< Salme 50 >
1 En Psalme af Asaf. Den Almægtige, Gud Herren har talt og kaldet ad Jorden, fra Solens Opgang indtil dens Nedgang.
Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
2 Fra Zion, Skønhedens Krone, aabenbarede Gud sig herligt.
Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
3 Vor Gud skal komme og ikke tie; en Ild for hans Ansigt skal fortære, og omkring ham stormer det saare.
Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
4 Han kalder ad Himmelen oventil og ad Jorden for at dømme sit Folk.
Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
5 „Samler mig mine hellige, som have sluttet Pagt med mig ved Offer‟.
“Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
6 Og Himlene kundgjorde hans Retfærdighed; thi Gud, han er Dommer. (Sela)
Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
7 Hør, mit Folk, og jeg vil tale; Israel! og jeg vil vidne imod dig; jeg er Gud, din Gud.
“Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
8 Jeg vil ikke gaa i Rette med dig for dine Slagtofre og for dine Brændofre, som ere altid for mig.
Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
9 Jeg vil ikke tage en Okse af dit Hus, ej heller Bukke af dine Stalde.
Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
10 Thi alle Dyrene i Skoven høre mig til, Dyrene paa Bjergene i Tusindtal.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
11 Jeg kender alle Fuglene paa Bjergene, og hvad der vrimler paa Marken, er hos mig.
Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
12 Dersom jeg hungrede, vilde jeg ikke sige dig det; thi Jorderige hører mig til og dets Fylde.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
13 Skulde jeg vel æde Oksers Kød eller drikke Bukkes Blod?
Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
14 Offer Gud Taksigelse og betal den Højeste dine Løfter!
Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
15 Og kald paa mig paa Nødens Dag; jeg vil udfri dig, og du skal ære mig.
na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
16 Men til den ugudelige siger Gud: Hvad kommer det dig ved at tale om mine Skikke og at tage min Pagt i din Mund,
Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
17 da du dog hader Tugt og kaster mine Ord bag dig?
Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
18 Dersom du ser en Tyv, da er du Ven med ham, og med Horkarle er din Del.
Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
19 Du skikker din Mund til ondt, og med din Tunge digter du Svig.
Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
20 Du sidder og taler imod din Broder, du sætter Klik paa din Moders Søn.
Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
21 Disse Ting har du gjort, og jeg har tiet; du har tænkt, at jeg vel var som du; men jeg vil straffe dig og stille det frem for dine Øjne.
Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
22 Forstaar dog dette, I, som have glemt Gud! at jeg ikke skal rive bort, og der ingen er, som frier.
“Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
23 Den, som ofrer Taksigelse, han ærer mig, og den, som agter paa Vejen, ham vil jeg lade se Guds Frelse.
Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”