< 2 Mosebog 39 >

1 Af det violette og røde Purpurgarn og det karmoisinrøde Garn tilvirkede de Pragtklæderne til Tjenesten i Helligdommen; og de tilvirkede Arons hellige Klæder, saaledes som HERREN havde paalagt Moses.
Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
2 De tilvirkede Efoden af Guldtraad, violet og rødt Purpurgarn, karmoisinrødt Garn og tvundet Byssus,
Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
3 idet de udhamrede Guldet i Plader og skar Pladerne ud i Traade til at væve ind i det violette og røde Purpurgarn, det karmoisinrøde Garn og det tvundne Byssus ved Kunstvævning.
Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
4 Derpaa forsynede de den med Skulderstykker til at hæfte paa; den blev hæftet sammen ved begge Hjørner.
Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
5 Og dens Bælte, som brugtes, naar den skulde tages paa, var i eet med den og af samme Arbejde, af Guldtraad, violet og rødt Purpurgarn, karmoisinrødt Garn og tvundet Byssus, saaledes som HERREN havde paalagt Moses.
Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
6 Derpaa tilvirkede de Sjohamstenene, indfattede i Guldfletværk og graverede som Signeter med Israels Sønners Navne;
Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
7 og de fæstede dem paa Efodens Skulderstykker, for at Stenene kunde bringe Israels Børn i Minde, saaledes som HERREN havde paalagt Moses.
Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
8 Derpaa tilvirkede de Brystskjoldet i Kunstvævning paa samme Maade som Efoden, af Guldtraad, violet og rødt Purpurgarn, karmoisinrødt Garn og tvundet Byssus;
Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
9 det var firkantet, og de lagde Brystskjoldet dobbelt; det var et Spand langt og et Spand bredt, lagt dobbelt.
Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
10 De udstyrede det med fire Rækker Sten: Karneol, Topas og Smaragd i den første Række,
Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
11 Rubin, Safir og Jaspis i den anden,
safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
12 Hyacint, Agat og Ametyst i den tredje,
safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
13 Krysolit, Sjoham og Onyks i den fjerde, omgivne med Guldfletværk i deres Indfatninger.
katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
14 Der var tolv Sten, svarende til Israels Sønners Navne, en for hvert Navn; det var graveret Arbejde som Signeter, saaledes at hver Sten bar Navnet paa en af de tolv Stammer.
Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
15 Til Brystskjoldet lavede de snoede Kæder af purt Guld, snoet Arbejde, som naar man snor Reb.
Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
16 Derpaa lavede de to Guldfletværker og to Guldringe og satte disse to Ringe paa Brystskjoldets øverste Hjørner,
Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
17 og de to Guldsnore knyttede de i de to Ringe paa Brystskjoldets Hjørner;
Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
18 Snorenes anden Ende anbragte de i de to Fletværker og fæstede dem paa Forsiden af Efodens Skulderstykker.
nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
19 Og de lavede to andre Guldringe og satte dem paa Brystskjoldets to andre Hjørner paa den indre Rand, der vendte mod Efoden.
Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
20 Og de lavede endnu to Guldringe og fæstede dem paa Efodens to Skulderstykker forneden paa Forsiden, hvor den var hæftet sammen med Skulderstykkerne, oven over Efodens Bælte;
Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
21 og de bandt med Ringene Brystskjoldet fast til Efodens Ringe ved Hjælp af en violet Purpursnor, saa at det kom til at sidde oven over Efodens Bælte og ikke kunde løsne sig fra Efoden, som HERREN havde paalagt Moses.
Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
22 Derpaa tilvirkede de Kaaben, som hører til Efoden, i vævet Arbejde, helt og holdent af violet Purpur.
Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
23 Midt paa havde Kaaben en Halsaabning ligesom Halsaabningen paa en Panserskjorte, omgivet af en Linning, for at den ikke skulde rives itu,
na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
24 og langs Kaabens nederste Kant syede de Granatæbler af violet og rødt Purpurgarn, karmoisinrødt Garn og tvundet Byssus,
Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
25 og de lavede Bjælder af purt Guld, som de anbragte mellem Granatæblerne langs Kaabens nederste Kant hele Vejen rundt, mellem Granatæblerne,
Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
26 saa at Bjælder og Granatæbler skiftede hele Vejen rundt langs Kaabens nederste Kant, til at bære ved Tjenesten, som HERREN havde paalagt Moses.
Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
27 Derpaa tilvirkede de Kjortlerne til Aron og hans Sønner af Byssus i vævet Arbejde,
Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
28 Hovedklædet af Byssus, Embedshuerne af Byssus, Linnedbenklæderne af tvundet Byssus,
na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
29 og Bæltet af tvundet Byssus, violet og rødt Purpurgarn og karmoisinrødt Garn i broget Vævning, som HERREN havde paalagt Moses.
Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
30 Derpaa lavede de Pandepladen, det hellige Diadem, af purt Guld og forsynede den med en Indskrift i graveret Arbejde som ved Signeter: »Helliget HERREN.«
Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
31 Og de fæstede en violet Purpursnor paa den til at binde den fast med oven paa Hovedklædet, som HERREN havde paalagt Moses.
Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
32 Saaledes fuldførtes alt Arbejdet ved Aabenbaringsteltets Bolig; og Israeliterne gjorde ganske som HERREN havde paalagt Moses; saaledes gjorde de.
Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
33 Derpaa bragte de Boligen til Moses, Teltdækket med alt dets Tilbehør, Knagerne, Brædderne, Tværstængerne, Pillerne og Fodstykkerne,
Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
34 Dækket af rødfarvede Væderskind og Dækket af Tahasjskind, det indre Forhæng,
kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
35 Vidnesbyrdets Ark med Bærestængerne, Sonedækket,
Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
36 Bordet med alt dets Tilbehør, Skuebrødene,
meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
37 Lysestagen af purt Guld med Lamperne, der skulde sættes paa den, og alt dens Tilbehør, Olien til Lysestagen,
kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
38 Guldalteret, Salveolien, den vellugtende Røgelse, Forhænget til Teltets Indgang,
madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
39 Kobberalteret med Kobbergitteret, Bærestængerne og alt dets Tilbehør, Vandkummen og Fodstykket,
madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
40 Omhængene til Forgaarden, Pillerne og Fodstykkerne, Forhænget til Forgaardens Indgang, Rebene og Teltpælene, alt Tilbehør til Tjenesten i Aabenbaringsteltets Bolig,
mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
41 Pragtklæderne til Tjenesten i Helligdommen, de hellige Klæder til Præsten Aron og hans Sønners Klæder til Præstetjenesten.
na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
42 Nøjagtigt som HERREN havde paalagt Moses, udførte Israeliterne hele Arbejdet.
Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
43 Da saa Moses hele Arbejdet efter, og se, de havde udført det, som HERREN havde sagt; saaledes havde de udført det. Og Moses velsignede dem.
Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.

< 2 Mosebog 39 >