< 1 Mosebog 24 >

1 Abraham var blevet gammel og til Aars, og HERREN havde velsignet ham i alle Maader.
Wakati huu Abrahamu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, naye Bwana alikuwa amembariki katika kila njia.
2 Da sagde Abraham til sin Træl, sit Hus's ældste, som stod for hele hans Ejendom: »Læg din Haand under min Lænd,
Akamwambia mtumishi wake mkuu wa vitu vyote katika nyumba yake, yule aliyekuwa msimamizi wa vitu vyote alivyokuwa navyo, “Weka mkono wako chini ya paja langu,
3 saa jeg kan tage dig i Ed ved HERREN, Himmelens og Jordens Gud, at du ikke vil tage min Søn en Hustru af Kana'anæernes Døtre, blandt hvem jeg bor,
Ninataka uape kwa Bwana, Mungu wa mbingu na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke kutoka binti za Wakanaani, ambao ninaishi miongoni mwao,
4 men drage til mit Land og min Hjemstavn og tage min Søn Isak en Hustru derfra!«
bali utakwenda katika nchi yangu na jamaa zangu umpatie Isaki mwanangu mke.”
5 Da sagde Trællen: »Men hvis nu Pigen ikke vil følge mig her til Landet, skal jeg saa bringe din Søn tilbage til det Land, du vandrede ud fra?«
Yule mtumishi akamuuliza, “Je, kama huyo mwanamke atakataa kuja nami katika nchi hii? Je, nimpeleke mwanao katika hiyo nchi uliyotoka?”
6 Abraham svarede: »Vogt dig vel for at bringe min Søn tilbage dertil!
Abrahamu akasema, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu huko.
7 HERREN, Himmelens Gud, som tog mig bort fra min Faders Hus og min Hjemstavns Land, som talede til mig og tilsvor mig, at han vil give mit Afkom dette Land, han vil sende sin Engel foran dig, saa du kan tage min Søn en Hustru derfra;
Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa nyumbani kwa baba yangu na nchi yangu niliyozaliwa na aliyesema nami na akaniahidi kwa kiapo, akisema, ‘Nitawapa watoto wako nchi hii,’ atatuma malaika wake akutangulie ili umpatie mwanangu mke kutoka huko.
8 men hvis Pigen ikke vil følge dig, saa er du løst fra Eden til mig; men i intet Tilfælde maa du bringe min Søn tilbage dertil!«
Kama huyo mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi utafunguliwa kutoka kiapo nilichokuapisha. Ila usimrudishe mwanangu huko.”
9 Da lagde Trællen sin Haand under sin Herre Abrahams Lænd og svor ham Eden.
Basi yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la bwana wake Abrahamu akamwapia kuhusu shauri hili.
10 Derpaa tog Trællen ti af sin Herres Kameler og alle Haande kostbare Gaver fra sin Herre og gav sig paa Vej til Nakors By i Aram-Naharajim.
Ndipo huyo mtumishi akachukua ngamia kumi miongoni mwa ngamia za bwana wake, akaondoka, akiwa amechukua aina zote za vitu vizuri kutoka kwa bwana wake. Akaelekea Aramu-Naharaimu na kushika njia kwenda mji wa Nahori.
11 Uden for Byen lod han Kamelerne knæle ved Brønden ved Aftenstid, ved den Tid Kvinderne gaar ud for at hente Vand;
Akawapigisha ngamia magoti karibu na kisima cha maji nje ya mji, ilikuwa inaelekea jioni, wakati ambapo wanawake wanakuja kuteka maji.
12 og han bad saaledes: »HERRE, du min Herre Abrahams Gud, lad det lykkes for mig i Dag og vis Miskundhed mod min Herre Abraham!
Kisha akaomba, “Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, nipatie ushindi leo, uonyeshe huruma kwa bwana wangu Abrahamu.
13 Se, jeg stiller mig her ved Vandkilden, nu Bymændenes Døtre gaar ud for at hente Vand;
Tazama, nimesimama karibu na kisima hiki cha maji, nao binti za watu wa mji huu wanakuja kuteka maji.
