< 2 Mosebog 29 >

1 Saaledes skal du bære dig ad med dem, naar du helliger dem til at gøre Præstetjeneste for mig: Tag en ung Tyr, to lydefri Vædre,
“Hili ndilo utakalofanya ili kuwaweka wakfu makuhani ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani: Chukua fahali mchanga mmoja na kondoo dume wawili wasio na dosari.
2 usyrede Brød, usyrede Kager, rørte i Olie, og usyrede Fladbrød, smurte med Olie; af fint Hvedemel skal du bage dem.
Kutokana na unga laini wa ngano usiotiwa chachu, tengeneza mikate na maandazi yaliyokandwa kwa mafuta, pamoja na mikate midogo myembamba.
3 Læg dem saa i een Kurv og bær dem frem i Kurven sammen med Tyren og de to Vædre.
Viwekwe vyote ndani ya kikapu na kuvitoa pamoja na yule fahali na wale kondoo dume wawili.
4 Lad derpaa Aron og hans Sønner træde hen til Aabenbaringsteltets Indgang og tvæt dem med Vand.
Kisha mlete Aroni na wanawe kwenye lango la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
5 Tag saa Klæderne og ifør Aron Kjortelen, Efodkaaben, Efoden og Brystskjoldet og bind Efoden fast paa ham med Bæltet.
Chukua yale mavazi na umvike Aroni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
6 Læg Hovedklædet om hans Hoved og fæst det hellige Diadem paa Hovedklædet.
Weka kilemba kichwani mwake na kuweka taji takatifu ishikamane na hicho kilemba.
7 Tag saa Salveolien og udgyd den paa hans Hoved og salv ham.
Chukua yale mafuta ya upako umimine juu ya kichwa chake.
8 Lad dernæst hans Sønner træde frem og ifør dem Kjortler,
Walete wanawe na uwavike makoti,
9 omgjord dem med Bælter og bind Huerne paa dem. Og Præsteværdigheden skal tilhøre dem med evig Ret. Saa skal du indsætte Aron og hans Sønner.
pia uwavike zile tepe za kichwani. Ndipo uwafunge Aroni na wanawe mishipi. Ukuhani ni wao kwa agizo la kudumu. Kwa njia hii utamweka wakfu Aroni na wanawe.
10 Før Tyren frem foran Aabenbaringsteltet, og Aron og hans Sønner skal lægge deres Hænder paa Tyrens Hoved.
“Mlete yule fahali mbele ya Hema la Kukutania, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
11 Slagt saa Tyren for HERRENS Aasyn ved Indgangen til Aabenbaringsteltet
Mchinje huyo fahali mbele za Bwana kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
12 og tag noget af Tyrens Blod og stryg det paa Alterets Horn med din Finger og udgyd Resten af Blodet ved Alterets Fod.
Chukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuipaka kwenye pembe za hayo madhabahu kwa kidole chako, na damu iliyobaki uimwage sehemu ya chini ya madhabahu.
13 Tag saa alt Fedtet paa Indvoldene, Leverlappen og begge Nyrerne med Fedtet paa dem og bring det som Røgoffer paa Alteret;
Kisha chukua mafuta yote ya huyo mnyama ya sehemu za ndani, yale yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, uviteketeze juu ya madhabahu.
14 men Tyrens Kød, dens Hud og dens Skarn skal du brænde uden for Lejren. Det er et Syndoffer.
Lakini nyama ya huyo fahali na ngozi yake na matumbo yake utavichoma nje ya kambi. Hii ni sadaka ya dhambi.
15 Derpaa skal du tage den ene Væder, og Aron og hans Sønner skal lægge deres Hænder paa dens Hoved.
“Chukua mmoja wa wale kondoo dume, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
16 Slagt saa Væderen, tag dens Blod og spræng det rundt om paa Alteret.
Mchinje huyo kondoo dume, chukua damu yake na uinyunyize pande zote za hayo madhabahu.
17 Skær saa Væderen i Stykker, tvæt dens Indvolde og Skinneben, læg dem paa Stykkerne og Hovedet
Mkate huyo kondoo dume vipande vipande na usafishe sehemu za ndani pamoja na miguu, ukiviweka pamoja na kichwa na vipande vingine.
18 og bring saa hele Væderen som Røgoffer paa Alteret. Det er et Brændoffer for HERREN; en liflig Duft, et Ildoffer for HERREN er det.
Kisha mteketeze huyo kondoo dume mzima juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
19 Derpaa skal du tage den anden Væder, og Aron og hans Sønner skal lægge deres Hænder paa dens Hoved.
“Mchukue yule kondoo dume mwingine, naye Aroni na wanawe waweke mikono yao juu ya kichwa chake.
