< Galaterne 4 >
1 Men jeg siger: Saa længe Arvingen er umyndig, er der ingen Forskel imellem ham og en Træl, skønt han er Herre over alt Godset;
Ninasema kwamba maadamu mrithi ni mtoto, hana tofauti na mtumwa, hata ingawa ni mmiliki wa mali yote.
2 men han staar under Formyndere og Husholdere indtil den af Faderen bestemte Tid.
Badala yake, yuko chini ya waangalizi na wadhamini mpaka wakati uliowekwa na baba yake.
3 Saaledes stode ogsaa vi, dengang vi vare umyndige, som Trælle under Verdens Børnelærdom.
Kadhalika pia na sisi, tulipokuwa watoto, tulishikiliwa katika utumwa wa kanuni za kwanza za ulimwengu.
4 Men da Tidens Fylde kom, udsendte Gud sin Søn, født af en Kvinde, født under Loven,
Lakini wakati sahihi ulipofika, Mungu alimtuma mwanawe, mzaliwa wa mwanamke, mzaliwa chini ya sheria.
5 for at han skulde løskøbe dem, som vare under Loven, for at vi skulde faa Sønneudkaarelsen.
Alifanya hivi ili kuwakomboa wale waliokuwa chini ya sheria, ili kwamba tupokee hali ya kuwa kama wana.
6 Men fordi I ere Sønner, har Gud udsendt i vore Hjerter sin Søns Aand, som raaber: Abba, Fader!
Kwa sababu ninyi ni wana, Mungu alimtuma Roho wa mwanawe ndani ya mioyo yetu, Roho aitaye, “Abba, Baba.”
7 Altsaa er du ikke længer Træl, men Søn; men er du Søn, da er du ogsaa Arving ved Gud.
Kwa sababu hii wewe si mtumwa tena bali mwana. Kama ni mwana, basi wewe pia ni mrithi kupitia Mungu.
8 Dengang derimod, da I ikke kendte Gud, trællede I for de Guder, som af Natur ikke ere det.
Hata kabla, wakati hamkumjua Mungu, mlikuwa watumwa kwa wale ambao kwa asili si miungu kabisa.
9 Men nu, da I have lært Gud at kende, ja, meget mere ere blevne kendte af Gud, hvor kunne I da atter vende tilbage til den svage og fattige Børnelærdom, som I atter forfra ville trælle under?
Lakini sasa kwamba mnamjua Mungu, au kwamba mnajulikana na Mungu, kwa nini mnarudi tena kwenye kanuni dhaifu za kwanza na zisizo za thamani? Je mnataka kuwa watumwa tena?
10 I tage Vare paa Dage og Maaneder og Tider og Aar.
Mnashika kwa uangalifu siku maalumu, miandamo ya miezi, majira, na miaka. Ninaogopa kwa ajili yenu.
11 Jeg frygter for, at jeg maaske har arbejdet forgæves paa eder.
Ninaogopa kwamba kwa namna fulani nimejitaabisha bure.
12 Vorder ligesom jeg, thi ogsaa jeg er bleven som I, Brødre! jeg beder eder. I have ikke gjort mig nogen Uret.
Ninawasihi, ndugu, muwe kama nilivyo, kwa kuwa pia nimekuwa kama mlivyo. Hamkunikosea.
13 Men I vide, at det var paa Grund af en Kødets Svaghed, at jeg første Gang forkyndte Evangeliet for eder;
Bali mnajua kwamba ilikuwa ni kwa sababu ya ugonjwa wa mwili kwamba nilihubiri injili kwenu kwa mara ya kwanza.
14 og det, som i mit Kød var eder til Fristelse, ringeagtede I ikke og afskyede I ikke, men I modtoge mig som en Guds Engel, som Kristus Jesus.
Ingawa hali yangu ya mwili iliwaweka katika jaribu, hamkunidharau au kunikataa. Badala yake mlinipokea kama malaika wa Mungu, kana kwamba nilikuwa Kristo Yesu mwenyewe.
15 Hvor er da nu eders Saligprisning? Thi jeg giver eder det Vidnesbyrd, at, om det havde været muligt, havde I udrevet eders Øjne og givet mig dem.
Kwa hiyo, iko wapi sasa furaha yenu? kwa kuwa ninashuhudia kwenu kwamba, ikiwezekana, mungelin'goa macho yenu na kunipa mimi.
16 Saa er jeg vel bleven eders Fjende ved at tale Sandhed til eder?
Hivyo sasa, je nimekuwa adui yenu kwa sababu ninawaambia ukweli?
