< Første Kongebog 14 >
1 Ved den Tid blev Jeroboams Søn Abija syg.
Wakati ule Abiya mwana wa Yeroboamu akaugua,
2 Da sagde Jeroboam til sin Hustru: »Tag og forklæd dig, saa man ikke kan kende, at du er Jeroboams Hustru, og begiv dig til Silo, thi der bor Profeten Ahija, som kundgjorde mig, at jeg skulde blive Konge over dette Folk;
naye Yeroboamu akamwambia mke wake, “Nenda ukajibadilishe, ili watu wasijue kwamba wewe ni mke wa Yeroboamu. Kisha uende Shilo. Nabii Ahiya yuko huko, yule aliyeniambia kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
3 tag ti Brød, noget Bagværk og en Krukke Honning med og henvend dig til ham, saa vil han sige dig, hvorledes det skal gaa Drengen!«
Chukua mikate kumi, maandazi kadhaa na gudulia la asali na umwendee. Atakuambia kitakachotokea kwa kijana.”
4 Jeroboams Hustru gjorde nu saaledes; hun begav sig til Silo og gik ind i Ahijas Hus. Ahija kunde ikke se, da hans Øjne var sløve af Alderdom;
Basi mke wa Yeroboamu akafanya kama alivyosema mumewe, akaenda kwenye nyumba ya Ahiya huko Shilo. Wakati huu Ahiya alikuwa kipofu naye alishindwa kuona kwa sababu ya umri wake.
5 men HERREN havde sagt til Ahija: »Se, Jeroboams Hustru kommer til dig for at høre sig for hos dig angaaende sin Søn, da han er syg; det og det skal du svare hende; men naar hun kommer, er hun forklædt.«
Lakini Bwana alikuwa amemwambia Ahiya, “Mke wa Yeroboamu anakuja kukuuliza kuhusu mwanawe, kwa kuwa ni mgonjwa, nawe utamjibu hivi na hivi. Atakapowasili, atajifanya kuwa ni mtu mwingine.”
6 Da nu Ahija hørte Lyden af hendes Trin, som hun gik ind ad Døren, sagde han: »Kom kun ind, Jeroboams Hustru! Hvorfor er du forklædt? Mig er det paalagt at bringe dig en tung Tidende.
Hivyo Ahiya aliposikia kishindo cha hatua zake mlangoni, akasema, “Karibu ndani, mke wa Yeroboamu. Kwa nini kujibadilisha? Nimetumwa kwako nikiwa na habari mbaya.
7 Gaa hen og sig til Jeroboam: Saa siger HERREN, Israels Gud: Jeg ophøjede dig af Folkets Midte og gjorde dig til Fyrste over mit Folk Israel
Nenda, ukamwambie Yeroboamu kwamba hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Nilikuinua miongoni mwa watu na kukufanya kiongozi juu ya watu wangu Israeli.
8 og rev Riget fra Davids Hus og gav dig det; dog har du ikke været som min Tjener David, der holdt mine Bud og fulgte mig af hele sit Hjerte og kun gjorde, hvad der er ret i mine Øjne,
Nikararua ufalme kutoka kwa nyumba ya Daudi na kukupa wewe, lakini hukuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye aliyashika maagizo yangu na kunifuata kwa moyo wake wote, akifanya tu lile lililokuwa sawa machoni pangu.
9 men du har handlet værre end alle dine Forgængere; du gik hen og krænkede mig og gjorde dig andre Guder og støbte Billeder, men mig kastede du bag din Ryg;
Umefanya maovu mengi kuliko wote waliokutangulia. Umejitengenezea miungu mingine, sanamu za chuma, umenighadhibisha na kunitupa nyuma yako.
10 se, derfor vil jeg bringe Ulykke over Jeroboams Hus og udrydde hvert mandligt Væsen, hver og en af Jeroboams Slægt i Israel, og jeg vil feje Jeroboams Hus bort, som man fejer Skarn bort, til der ikke er Spor tilbage!
“‘Kwa sababu ya hili, nitaleta maafa juu ya nyumba ya Yeroboamu. Nitakatilia mbali kutoka kwa Yeroboamu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, mtumwa au mtu huru. Nitachoma nyumba ya Yeroboamu mpaka iteketee yote kama mtu achomaye kinyesi.
11 Den af Jeroboams Slægt, som dør i Byen, skal Hundene æde, og den, som dør paa Marken, skal Himmelens Fugle æde, thi det er HERREN, der har talet!
Mbwa watawala wale walio wa nyumba ya Yeroboamu watakaofia ndani ya mji na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani. Bwana amesema!’
12 Men gaa nu hjem! Naar din Fod betræder Byen, skal Barnet dø;
“Kukuhusu wewe, rudi nyumbani. Wakati utakapotia mguu katika mji wako, kijana atakufa.
13 og hele Israel skal holde Dødeklage over ham og jorde ham, thi han er den eneste af Jeroboams Slægt, der skal komme i en Grav; thi hos ham fandtes dog noget, der vandt HERREN Israels Guds Behag inden for Jeroboams Slægt.
Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Kwa sababu ni yeye pekee wa nyumba ya Yeroboamu atakayezikwa, kwa sababu ni yeye peke yake ndani ya nyumba ya Yeroboamu ambaye Bwana, Mungu wa Israeli, ameona kitu chema kwake.