20 Slagt saa Væderen, tag noget af dens Blod og stryg det paa Arons og hans Sønners højre Øreflip og paa deres højre Tommelfinger og højre Tommeltaa og spræng Resten af Blodet rundt om paa Alteret.
Mchinje, uchukue sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye masikio ya Aroni na wanawe, kwenye vidole gumba vya mikono yao ya kuume, pia kwenye vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Kisha nyunyiza hiyo damu pande zote za madhabahu.
21 Tag saa noget af Blodet paa Alteret og af Salveolien og stænk det paa Aron og hans Klæder, ligeledes paa hans Sønner og deres Klæder, saa bliver han hellig, han selv og hans Klæder og ligeledes hans Sønner og deres klæder.
Pia chukua sehemu ya damu iliyo juu ya madhabahu na sehemu ya mafuta ya upako, umnyunyizie Aroni na mavazi yake, pia wanawe na mavazi yao. Ndipo Aroni na wanawe pamoja na mavazi yao watakuwa wamewekwa wakfu.
22 Derpaa skal du tage Fedtet af Væderen, Fedthalen, Fedtet paa Indvoldene, Leverlappen, begge Nyrerne med Fedtet paa dem, dertil den højre Kølle, thi det er en Indsættelsesvæder,
“Chukua mafuta ya huyu kondoo dume, mafuta ya mkia, mafuta ya sehemu za ndani yale yanayofunika ini, figo zote mbili na mafuta yake, pamoja na paja la kulia. (Huyo ndiye kondoo dume kwa ajili ya kuwaweka wakfu.)
23 og en Skive Brød, en Oliebrødkage og et Fladbrød af Kurven med de usyrede Brød, som staar for HERRENS Aasyn,
Kutoka kwenye kile kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu, kilichoko mbele za Bwana, chukua mkate, andazi lililokandwa kwa mafuta na mkate mdogo mwembamba.
24 og lægge det alt sammen paa Arons og hans Sønners Hænder og lade dem udføre Svingningen dermed for HERRENS Aasyn.
Viweke vitu hivi vyote mikononi mwa Aroni na wanawe na uviinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
25 Tag det saa igen fra dem og bring det som Røgoffer paa Alteret oven paa Brændofferet til en liflig Duft for HERRENS Aasyn, et Ildoffer er det for HERREN.
Kisha vichukue vitu hivyo kutoka mikononi mwao, uviteketeze juu ya madhabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kupendeza kwa Bwana, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
26 Tag derpaa Brystet af Arons Indsættelsesvæder og udfør Svingningen dermed for HERRENS Aasyn: det skal være din Del.
Baada ya kuchukua kidari cha huyo kondoo dume wa kuwekwa wakfu kwa Aroni, kiinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, nayo itakuwa fungu lako.
27 Saaledes skal du hellige Svingningsbrystet og Offerydelseskøllen, det, hvormed Svingningen udføres, og det, som ydes af Arons og hans Sønners Indsættelsesvæder.
“Weka wakfu zile sehemu za kondoo dume aliyetumika kwa kumweka wakfu Aroni na wanawe: kidari kile kilichoinuliwa na lile paja lililotolewa.
28 Og det skal tilfalde Aron og hans Sønner som en Rettighed, de har Krav paa fra Israeliternes Side til evig Tid; thi det er en Offerydelse, og som Offerydelse skal Israeliterne give det af deres Takofre, som deres Offerydelse til HERREN.
Siku zote hili litakuwa fungu la kawaida kutoka kwa Waisraeli kwa ajili ya Aroni na wanawe. Hili ni toleo la Waisraeli watakalotoa kwa Bwana kutoka sadaka zao za amani.
29 Arons hellige Klæder skal tilfalde hans Sønner efter ham, for at de kan salves og indsættes i dem.
“Mavazi matakatifu ya Aroni yatakuwa ya wazao wake ili kwamba waweze kutiwa mafuta na kuwekwa wakfu wakiwa wameyavaa.
30 I syv Dage skal de bæres af den af hans Sønner, som bliver Præst i hans Sted, den, som skal gaa ind i Aabenbaringsteltet for at gøre Tjeneste i Helligdommen.
Mwana atakayeingia mahali pake kuwa kuhani na kuja kwenye Hema la Kukutania kuhudumu katika Mahali Patakatifu atayavaa kwa siku saba.
31 Saa skal du tage Indsættelsesvæderen og koge dens Kød paa et helligt Sted;
“Chukua nyama ya huyo kondoo dume wa kuwaweka wakfu uipike katika Mahali Patakatifu.
32 og Aron og hans Sønner skal spise Væderens Kød og Brødet i Kurven ved Indgangen til Aabenbaringsteltet;
Aroni na wanawe wataila ile nyama ya huyo kondoo dume pamoja na ile mikate iliyo kwenye hicho kikapu wakiwa hapo ingilio la Hema la Kukutania.
