< Daniel 8 >

1 I Kong Belsazzars tredje Regeringsaar viste der sig et Syn for mig, Daniel; det kom efter det, som tidligere havde vist sig for mig.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Mfalme Belshaza, mimi Danieli, nilipata maono, baada ya maono ambayo yalikuwa yamenitokea mbeleni.
2 Jeg skuede i Synet, og det var mig, som om jeg var i Borgen Susan i Landskabet Elam; og jeg saa mig i Synet staaende ved Floden Ulaj.
Katika maono yangu, nilijiona nikiwa ndani ya ngome ya Shushani katika jimbo la Elamu. Katika maono nilikuwa kando ya Mto Ulai.
3 Da løftede jeg mine Øjne og skuede, og se, en Væder stod ved Floden; den havde to store Horn, det ene større end det andet, og det største skød op sidst.
Nikatazama juu, na hapo mbele yangu kulikuwa na kondoo dume mwenye pembe mbili, akiwa amesimama kando ya mto, nazo pembe zake zilikuwa ndefu. Pembe moja ilikuwa ndefu kuliko hiyo nyingine, lakini iliendelea kukua baadaye.
4 Jeg saa Væderen stange mod Vest, Nord og Syd; intet Dyr kunde modstaa den, ingen kunde redde af dens Vold, og den gjorde, hvad den vilde, og blev mægtig.
Nikamtazama yule kondoo dume alivyokuwa akishambulia kuelekea magharibi, kaskazini na kusini. Hakuna mnyama yeyote aliyeweza kusimama dhidi yake, wala hakuna aliyeweza kuokoa kutoka nguvu zake. Alifanya kama atakavyo, naye akawa mkuu.
5 Videre saa jeg nøje til, og se, en Gedebuk kom fra Vest farende hen over hele Jorden, men uden at røre den; og Bukken havde et anseligt Horn i Panden.
Nilipokuwa ninatafakari hili, ghafula beberu mwenye pembe moja kubwa sana katikati ya macho yake alikuja kutoka magharibi, akiruka kasi juu ya dunia yote bila kugusa ardhi.
6 Den kom hen til den tvehornede Væder, som jeg havde set staa ved Floden, og løb imod den med ubændig Kraft;
Alikuja akimwelekea yule kondoo dume mwenye pembe mbili niliyemwona akisimama kando ya mto, akamshambulia kwa hasira nyingi.
7 og jeg saa, hvorledes den, da den naaede Væderen, rasende stormede imod den, stødte til den og sønderbrød begge dens Horn; og Væderen havde ikke Kraft til at modstaa den, men Bukken kastede den til Jorden og trampede paa den, og ingen reddede Væderen af dens Vold.
Nikamwona akimshambulia yule kondoo dume kwa hasira nyingi, akimpiga yule kondoo dume na kuvunja pembe zake mbili. Yule kondoo dume hakuwa na nguvu za kumzuia yule beberu, hivyo akamwangusha yule kondoo dume chini na kumkanyaga, wala hakuna aliyeweza kumwokoa yule kondoo dume kutoka nguvu za huyo beberu.
8 Derpaa blev Gedebukken saare mægtig; men som den var allermægtigst, brødes det store Horn af, og i Stedet voksede fire andre frem mod alle fire Verdenshjørner.
Yule beberu akawa mkubwa sana, lakini katika kilele cha nguvu zake ile pembe yake ndefu ilivunjika, na mahali pake pakaota pembe nne kubwa kuelekea pande nne za dunia.
9 Men fra det ene af dem skød et andet og lille Horn op, og det voksede umaadeligt mod Syd og Øst og mod det herlige Land;
Kutoka mojawapo ya zile pembe nne palitokea pembe ndogo ukaongezeka nguvu kuelekea kusini, na kuelekea mashariki, na kuelekea Nchi ya Kupendeza.
10 og det voksede helt op til Himmelens Hær, styrtede nogle af Hæren og af Stjernerne til Jorden og trampede paa dem.
Pembe hiyo ikaendelea kukua hadi kufikia jeshi la mbinguni, nayo ikalitupa baadhi ya jeshi la vitu vya angani hapa chini duniani, na kulikanyaga.
11 Og det hovmodede sig mod Hærens Øverste; hans daglige Offer blev ophævet, og hans Helligdoms Sted kastedes til Jorden.
Pembe hiyo ikajikweza ili iwe kama Mkuu wa hilo jeshi; ikamwondolea dhabihu ya kila siku, napo mahali pake patakatifu pakashushwa chini.
12 Og paa Alteret for det daglige Offer lagdes en Misgerning; Sandheden kastedes til Jorden, og Hornet havde Lykke med, hvad det gjorde.
Kwa sababu ya uasi, jeshi la watakatifu na dhabihu za kila siku vikatiwa mikononi mwake. Ikafanikiwa katika kila kitu ilichofanya, nayo kweli ikatupwa chini.
13 Da hørte jeg en hellig tale, og en anden hellig spurgte den talende: »Hvor lang Tid gælder Synet om, at det daglige Offer ophæves, Ødelæggelsens Misgerning opstilles, og Helligdommen og Hæren nedtrampes?«
Kisha nikamsikia mtakatifu mmoja akizungumza na mtakatifu mwingine, akamwambia, “Je, itachukua muda gani maono haya yatimie: maono kuhusu dhabihu ya kila siku, uasi unaosababisha ukiwa, kutwaliwa kwa mahali patakatifu, na jeshi litakalokanyagwa chini ya nyayo?”
