< Salme 31 >

1 Til Sangmesteren; en Psalme af David. Herre! jeg tror paa dig, lad mig ikke beskæmmes evindelig; udfri mig ved din Retfærdighed.
Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
2 Bøj dit Øre til mig, red mig hastelig; vær mig en fast Klippe, en sikker Borg til at frelse mig.
Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
3 Thi du er min Klippe og min Befæstning, og for dit Navns Skyld vil du lede mig og føre mig.
Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
4 Du vil udføre mig af Garnet, som de have skjult for mig; thi du er min Styrke.
Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
5 I din Haand befaler jeg min Aand; du forløste mig, Herre, du sande Gud!
Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
6 Jeg hader dem, som tage Vare paa Løgnens Gøglebilleder; men paa Herren forlader jeg mig.
Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
7 Jeg vil fryde mig og være glad ved din Miskundhed; thi du har set min Elendighed, du har kendt min Sjæleangest.
Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
8 Du overantvordede mig ikke i Fjendens Haand; du lod mine Fødder staa paa et vidt Rum.
Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
9 Herre! vær mig naadig, thi jeg er angest; hentæret af Sorg er mit Øje, min Sjæl og min Krop.
Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
10 Thi mit Liv er svundet hen i Bedrøvelse og mine Aar i Suk; min Kraft er brudt for min Misgernings Skyld, og mine Ben ere hentørrede.
Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
11 Ved alle mine Fjender er jeg bleven til Spot, og det i rigt Maal for mine Naboer og til Forskrækkelse for mine Kyndinge; de, som saa mig udenfor, flyede fra mig.
Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
12 Jeg blev glemt, ude af Sinde som en død, jeg var som et Kar, der gaar tabt.
Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
13 Thi jeg hørte manges Bagtalelse, der var Rædsel trindt omkring; idet de raadsloge sammen over mig, tænkte de at tage Livet af mig.
Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
14 Men jeg forlader mig paa dig, Herre! jeg sagde: Du er min Gud.
Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
15 Mine Tider ere i din Haand; red mig fra mine Fjenders Haand og fra dem, som forfølge mig.
Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
16 Lad dit Ansigt lyse over din Tjener; frels mig ved din Miskundhed.
Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
17 Herre! lad mig ikke beskæmmes, thi jeg har kaldt paa dig; lad de ugudelige beskæmmes, lad dem tie i Dødsriget. (Sheol h7585)
Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol h7585)
18 Lad de falske Læber blive stumme, som tale frækt i Hovmod og Foragt imod den retfærdige.
Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
19 Hvor stor er din Godhed, som du har gemt for dem, som dig frygte, hvilken du har udvist imod dem, som tro paa dig, for Menneskens Børn.
Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
20 Du vil skjule dem i dit Ansigts Skjul for Menneskers Sammensværgelser; du vil gemme dem i en Hytte for Tungers Kiv.
Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
21 Lovet være Herren! thi han har underligt bevist sin Miskundhed imod mig i en fast Stad.
Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
22 Og jeg sagde, der jeg var forfærdet: Jeg er udryddet fra dine Øjne; men du hørte mine ydmyge Begæringers Røst, da jeg raabte til dig.
Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
23 Elsker Herren, alle hans hellige! Herren bevarer de trofaste og betaler i Overmaal ham, som øver Hovmod.
Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
24 Værer frimodige, og han skal styrke eders Hjerte, alle I, som haabe paa Herren!
Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.

< Salme 31 >