< 1 Mosebog 6 >

1 Da nu Menneskene begyndte at blive talrige paa Jorden og der fødtes dem Døtre,
Watu walipoanza kuongezeka idadi katika uso wa dunia na watoto wa kike wakazaliwa kwao,
2 fik Gudssønnerne Øje paa Menneskedøtrenes Skønhed, og de tog saa mange af dem, som de lystede, til Hustruer.
wana wa Mungu wakawaona kuwa hao binti za wanadamu walikuwa wazuri wa sura, wakaoa yeyote miongoni mwao waliyemchagua.
3 Da sagde HERREN: »Min Aand skal ikke for evigt blive i Menneskene, eftersom de jo dog er Kød; deres Dage skal være 120 Aar.«
Ndipo Bwana akasema, “Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye ni wa kufa, siku zake zitakuwa miaka 120.”
4 I hine Dage, da Gudssønnerne gik ind til Menneskedøtrene og disse fødte dem Børn — men ogsaa senere hen i Tiden — levede Kæmperne paa Jorden. Det er Heltene, hvis Ry naar tilbage til Fortids Dage.
Wanefili walikuwako duniani siku hizo, na baadaye, hao wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu na kuzaa nao. Wanefili walikuwa mashujaa na watu waliojulikana wa zamani hizo.
5 Men HERREN saa, at Menneskenes, Ondskab tog til paa Jorden, og at deres Hjerters Higen og Tragten kun var ond Dagen lang.
Bwana akaona jinsi uovu wa mwanadamu ulivyokuwa mkubwa duniani, na ya kuwa kila mwelekeo wa mawazo ya moyo wake wakati wote ulikuwa mbaya tu.
6 Da angrede HERREN, at han havde gjort Menneskene paa Jorden, og det skar ham i Hjertet.
Bwana akasikitika kwamba alimuumba mwanadamu duniani, moyo wa Mungu ukajaa masikitiko.
7 Og HERREN sagde: »Jeg vil udslette Menneskene, som jeg har skabt, af Jordens Flade, baade Mennesker, Kvæg, Kryb og Himmelens, Fugle, thi jeg angrer, at jeg gjorde dem!«
Kwa hiyo Bwana akasema, “Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemuumba kutoka kwenye uso wa dunia, wanadamu na wanyama, pamoja na viumbe vitambaavyo na ndege wa angani. Kwa maana nasikitika kuwaumba.”
8 Men Noa fandt Naade for HERRENS Øjne.
Lakini Noa akapata kibali machoni pa Bwana.
9 Dette er Noas Slægtebog. Noa var en retfærdig, ustraffelig Mand blandt sine samtidige; Noa vandrede med Gud.
Hivi ndivyo vizazi vya Noa. Noa alikuwa mtu wa haki, na mkamilifu miongoni mwa watu wa wakati wake, tena alitembea na Mungu.
10 Noa avlede tre Sønner: Sem, Kam og Jafet.
Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi.
11 Men Jorden fordærvedes for Guds Øjne, og Jorden blev fuld af Uret;
Wakati huu dunia ilikuwa imejaa uharibifu na ukatili machoni pa Mungu.
12 og Gud saa til Jorden, og se, den var fordærvet, thi alt Kød havde fordærvet sin Vej paa Jorden.
Mungu akaona jinsi dunia ilivyoharibika, kwa maana watu wote duniani walikuwa wameharibu njia zao.
13 Da sagde Gud til Noa: »Jeg har besluttet at gøre Ende paa alt Kød, fordi Jorden ved deres Skyld et fuld af Uret; derfor vil jeg nu udrydde dem af Jorden.
Kwa hiyo Mungu akamwambia Noa, “Nitawaangamiza watu wote, kwa kuwa dunia imejaa ukatili kwa sababu yao. Hakika mimi nitaangamiza watu pamoja na dunia.
14 Men du skal gøre dig en Ark af Gofertræ og indrette den med Rum ved Rum og overstryge den med Beg baade indvendig og udvendig;
Kwa hiyo jitengenezee safina kubwa kwa mbao za mvinje, tengeneza vyumba ndani yake na uipake lami ndani na nje.
15 og saaledes skal du bygge Arken: Den skal være 300 Alen lang, 50 Alen bred og 30 Alen høj;
Hivi ndivyo utakavyoitengeneza: Safina iwe na urefu wa dhiraa 300, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini.
16 du skal anbringe Taget paa Arken, og det skal ikke rage længer ud end een Alen fra oven; paa Arkens Side skal du sætte Døren, og du skal indrette den med et nederste, et mellemste og et øverste Stokværk.
Itengenezee paa na umalizie safina kwa kuacha nafasi ya dhiraa moja juu. Weka mlango ubavuni mwa safina, na uifanye ya ghorofa ya chini, ya kati na ya juu.
17 Se, jeg bringer nu Vandfloden over Jorden for at udrydde alt Kød under Himmelen, som har Livsaande; alt, hvad der er paa Jorden, skal forgaa.
Nitaleta gharika ya maji juu ya nchi ili kuangamiza uhai wote chini ya mbingu, kila kiumbe chenye pumzi ya uhai ndani yake. Kila kitu juu ya nchi kitaangamia.
18 Men jeg vil oprette min Pagt med dig. Du skal gaa ind i Arken med dine Sønner, din Hustru og dine Sønnekoner;
Lakini Mimi nitaweka Agano langu na wewe, nawe utaingia ndani ya Safina, wewe pamoja na mke wako, wanao na wake zao.
19 og af alle Dyr, af alt Kød skal du bringe et Par af hver Slags ind i Arken for at holde dem i Live hos dig. Han og Hundyr skal det være,
Utaingiza ndani ya Safina kila aina ya kiumbe hai wawili wawili, wa kiume na wa kike, ili kuwahifadhi hai pamoja na wewe.
20 af Fuglene efter deres Arter, af Kvæget efter dets Arter og af alt Jordens Kryb efter dets Arter; Par for Par skal de gaa ind til dig for at holdes i Live.
Wawili wa kila aina ya ndege, wa kila aina ya mnyama na wa kila aina ya kitambaacho ardhini watakuja kwako ili wahifadhiwe hai.
21 Og du skal indsamle et Forraad af alle Slags Levnedsmidler, for at det kan tjene dig og dem til Føde.«
Utachukua kila aina ya chakula kitakacholiwa, na ukiweke akiba kama chakula kwa ajili yako na yao.”
22 Og Noa gjorde ganske som Gud havde paalagt ham; saaledes gjorde han.
Noa akafanya kila kitu kama vile Mungu alivyomwamuru.

< 1 Mosebog 6 >

The World is Destroyed by Water
The World is Destroyed by Water