14 og siger jeg nu til en Pige: Hæld din Krukke og giv mig at drikke! og siger saa hun: Drik kun, og jeg vil ogsaa give dine Kameler at drikke! lad det da være hende, du har udset til din Tjener Isak; saaledes vil jeg kunne kende, at du har vist Miskundhed mod min Herre!«
Basi na iwe hivi, nitakapomwambia binti mmojawapo, ‘Tafadhali tua mtungi wako nipate kunywa maji,’ naye akisema, ‘Kunywa, nitawanywesha na ngamia wako pia.’ Basi na awe ndiye uliyemchagua kwa ajili ya mtumishi wako Isaki. Kwa hili nitajua umemhurumia bwana wangu.”
15 Knap var han færdig med at bede, se, da kom Rebekka, en Datter af Betuel, der var en Søn af Abrahams Broder Nakors Hustru Milka, gaaende med Krukken paa Skulderen,
Ikawa kabla hajamaliza kuomba, Rebeka akatokea akiwa na mtungi begani mwake. Alikuwa binti wa Bethueli. Bethueli alikuwa mwana wa Milka aliyekuwa mke wa Nahori ndugu wa Abrahamu.
16 en saare smuk Kvinde, Jomfru, endnu ikke kendt af nogen Mand. Hun steg ned til Kilden, fyldte sin Krukke og steg op igen.
Huyu msichana alikuwa mzuri sana wa sura, bikira, ambaye hakuna mtu aliyekuwa amekutana naye kimwili. Aliteremka kisimani, akajaza mtungi wake akapanda juu.
17 Da ilede Trællen hen til hende og sagde: »Giv mig lidt Vand at drikke af din Krukke!«
Ndipo yule mtumishi akaharakisha kukutana naye akamwambia, “Tafadhali nipe maji kidogo katika mtungi wako.”
18 Hun svarede: »Drik, Herre!« og løftede straks Krukken ned paa sin Haand og lod ham drikke;
Yule msichana akasema, “Kunywa, bwana wangu.” Akashusha kwa haraka mtungi mkononi mwake na akampa, akanywa.
19 og da hun havde slukket hans Tørst, sagde hun: »Jeg vil ogsaa øse Vand til dine Kameler, til de har slukket deres Tørst.«
Baada ya kumpa yule mtumishi yale maji, akamwambia, “Nitateka maji kwa ajili ya ngamia zako pia mpaka wote watosheke.”
20 Saa skyndte hun sig hen og tømte Krukken i Truget og løb tilbage til Brønden for at øse, og saaledes øste hun til alle hans Kameler.
Akafanya haraka kumimina maji kwenye birika ya kunyweshea wanyama, akakimbia kisimani kuteka maji mengine na akateka ya kuwatosha ngamia wake wote.
21 Imidlertid stod Manden og saa tavs paa hende for at faa at vide, om HERREN havde ladet hans Rejse lykkes eller ej;
Pasipo kusema neno, yule mtumishi akamtazama kwa makini aone kama Bwana ameifanikisha safari yake, au la.
22 og da Kamelernes Tørst var slukket, tog han en gylden Næsering, der vejede en halv Sekel, og to Armbaand, der vejede ti Guldsekel, og satte dem paa hendes Arme;
Ikawa ngamia walipokwisha kunywa wote, yule mtumishi akampa huyo msichana pete ya puani ya dhahabu yenye uzito wa beka moja na bangili mbili za dhahabu zenye uzito wa shekeli kumi.
23 og han sagde til hende: »Sig mig, hvis Datter du er! Er der Plads til os i din Faders Hus for Natten?«
Kisha akamuuliza, “Wewe ni binti wa nani? Tafadhali uniambie, je, kuna nafasi katika nyumba ya baba yako tutakapoweza kulala?”
24 Hun svarede: »Jeg er Datter af Betuel, som Milka fødte Nakor; «
Yule msichana akamjibu, “Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Milka aliyemzalia Nahori.”
25 og videre sagde hun: »Der er rigeligt baade af Straa og Foder hos os og Plads til at overnatte!«
Akaendelea kusema, “Kwetu kuna majani mengi na malisho, tena kuna nafasi kwa ajili yenu kulala.”
26 Da bøjede Manden sig og tilbad HERREN,
Yule mtumishi akasujudu na kumwabudu Bwana,
27 idet han sagde: »Lovet være HERREN, min Herre Abrahams Gud, som ikke har unddraget min Herre sin Miskundhed og Trofasthed! HERREN har ført mig paa Vejen til min Herres Broders Hus.«
akisema, “Atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hakuondoa wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Mimi nami, Bwana ameniongoza safarini akanifikisha nyumbani kwa jamaa za bwana wangu.”
