< Salme 135 >

1 Lover Herrens Navn, lover, I Herrens Tjenere!
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 I, som staa i Herrens Hus, i vor Guds Hus's Forgaarde.
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Lover Herren; thi Herren er god; lovsynger hans Navn; thi det er lifligt.
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 Thi Herren har udvalgt sig Jakob, Israel til sin Ejendom.
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 Thi jeg ved, at Herren er stor, og at vor Herre er større end alle Guder.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 Herren gør alt, hvad ham behager, i Himmelen og paa Jorden, i Havene og i alle Afgrunde.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 Han gør, at Dampe opstige fra Jordens Grænse; han gør Lynene til Regn, han udfører Vejret af sine Forraadskamre.
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 Han, som slog de førstefødte i Ægypten, baade Mennesker og Dyr;
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 han sendte Tegn og underlige Ting i din Midte, Ægypten! paa Farao og paa alle hans Tjenere;
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 han, som slog mange Folk og ihjelslog stærke Konger:
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 Amoriternes Konge Sihon og Basans Konge Og samt alle Riger i Kanaan;
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 og han gav deres Land til Arv, til Arv for sit Folk Israel.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 Herre! dit Navn bliver evindelig; Herre! din Ihukommelse bliver fra Slægt til Slægt.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 Thi Herren skal dømme sit Folk, og det skal angre ham for hans Tjeneres Skyld.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 Hedningernes Afguder ere Sølv og Guld, et Menneskes Hænders Gerning.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 De have Mund, men tale ikke; de have Øjne, men se ikke.
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 De have Øren, men høre ikke, og der er ingen Aande i deres Mund.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Ligesom disse ere, saa blive de, som gøre dem, ja, hver den, som forlader sig paa dem.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Israels Hus! lover Herren; Arons Hus! lover Herren.
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Levis Hus! lover Herren; I, som frygte Herren! lover Herren.
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Lovet være Herren fra Zion, han, som bor i Jerusalem! Halleluja!
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Salme 135 >