< Ezekiel 1 >

1 I det tredivte Aar paa den femte Dag i den fjerde Maaned da jeg var blandt de Landflygtige ved Floden Kebar, skete det, at Himmelen aabnede sig, og jeg skuede Syner fra Gud.
Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.
2 Den femte Dag i Maaneden — det var det femte Aar efter at Kong Jojakin var bortført —
Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini,
3 kom HERRENS Ord til Præsten Ezekiel, Buzis Søn, i Kaldæernes Land ved Floden Kebar, og HERRENS Haand kom over ham der.
neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.
4 Jeg skuede og se, et Stormvejr kom fra Nord, og en vældig Sky fulgte med, omgivet af Straaleglans og hvirvlende Ild, i hvis Midte det glimtede som funklende Malm.
Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto.
5 Midt i Ilden var der noget ligesom fire levende Væsener, og de saa saaledes ud: De havde et Menneskes Skikkelse;
Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu,
6 men de havde hver fire Ansigter og fire Vinger;
lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne.
7 deres Ben var lige og deres Fodsaaler som en Kalvs; de skinnede som funklende Kobber, og deres Vingeslag var hurtigt;
Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa.
8 der var Menneskehænder under Vingerne paa alle fire Sider.
Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa,
9 De fire levende Væseners Ansigter vendte sig ikke, naar de gik, men de gik alle lige ud.
nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.
10 Ansigterne saa saaledes ud: De havde alle fire et Menneskeansigt fortil, et Løveansigt til højre, et Okseansigt til venstre og et Ørneansigt bagtil;
Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai.
11 Vingerne var paa dem alle fire udbredt opad, saaledes at to og to rørte hinanden, og to skjulte deres Legemer.
Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake.
12 De gik alle lige ud; hvor Aanden vilde have dem hen gik de; de vendte sig ikke, naar de gik.
Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka.
13 Midt imellem de levende Væsener var der noget som glødende Kul at se til, som Blus, der for hid og did imellem dem, og Ilden udsendte Straaleglans, og Lyn for ud derfra.
Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi.
14 Og Væsenerne løb frem og tilbage, som Lynglimt at se til.
Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.
15 Videre skuede jeg, og se, der var et Hjul paa Jorden ved Siden af hvert af de fire levende Væsener;
Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne.
16 og Hjulene var at se til som funklende Krysolit; de saa alle fire ens ud, og de var lavet saaledes, at der i hvert Hjul var et andet Hjul;
Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake.
17 de kunde derfor gaa til alle fire Sider; de vendte sig ikke, naar de gik.
Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda.
18 Videre skuede jeg, og se, der var Fælge paa dem, og Fælgene var paa dem alle fire rundt om fulde af Øjne.
Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.
19 Og naar de levende Væsener gik, gik ogsaa Hjulene ved Siden af, og naar Væsenerne løftede sig fra Jorden, løftede ogsaa Hjulene sig;
Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka.
20 hvor Aanden vilde have dem hen, gik Hjulene, og de løftede sig samtidig, thi det levende Væsens Aand var i Hjulene;
Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
21 naar Væsenerne gik, gik ogsaa de; naar de standsede, standsede ogsaa de, og naar de løftede sig fra Jorden, løftede ogsaa Hjulene sig samtidig, thi det levende Væsens Aand var i Hjulene.
Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
22 Oven over Væsenernes Hoveder var der noget ligesom en Himmelhvælving, funklende som Krystal, udspændt oven over deres Hoveder;
Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha.
23 og under Hvælvingen var deres Vinger udspændt, den ene mod den anden; hvert af dem havde desuden to, som skjulte deres Legemer.
Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake.
24 Og naar de gik, lød Vingesuset for mig som mange Vandes Brus, som den Almægtiges Røst; det buldrede som en Hær.
Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi, kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.
25 Det drønede oven over Hvælvingen over deres Hoveder; men naar de stod, sænkede de Vingerne.
Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa.
26 Men oven over Hvælvingen over deres Hoveder var der noget som Safir at se til, noget ligesom en Trone, og paa den, ovenover, var der noget ligesom et Menneske at se til.
Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu.
27 Og jeg skuede noget som funklende Malm fra det, der saa ud som hans Hofter, og opefter; og fra det, der saa ud som hans Hofter, og nedefter skuede jeg noget som Ild at se til; og Straaleglans omgav ham.
Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka.
28 Som Regnbuen, der viser sig i Skyen paa en Regnvejrsdag, var Straaleglansen om ham at se til. Saaledes saa HERRENS Herlighedsaabenbarelse ud. Da jeg skuede det, faldt jeg paa mit Ansigt. Og jeg hørte en Røst, som talede.
Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka. Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.

< Ezekiel 1 >