28 Pigen løb imidlertid hjem og fortalte alt dette i sin Moders Hus.
Yule msichana akakimbia akawaeleza watu wa nyumbani mwa mama yake kuhusu mambo haya.
29 Men Rebekka havde en Broder ved Navn Laban; han løb ud til Manden ved Kilden;
Rebeka alikuwa na kaka aliyeitwa Labani, huyo akaharakisha kukutana na yule mtumishi kule kisimani.
30 og da han saa Næseringen og Armbaandene paa sin Søsters Arme og hørte sin Søster Rebekka fortælle, hvad Manden havde sagt til hende, gik han ud til Manden, som stod med sine Kameler ved Kilden;
Mara alipoiona ile pete puani, na bangili mikononi mwa dada yake na kusikia yale maneno Rebeka aliyoambiwa na huyo mtumishi, alimwendea huyo mtumishi, akamkuta amesimama karibu na ngamia wake pale karibu na kisima.
31 og han sagde: »Kom, du HERRENS velsignede, hvorfor staar du herude? Jeg har ryddet op i Huset og gjort Plads til Kamelerne.«
Akamwambia, “Karibu nyumbani wewe uliyebarikiwa na Bwana, kwa nini unasimama huko nje? Mimi nimekuandalia nyumba na mahali kwa ajili ya ngamia.”
32 Saa kom Manden hen til Huset og tog Seletøjet af Kamelerne, og Laban bragte Straa og Foder til dem og Vand til Fodtvæt for Manden og hans Ledsagere.
Hivyo yule mtumishi akaenda nyumbani, mizigo ikaondolewa juu ya ngamia. Majani na malisho yakaletwa kwa ajili ya ngamia na maji kwa ajili yake na watu wake ili kunawa miguu.
33 Men da der blev sat Mad for ham, sagde han: »Jeg vil intet nyde, før jeg har røgtet mit Ærinde!« De svarede: »Sig frem!«
Ndipo chakula kikaandaliwa kwa ajili yake, lakini akasema, “Sitakula mpaka niwe nimewaambia yale niliyo nayo ya kusema.” Labani akasema, “Basi tuambie.”
34 Saa sagde han: »Jeg er Abrahams Træl.
Hivyo akasema, “Mimi ni mtumishi wa Abrahamu.
35 HERREN har velsignet min Herre i rigt Maal, saa han er blevet en velstaaende Mand, og givet ham Smaakvæg og Hornkvæg, Sølv og Guld, Trælle og Trælkvinder, Kameler og Æsler;
Bwana amembariki sana bwana wangu, amekuwa tajiri. Amempa kondoo na ngʼombe, fedha na dhahabu, watumishi wa kiume na wa kike, ngamia na punda.
36 og Sara, min Herres Hustru, har født ham en Søn i hans Alderdom, og ham har han givet alt, hvad han ejer.
Sara mkewe bwana wangu amemzalia mwana katika uzee wake, naye amempa kila kitu alichokuwa nacho.
37 Og nu har min Herre taget mig i Ed og sagt: Du maa ikke tage min Søn en Hustru blandt Kana'anæernes Døtre, i hvis Land jeg bor;
Naye bwana wangu ameniapisha na akasema, ‘Kamwe usimtwalie mwanangu mke katika binti za Wakanaani, ambao ninaishi katika nchi yao,
38 Men du skal drage til min Faders Hus og min Slægt og tage min Søn en Hustru derfra!
ila uende mpaka kwa jamaa ya baba yangu na ukoo wangu mwenyewe, ukamtwalie mwanangu mke huko.’
39 Og da jeg sagde til min Herre: Men hvis nu Pigen ikke vil følge med mig?
“Kisha nikamuuliza bwana wangu, ‘Je, kama huyo mwanamke hatakubali kurudi nami?’
40 svarede han: HERREN, for hvis Aasyn jeg har vandret, vil sende sin Engel med dig og lade din Rejse lykkes, saa du kan tage min Søn en Hustru af min Slægt og min Faders Hus;
“Akanijibu, ‘Bwana ambaye nimetembea mbele zake, atatuma malaika wake pamoja nawe, na kuifanikisha safari yako, ili uweze kupata mke kwa ajili ya mwanangu katika ukoo wangu na kutoka jamaa ya baba yangu.
