< Første Krønikebog 26 >

1 Dørvogternes Skifter var følgende: af Koraiterne Mesjelemja, en Søn af Kore af Abi'asafs Sønner.
Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.
2 Mesjelemja havde Sønner: Zekarja den førstefødte, Jediael den anden, Zebadja den tredje, Jatniel den fjerde,
Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,
3 Elam den femte, Johanan den sjette og Eljoenaj den syvende.
Elamu wa tano Yehohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.
4 Obed-Edom havde Sønner: Sjemaja den førstefødte, Jozabad den anden, Joa den tredje, Sakar den fjerde, Netan'el den femte,
Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,
5 Ammiel den sjette, Issakar den syvende og Pe'ulletaj den ottende; thi Gud havde velsignet ham.
Amieli wa sita, Isakari wa saba, na Peulethai wa nane. (Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)
6 Hans Søn Sjemaja fødtes Sønner, som var Herskere i deres Fædrenehus, da de var dygtige Folk.
Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.
7 Sjemajas Sønner var: Otni, Refael, Obed, Elzabad og hans Brødre, dygtige Folk, Elihu og Semakja;
Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.
8 alle disse hørte tillige med deres Sønner og Brødre til Obed-Edoms Sønner, dygtige Folk med Evner til Tjenesten, i alt to og tresindstyve Efterkommere af Obed-Edom.
Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.
9 Mesjelemja havde Sønner og Brødre, dygtige Folk, atten.
Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.
10 Hosa at Meraris Sønner havde Sønner: Sjimri, som var Overhoved — thi skønt han ikke var den førstefødte, gjorde hans Fader ham til Overhoved —
Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),
11 Hilkija den anden, Tebalja den tredje og Zekarja den fjerde. Hosas Sønner og Brødre var i alt tretten.
Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.
12 Disse Dørvogternes Skifter, deres Overhoveder sammen med deres Brødre, blev Vagttjenesten overdraget, og saaledes gjorde de Tjeneste i HERRENS Hus;
Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Bwana kama jamaa zao walivyokuwa nazo.
13 og om hver enkelt Port kastede de Lod mellem smaa som store, efter deres Fædrenehuse.
Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.
14 Loddet for Østporten ramte Sjelemja. Ogsaa for hans Søn Zekarja, en klog Raadgiver, kastede man Lod, og Loddet traf Nordporten.
Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.
15 For Obed-Edom traf det Sydporten og for hans Sønner Forraadskamrene.
Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.
16 Og for Hosa traf Loddet Vestporten tillige med Sjalleketporten ved Vejen, der fører opad, den ene Vagtpost ved den anden.
Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa. Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa:
17 Mod Øst var der seks Leviter, mod Nord daglig fire, mod Syd daglig tre, ved hvert af Forraadskamrene to,
Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.
18 ved Parbar mod Vest var der fire ved Vejen, to ved Parbar.
Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.
19 Det var Dørvogternes Skifter af Koraiternes og Meraris Efterkommere.
Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.
20 Deres Brødre Leviterne, som havde Tilsyn med Guds Hus's Skatkamre og Skatkamrene til Helliggaverne:
Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
21 Ladans Sønner, Gersoniternes Efterkommere gennem Ladan, Overhovederne for Gersoniten Ladans Fædrenehuse: Jehieliterne.
Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli,
22 Jehieliternes Sønner Zetam og hans Broder Joel havde Tilsynet med HERRENS Hus's Skatte.
wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Bwana.
23 Af Amramiterne, Jizhariterne, Hebroniterne og Uzzieliterne
Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:
24 var Sjubael, en Søn af Moses's Søn Gersom, Overopsynsmand over Skattene.
Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.
25 Hans fra Eliezer nedstammende Brødre: Hans Søn Rehabja, hans Søn Jesja'ja, hans Søn Joram, hans Søn Zikri, hans Søn Sjelomit.
Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi.
26 Denne Sjelomit og hans Brødre havde Tilsynet med de Skatte af Helliggaver, som Kong David, Fædrenehusenes Overhoveder, Tusind- og Hundredførerne og Hærførerne havde helliget —
Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.
27 de havde helliget dem af Krigsbyttet til Hjælp ved Bygningen at HERRENS Hus —
Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana.
28 og med alt, hvad Seeren Samuel, Saul, Kisj's Søn, Abner, Ners Søn, og Joab, Zerujas Søn, havde helliget; alt, hvad der var helliget, var betroet Sjelomit og hans Brødre.
Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.
29 Af Jizhariterne udtoges Konanja og hans Sønner til Arbejdet ude i Israel som Fogeder og Dommere.
Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.
30 Af Hebroniterne var Hasjabja og hans Brødre, 1700 dygtige Folk, sat til at varetage alt, hvad der vedrørte HERRENS Tjeneste og Kongens Tjeneste i Israel vesten for Jordan.
Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote za Bwana na utumishi wa mfalme.
31 Til Hebroniterne hørte Jerija, Overhovedet for Hebroniterne, efter deres Nedstamning, efter Fædrenehusene — i Davids fyrretyvende Regeringsaar blev der iværksat en Undersøgelse angaaende dem, og der fandtes dygtige Folk iblandt dem i Ja'zer i Gilead —
Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.
32 og hans Brødre, 2700 dygtige Folk, Overhoveder for Fædrenehusene; dem satte Kong David over Rubeniterne, Gaditerne og Manasses halve Stamme til at varetage alle Sager, som vedrørte Gud og Kongen.
Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.

< Første Krønikebog 26 >