14 Han svarede: »2300 Aftener og Morgener; saa skal Helligdommen komme til sin Ret igen!«
Akaniambia, “Itachukua siku 2,300. Ndipo mahali patakatifu patawekwa wakfu tena.”
15 Medens jeg, Daniel, nu saa Synet og søgte at forstaa det, se, da stod der for mig en som en Mand at se til,
Mimi Danieli nilipokuwa ninaangalia maono na kujaribu kuelewa, mbele yangu alisimama mmoja aliyefanana na mwanadamu.
16 og jeg hørte en menneskelig Røst raabe over Ulaj: »Gabriel, udlæg ham Synet!«
Kisha nikasikia sauti ya mwanadamu kutoka Mto Ulai ikiita, “Gabrieli, mwambie mtu huyu maana ya maono haya.”
17 Saa kom han hen, hvor jeg stod, og ved hans Komme blev jeg overvældet af Rædsel og faldt paa mit Ansigt. Og han sagde til mig: »Se nøje til, Menneskesøn, thi Synet gælder Endens Tid!«
Alipokuwa akikaribia pale nilipokuwa nimesimama, niliogopa, nikaanguka kifudifudi. Akaniambia, “Mwana wa mwanadamu, fahamu kuwa maono haya yanahusu siku za mwisho.”
18 Medens han talede med mig, laa jeg bedøvet med Ansigtet mod Jorden; men han rørte ved mig og fik mig paa Benene
Alipokuwa akinena nami, nilikuwa katika usingizi mzito, huku nimelala kifudifudi. Ndipo aliponigusa na kunisimamisha wima.
19 og sagde: »Se, jeg vil kundgøre dig, hvad der skal ske i Vredens sidste Tid; thi Synet gælder Endens bestemte Tid.
Akaniambia, “Nitakuambia yale yatakayotokea baadaye wakati wa ghadhabu, kwa sababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho ulioamriwa.
20 Den tvehornede Væder, du saa, er Kongerne af Medien og Persien,
Kondoo dume mwenye pembe mbili ambaye ulimwona anawakilisha wafalme wa Umedi na Uajemi.
21 den laadne Buk er Kongen af Grækenland, og det store Horn i dens Pande er den første Konge.
Yule beberu mwenye nywele nyingi ni mfalme wa Uyunani, nayo ile pembe ndefu katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
22 At det brødes af, og at fire andre voksede frem i Stedet, betyder, at fire Riger skal fremstaa af hans Folk, dog uden hans Kraft.
Zile pembe nne zilizoota badala ya ile pembe iliyovunjika zinawakilisha falme nne ambazo zitatokea kutoka taifa lake, lakini hakuna hata mmoja utakaokuwa na nguvu kama ule uliovunjika.
23 Men i deres Herredømmes sidste Tid, naar Overtrædelserne har gjort Maalet fuldt, skal en fræk og rænkefuld Konge fremstaa.
“Katika sehemu ya mwisho ya utawala wao, wakati waasi watakapokuwa waovu kabisa, atainuka mfalme mwenye uso mkali, aliye stadi wa hila.
24 Hans Magt skal blive stor, dog ikke som hins; han skal tale utrolige Ting og have Lykke med, hvad han gør, og gennemføre sine Raad og ødelægge mægtige Mænd.
Atakuwa na nguvu nyingi, lakini si kwa uwezo wake mwenyewe. Atasababisha uharibifu wa kutisha, na atafanikiwa kwa chochote anachofanya. Atawaangamiza watu maarufu na watu watakatifu.
25 Mod de hellige skal hans Tanke rettes; hans svigefulde Raad skal lykkes ham, og han skal sætte sig store Ting for og styrte mange i Ulykke i deres Tryghed. Mod Fyrsternes Fyrste skal han rejse sig, men saa skal han knuses, dog ikke ved Menneskehaand.
Atasababisha udanganyifu ustawi, naye atajihesabu mwenyewe kuwa bora. Wakati wajisikiapo kuwa wako salama, atawaangamiza wengi, na kushindana na Mkuu wa wakuu. Lakini ataangamizwa, isipokuwa si kwa uwezo wa mwanadamu.
26 Synet om Aftenerne og Morgenerne, hvorom der var Tale, er Sandhed. Men du skal lukke for Synet; thi det gælder en fjern Fremtid.«
“Maono kuhusu jioni na asubuhi ambayo umepewa ni kweli, lakini yatie muhuri maono haya, kwa maana yanahusu wakati mrefu ujao.”
27 Men jeg, Daniel, laa syg en Tid lang; saa stod jeg op og udførte min Gerning i Kongens Tjeneste. Jeg var rædselslagen over Synet og forstod det ikke.
Mimi Danieli nilikuwa nimechoka sana, na nikalala nikiwa mgonjwa kwa siku kadhaa. Ndipo nikaamka, nikaenda kwenye shughuli za mfalme. Nilifadhaishwa na maono hayo, nami sikuweza kuyaelewa.

< Daniel 8 >