41 i modsat Fald er du løst fra Eden til mig; kommer du til min Slægt, og de ikke vil give dig hende, er du løst fra Eden til mig!
Kisha, utakapokwenda kwenye ukoo wangu, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu hata kama wakikataa kukupa huyo binti, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu.’
42 Da jeg nu i Dag kom til Kilden, bad jeg saaledes: HERRE, du min Herre Abrahams Gud! Vilde du dog lade den Rejse lykkes, som jeg nu har for!
“Nilipokuja kisimani leo nilisema, ‘Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ikikupendeza, naomba uifanikishe safari niliyoijia.
43 Se, jeg stiller mig her ved Kilden, og siger jeg nu til den Pige, der kommer for at øse Vand: Giv mig lidt Vand at drikke af din Krukke!
Tazama, ninasimama kando ya kisima hiki, kama mwanamwali akija kuteka maji nami nikimwambia, tafadhali niruhusu ninywe maji kidogo kutoka kwenye mtungi wako,
44 og svarer saa hun: Drik selv, og jeg vil ogsaa øse Vand til dine Kameler! lad hende da være den Kvinde, HERREN har udset til min Herres Søn!
naye kama akiniambia, “Kunywa, nami nitateka maji kwa ajili ya ngamia wako pia,” basi huyo awe ndiye mke ambaye Bwana amemchagulia mwana wa bwana wangu.’
45 Og knap var jeg færdig med at tale saaledes ved mig selv, se, da kom Rebekka med sin Krukke paa Skulderen og steg ned til Kilden og øste Vand, og da jeg sagde til hende: Giv mig noget at drikke!
“Kabla sijamaliza kuomba moyoni mwangu, Rebeka akatokea, amebeba mtungi begani mwake. Akashuka kisimani akateka maji, nami nikamwambia, ‘Tafadhali nipe maji ninywe.’
46 løftede hun straks sin Krukke ned og sagde: Drik kun, og jeg vil ogsaa give dine Kameler at drikke! Saa drak jeg, og hun gav ogsaa Kamelerne at drikke.
“Akafanya haraka kushusha mtungi wake begani na kusema, ‘Kunywa na nitawanywesha ngamia wako pia,’ basi nikanywa, akawanywesha na ngamia pia.
47 Da spurgte jeg hende: Hvis Datter er du? Og hun sagde: Jeg er Datter af Betuel, Nakors og Milkas Søn! Saa satte jeg Ringen i hendes Næse og Armbaandene paa hendes Arme;
“Nikamuuliza, ‘Wewe ni binti wa nani?’ “Akasema, ‘Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Nahori, Milka aliyemzalia.’ “Ndipo nilipotia pete puani mwake na bangili mikononi mwake,
48 og jeg bøjede mig og tilbad HERREN, og jeg lovede HERREN, min Herre Abrahams Gud, som havde ført mig den rigtige Vej, saa jeg: kunde tage min Herres Broderdatter til hans Søn!
nikasujudu na nikamwabudu Bwana. Nikamtukuza Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, aliyeniongoza katika njia sahihi ili nimtwalie mwana na bwana wangu mke katika jamaa zake.
49 Hvis I nu vil vise min Herre Godhed og Troskab, saa sig mig det, og hvis ikke, saa sig mig det, for at jeg kan have noget at rette mig efter!«
Ikiwa mtaonyesha wema na uaminifu kwa bwana wangu, mniambie, la sivyo, mniambie, ili niweze kujua njia ya kugeukia.”
50 Da sagde Laban og Betuel: »Denne Sag kommer fra HERREN, vi kan hverken gøre fra eller til!
Labani na Bethueli wakajibu, “Jambo hili limetoka kwa Bwana, hatuwezi kukuambia jambo lolote baya au jema.
51 Der staar Rebekka foran dig, tag hende og drag bort, at hun kan: blive din Herres Søns Hustru, saaledes som HERREN har sagt!«
Rebeka yuko hapa, mchukue na uende, awe mke wa mwana wa bwana wako, sawasawa na Bwana alivyoongoza.”
52 Da Abrahams Træl hørte deres Ord, kastede han sig til Jorden for HERREN.
Ikawa huyo mtumishi wa Abrahamu aliposikia waliyosema, alisujudu mpaka nchi mbele za Bwana.
53 Derpaa fremtog Trællen Sølv og Guldsmykker og Klæder og gav Rebekka dem, og til hendes Broder og Moder uddelte han Gaver.
