baridi na wa joto, wakati wa kiangazi na wa masika, usiku na mchana kamwe havitakoma.”