33 de skal spise de Stykker, hvorved der skaffes Soning ved deres Indsættelse og Indvielse, og ingen Lægmand maa spise deraf, thi det er helligt.
Watakula sadaka hizi ambazo upatanisho ulifanywa kwazo kwa ajili ya kuwaweka wakfu na kuwatakasa. Lakini hakuna mtu mwingine yeyote anayeruhusiwa kuvila, kwa sababu ni vitakatifu.
34 Og dersom der bliver noget af Indsættelseskødet eller Brødet tilovers til næste Morgen, da skal du opbrænde det tiloversblevne; spises maa det ikke, thi det er helligt.
Ikiwa nyama yoyote ya huyo kondoo dume iliyotumika kwa kuwaweka wakfu au mkate wowote umebaki mpaka asubuhi, vichomwe. Kamwe visiliwe, kwa sababu ni vitakatifu.
35 Saaledes skal du forholde dig over for Aron og hans Sønner, ganske som jeg har paalagt dig. Syv Dage skal du foretage Indsættelsen;
“Hivyo utamfanyia Aroni na wanawe kila kitu kama vile nilivyokuamuru: Utachukua muda wa siku saba kuwaweka wakfu.
36 daglig skal du ofre en Syndoffertyr til Soning og rense Alteret for Synd ved at fuldbyrde Soningen paa det, og du skal salve det for at hellige det.
Utatoa dhabihu ya fahali kila siku kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho. Takasa madhabahu kwa kufanya upatanisho kwa ajili yake, nayo uitie mafuta na kuiweka wakfu.
37 Syv Dage skal du fuldbyrde Soningen paa Alteret og hellige det; saaledes bliver Alteret højhelligt; enhver, der kommer i Berøring med Alteret, bliver hellig.
Kwa muda wa siku saba fanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuiweka wakfu. Ndipo madhabahu itakuwa takatifu sana na chochote kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.
38 Hvad du skal ofre paa Alteret, er følgende: Hver Dag to aargamle Lam som stadigt Offer.
“Kwa kawaida hiki ndicho utakachotoa juu ya madhabahu kila siku: wana-kondoo wawili wenye umri wa mwaka mmoja.
39 Det ene Lam skal du ofre om Morgenen og det andet ved Aftenstid.
Utamtoa mmoja asubuhi na huyo mwingine jioni.
40 Sammen med det første Lam skal du bringe en Tiendedel Efa fint Hvedemel, rørt i en Fjerdedel Hin Olie af knuste Oliven, og et Drikoffer af en Fjerdedel Hin Vin.
Pamoja na mwana-kondoo wa kwanza utatoa efa moja ya unga wa ngano laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa, pamoja na robo ya hini ya divai kuwa sadaka ya kinywaji.
41 Og det andet Lam skal du ofre ved Aftenstid; sammen med det skal du ofre et Afgrødeoffer og et Drikoffer som om Morgenen til en liflig Duft, et Ildoffer for HERREN.
Huyo mwana-kondoo mwingine mtoe dhabihu wakati wa machweo pamoja na sadaka za unga na za kinywaji kama vile ulivyofanya asubuhi, kuwa harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
42 Det skal være et stadigt Brændoffer, som I skal bringe, Slægt efter Slægt, ved Indgangen til Aabenbaringsteltet for HERRENS Aasyn, hvor jeg vil aabenbare mig for dig for at tale til dig,
“Kwa vizazi vijavyo itakuwa kawaida kutoa sadaka hii ya kuteketezwa kila mara kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Hapo ndipo nitakapokutana na ninyi na kusema nanyi,
43 og hvor jeg vil aabenbare mig for Israels Børn, og det skal helliges ved min Herlighed.
Huko ndipo nitakapokutana na Waisraeli, nalo Hema la Kukutania litatakaswa na utukufu wangu.
44 Jeg vil hellige Aabenbaringsteltet og Alteret, og Aron og hans Sønner vil jeg hellige til at gøre Præstetjeneste for mig.
“Kwa hiyo nitaliweka wakfu Hema la Kukutania pamoja na madhabahu, nami nitamweka wakfu Aroni na wanawe ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani.
45 Og jeg vil bo midt iblandt Israels Børn og være deres Gud;
Ndipo nitakapofanya makao miongoni mwa Waisraeli na kuwa Mungu wao.
46 og de skal kende, at jeg HERREN er deres Gud, som førte dem ud af Ægypten for at bo midt iblandt dem, jeg HERREN deres Gud!
Nao watajua kuwa Mimi Ndimi Bwana Mungu wao, aliyewatoa Misri ili nipate kufanya makao miongoni mwao. Mimi Ndimi Bwana Mungu wao.

< 2 Mosebog 29 >