Ndipo huyo mtumishi akatoa vitu vilivyotengenezwa kwa dhahabu na kwa fedha pamoja na mavazi, akampa Rebeka, pia akawapa zawadi za thamani kubwa nduguye na mamaye.
54 Saa spiste og drak han og hans Ledsagere og overnattede der. Da de var staaet op næste Morgen, sagde han: »Lad mig nu fare til min Herre!«
Kisha yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye wakala, wakanywa na kulala palepale. Walipoamka asubuhi, yule mtumishi, akasema, “Nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
55 Men Rebekkas Broder og Moder svarede: »Lad dog Pigen blive hos os i nogen Tid, en halv Snes Dage eller saa, siden kan du drage bort!«
Lakini ndugu yake Rebeka pamoja na mama yake wakajibu, “Acha binti akae kwetu siku kumi au zaidi, ndipo mwondoke.”
56 Da sagde han til dem: »Ophold mig ikke, nu HERREN har ladet min Rejse lykkes; lad mig fare! Jeg vil drage til min Herre!«
Lakini yule mtumishi akawaambia, “Msinicheleweshe, kwa kuwa Bwana amefanikisha safari yangu, nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
57 De svarede; »Lad os kalde paa. Pigen og spørge hende selv!«
Ndipo wakasema, “Acha tumwite huyo binti tumuulize, tusikie atakavyosema.”
58 Og de kaldte paa Rebekka og spurgte hende: »Vil du drage med denne Mand?« Hun svarede: »Ja, jeg vil!«
Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je, utakwenda na mtu huyu?” Akasema, “Nitakwenda.”
59 Da tog de Afsked med deres, Søster Rebekka og hendes Amme og med Abrahams Træl og hans Ledsagere;
Hivyo wakamwaga ndugu yao Rebeka aondoke, pamoja na mjakazi wake, mtumishi wa Abrahamu na watu wake.
60 og de velsignede Rebekka og sagde: »Maatte du, vor Søster, blive til ti Tusind Tusinder, og maatte dit Afkom indtage dine Fjenders Porte!«
Wakambariki Rebeka, wakamwambia, “Ndugu yetu, uwe wewe kumi elfu, mara elfu nyingi, nao wazao wako wamiliki malango ya adui zao.”
61 Saa brød Rebekka og hendes Piger op, og de satte sig paa Kamelerne og fulgte med Manden; og Trællen tog Rebekka og drog bort.
Rebeka na vijakazi wake wakajiandaa, wakapanda ngamia zao wakafuatana na yule mtu. Hivyo yule mtumishi akamchukua Rebeka akaondoka.
62 Isak var imidlertid draget til Ørkenen ved Be'er-lahaj-ro'i, og han boede i Sydlandet.
Basi Isaki alikuwa ametoka Beer-Lahai-Roi, kwa kuwa alikuwa anaishi nchi ya Negebu.
63 Da han engang ved Aftenstid var gaaet ud paa Marken for at bede, saa han op og fik Øje paa nogle Kameler, der nærmede sig.
Isaki akatoka kwenda shambani kutafakari wakati wa jioni, alipoinua macho yake, akaona ngamia wanakuja.
64 Men da Rebekka saa op og fik Øje paa Isak, lod hun sig glide ned af Kamelen
Rebeka pia akainua macho akamwona Isaki. Akashuka kutoka kwenye ngamia wake
65 og spurgte Trællen: »Hvem er den Mand der, som kommer os i Møde paa Marken?« Trællen svarede: »Det er min Herre!« Da tog hun sit Slør og tilhyllede sig.
na akamuuliza yule mtumishi, “Ni nani mtu yule aliye kule shambani anayekuja kutulaki?” Yule mtumishi akajibu, “Huyu ndiye bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
66 Men Trællen fortalte Isak alt, hvad han havde udrettet.
Kisha yule mtumishi akamweleza Isaki mambo yote aliyoyatenda.
67 Da førte Isak Rebekka ind i sin Moder Saras Telt og tog hende til Hustru; og han fik hende kær. Saaledes blev Isak trøstet efter sin Moder.
Ndipo Isaki akamwingiza Rebeka katika hema la Sara mama yake, Isaki akamchukua Rebeka, hivyo akawa mke wake. Isaki akampenda, akafarijika baada ya kifo cha mama yake.

< 1 Mosebog 24 >