< Salme 33 >

1 Synger med Fryd, I retfærdige, i Herren! Lovsang sømmer sig for de oprigtige.
Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
2 Takker Herren med Harpe; og leger for ham paa Psaltre med ti Strenge.
Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
3 Synger ham en ny Sang, leger lifligt paa Strengeleg med Frydeklang.
Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
4 Thi Herrens Ord er ret, og al hans Gerning er trofast.
Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
5 Han elsker Retfærdighed og Dom; Jorden er fuld af Herrens Miskundhed.
Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
6 Himlene ere gjorte ved Herrens Ord og al deres Hær ved hans Munds Aande.
Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
7 Han holder Vandet sammen i Havet som en Dynge; han lægger de dybe Vande i Forraadskamre.
Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
8 Al Jorden frygte Herren! alle Verdens Indbyggere bæve for ham!
Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
9 Thi han talte, og det skete; han bød, saa stod det der.
Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
10 Herren gjorde Hedningernes Raad til intet, han forstyrrede Folkenes Tanker.
Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
11 Herrens Raad bestaar evindelig, hans Hjertes Tanker fra Slægt til Slægt.
Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
12 Saligt er det Folk, hvis Gud Herren er, det Folk, som han udvalgte sig til Arv.
Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
13 Herren skuede ud fra Himmelen, han saa alle Menneskens Børn.
Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
14 Han saa ned fra sit Højsæde til alle Jordens Indbyggere.
kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
15 Han er den, som danner deres Hjerter til Hobe, som agter paa alle deres Gerninger.
yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
16 En Konge frelses ikke ved stor Magt, en vældig fries ikke ved stor Kraft.
Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
17 Hesten slaar fejl til Frelse og kan ikke redde ved sin store Styrke.
Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
18 Se, Herrens Øje er til dem, som ham frygte, som haabe paa hans Miskundhed,
Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
19 for at fri deres Sjæl fra Død og holde dem i Live i Hungersnøden.
ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
20 Vor Sjæl bier efter Herren, han er vor Hjælp og vort Skjold.
Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
21 Thi i ham glædes vort Hjerte; thi vi forlade os paa hans hellige Navn.
Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
22 Herre! din Miskundhed være over os, ligesom vi haabe paa dig!
Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.

< Salme 33 >