14 Men HERREN vil oprejse sig en Konge over Israel, der skal udrydde Jeroboams Hus paa den Dag.
“Bwana atajiinulia mwenyewe mfalme juu ya Israeli ambaye ataikatilia mbali jamaa ya Yeroboamu. Siku ndiyo hii! Nini? Naam, hata sasa hivi.
15 Men ogsaa siden vil HERREN slaa Israel, saa at de svajer hid og did som Sivet i Vandet, og rykke Israel op fra dette herlige Land, som han gav deres Fædre, og sprede dem hinsides Floden, fordi de har lavet sig Asjerastøtter og krænket HERREN;
Naye Bwana ataipiga Israeli, hata iwe kama unyasi unaosukwasukwa juu ya maji. Ataingʼoa Israeli kutoka nchi hii nzuri aliyowapa baba zao na kuwatawanya ngʼambo ya Mto Frati, kwa sababu wamemghadhibisha Bwana kwa kutengeneza nguzo za Ashera
16 og han vil give Israel til Pris for de Synders Skyld, Jeroboam har begaaet og forledt Israel til.«
Naye atawaacha Israeli kwa ajili ya makosa ya Yeroboamu aliyoyatenda na kusababisha Israeli kuyatenda.”
17 Da gav Jeroboams Hustru sig paa Vej og kom til Tirza; og da hun betraadte Husets Tærskel, døde Drengen;
Kisha mke wa Yeroboamu akainuka, akaondoka kwenda Tirsa. Mara alipokanyaga kizingiti cha mlango, kijana akafa.
18 og man jordede ham, og hele Israel holdt Dødeklage over ham efter det Ord, HERREN havde talet ved sin Tjener, Profeten Ahija.
Wakamzika na Israeli yote ikamwombolezea, kama Bwana alivyokuwa amesema kupitia mtumishi wake, nabii Ahiya.
19 Hvad der ellers er at fortælle om Jeroboam, hvorledes han førte Krig, og hvorledes han herskede staar jo optegnet i Israels Kongers Krønike.
Matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, vita vyake na jinsi alivyotawala, vimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
20 Jeroboams Regeringstid udgjorde to og tyve Aar. Saa lagde han sig til Hvile hos sine Fædre, og hans Søn Nadab blev Konge i hans Sted.
Yeroboamu akawatawala kwa miaka ishirini na miwili, kisha akalala na baba zake. Naye Nadabu mwanawe akawa mfalme baada yake.
21 Rehabeam, Salomos Søn, blev Konge i Juda. Rehabeam var een og fyrretyve Aar gammel, da han blev Konge, og han herskede sytten Aar i Jerusalem, den By, HERREN havde udvalgt af alle Israels Stammer for der at stedfæste sit Navn. Hans Moder var en ammonitisk Kvinde ved Navn Na'ama.
Rehoboamu mwana wa Solomoni alikuwa mfalme wa Yuda. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipoanza kutawala, naye akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua kutoka makabila yote ya Israeli ili apate kuliweka humo Jina lake. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni.
22 Og Juda gjorde, hvad der var ondt i HERRENS Øjne, og med de Synder, de begik, vakte de hans Nidkærhed, mere end deres Fædre havde gjort.
Yuda wakatenda maovu machoni pa Bwana. Kwa dhambi walizotenda wakachochea hasira yake yenye wivu zaidi kuliko baba zao walivyofanya.
23 Ogsaa de byggede sig Offerhøje, Stenstøtter og Asjerastøtter paa alle høje Steder og under alle grønne Træer;
Pia wakajijengea mahali pa juu pa kuabudia miungu, mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kilichoinuka na kila mti uliotanda.
24 ja, der var endog Mandsskøger i Landet. De øvede alle de Vederstyggeligheder, som var begaaet af de Folk, HERREN havde drevet bort foran Israeliterne.
Walikuwepo hata wanaume mahanithi wa mahali pa ibada za sanamu katika nchi; watu wakajiingiza katika kutenda machukizo ya mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli.
25 Men i Kong Rehabeams femte Regeringsaar drog Ægypterkongen Sjisjak op imod Jerusalem
Katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu.
26 og tog Skattene i HERRENS Hus og i Kongens Palads; alt tog han, ogsaa de Guldskjolde, Salomo havde ladet lave.
Akachukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao zote za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
27 Kong Rehabeam lod da i Stedet lave Kobberskjolde og gav dem i Forvaring hos Høvedsmændene for Livvagten, der holdt Vagt ved Indgangen til Kongens Palads;
Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
28 og hver Gang Kongen begav sig til HERRENS Hus, hentede Livvagten dem, og bagefter bragte de dem tilbage til Vagtstuen.
Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana, walinzi walizichukua hizo ngao, na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
29 Hvad der ellers er at fortælle om Rehabeam, alt, hvad han gjorde, staar jo optegnet i Judas Kongers Krønike.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Rehoboamu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
30 Rehabeam og Jeroboam laa i Krig med hinanden hele Tiden.
Kulikuwa na vita vinavyoendelea kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
31 Saa lagde Rehabeam sig til Hvile hos sine Fædre og blev jordet hos sine Fædre i Davidsbyen. Hans Moder var en ammonitisk Kvinde ved Navn Na'ama. Og hans Søn Abija blev Konge i hans Sted.
Naye Rehoboamu akalala na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.