17 De ere nidkære for eder, dog ikke for det gode; men de ville udelukke eder, for at I skulle være nidkære for dem.
Wanawatafuta kwa shauku, bali si kwa mema. Wanataka kuwatenganisha ninyi na mimi ili muwafuate.
18 Men det er godt at vise sig nidkær i det gode til enhver Tid, og ikke alene, naar jeg er nærværende hos eder.
Ni vyema daima kuwa na shauku kwa sababu zilizo njema, na si tu wakati ninapokuwa pamoja nanyi.
19 Mine Børn, som jeg atter føder med Smerte, indtil Kristus har vundet Skikkelse i eder!
Wanangu wadogo, ninaumwa uchungu kwa ajili yenu tena mpaka Kristo aumbike ndani yenu.
20 — ja jeg vilde ønske, at jeg nu var til Stede hos eder og kunde omskifte min Røst; thi jeg er raadvild over for eder.
Ningependa kuwepo pale pamoja nanyi sasa na kugeuza sauti yangu, kwa sababu ninamashaka juu yenu.
21 Siger mig, I, som ville være under Loven, høre I ikke Loven?
Niambieni, ninyi ambao mnatamani kuwa chini ya sheria, hamsikii sheria isemavyo?
22 Der er jo skrevet, at Abraham havde to Sønner, en med Tjenestekvinden og en med den frie Kvinde.
Kwa kuwa imeandikwa kwamba Abrahamu alikuwa na wana wa kiume wawili, mmoja kwa yule mwanamke mtumwa na mwingine kwa mwanamke huru.
23 Men Tjenestekvindens Søn er avlet efter Kødet, den frie Kvindes ved Forjættelsen.
Hata hivyo, yule wa mtumwa alizaliwa kwa mwili tu, bali yule wa mwanamke huru alizaliwa kwa ahadi.
24 Dette har en billedlig Betydning. Thi disse Kvinder ere tvende Pagter, den ene fra Sinai Bjerg, som føder til Trældom: Denne er Hagar.
Mambo haya yanaweza kuelezwa kwa kutumia mfano, kwa kuwa wanawake hawa wanafanana na maagano mawili. Mojawapo kutoka katika mlima Sinai. Huzaa watoto ambao ni watumwa. huyu ni Hajiri.
25 Thi „Hagar” er Sinai Bjerg i Arabien, men svarer til det nuværende Jerusalem; thi det er i Trældom med sine Børn.
Sasa Hajiri ni mlima Sinai ulioko Arabuni. Hufananishwa na Yerusalem ya sasa, kwa kuwa ni mtumwa pamoja na watoto wake.
26 Men Jerusalem heroventil er frit, og hun er vor Moder.
Bali Yerusalemu ambayo iko juu ni huru, na hii ndiyo mama yetu.
27 Thi der er skrevet: „Fryd dig, du ufrugtbare, du, som ikke føder! bryd ud og raab, du, som ikke har Fødselsveer! thi mange ere den enliges Børn fremfor hendes, som har Manden.”
Kwa kuwa imeandikwa, “Furahi, wewe mwanamke uliye tasa, wewe usiye zaa. Paza sauti na upige kelele kwa furaha, wewe ambaye huna uzoefu wa kuzaa. kwa maana wengi ni watoto wa aliye tasa, zaidi ya wale wa yule ambaye ana mume.”
28 Men vi, Brødre! ere Forjættelsens Børn i Lighed med Isak.
Sasa ndugu, kama Isaka, ninyi ni watoto wa ahadi.
29 Men ligesom dengang han, som var avlet efter Kødet, forfulgte ham, som var avlet efter Aanden, saaledes ogsaa nu.
Kwa wakati ule ambao mtu ambaye alizaliwa kwa mujibu wa mwili alimtesa yule aliyezaliwa kwa mujibu wa Roho. Kwa sasa ni vilevile.
30 Men hvad siger Skriften: „Uddriv Tjenestekvinden og hendes Søn; thi Tjenestekvindens Søn skal ingenlunde arve med den frie Kvindes Søn.”
Maandiko husemaje? “Muondoe mwanamke mtumwa pamoja na mwanawe wa kiume. Kwa kuwa mtoto wa mwanamke mtumwa hatarithi pamoja na mtoto wa mwanamke huru.”
31 Derfor, Brødre! ere vi ikke Tjenestekvindens Børn, men den frie Kvindes.
Kwa hiyo, ndugu, sisi si watoto wa mwanamke mtumwa, bali ni wa mwanamke huru.