< Salme 104 >
1 Min Sjæl, lov Herren; Herre, min Gud! du er saare stor, du har iført dig Majestæt og Herlighed.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 Han ifører sig Lys som et Klædebon, han udbreder Himmelen som et Telt.
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 Han hvælver sine Sale i Vandene; han gør Skyerne til sin Vogn, han vandrer paa Vejrets Vinger.
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 Han gør Vindene til sine Engle, gloende Ild til sine Tjenere.
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 Han grundfæstede Jorden paa dens Grundvold, den skal ikke rokkes i al Evighed.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 Du havde skjult den med Havet som med et Klæde, Vandene stode over Bjergene.
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 De flyede for din Trusel, de fore hastelig bort for din Tordens Røst.
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 Bjergene fore op, Dalene fore ned til det Sted, som du grundfæstede for dem.
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 Du satte en Grænse, hvorover de ikke skulde gaa; de skulde ikke skjule Jorden igen.
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 Han lader Kilder opvælde i Dalene; de rinde imellem Bjergene.
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 De give alle Markens Dyr at drikke, Vildæsler slukke deres Tørst.
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 Over dem bo Himmelens Fugle; ud fra Grenene lade de deres Røst høre.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 Han vander Bjergene fra sine høje Sale; Jorden mættes af dine Gerningers Frugt.
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 Han lader Græs gro for Kvæget og Urter til Menneskens Tjeneste for at fremføre Brød af Jorden.
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 Og Vin glæder et Menneskes Hjerte, hans Ansigt bliver frydefuldt af Olie, og Brød vederkvæger et Menneskes Hjerte.
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 Herrens Træer mættes af Væde, Libanons Cedre, som han har plantet;
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 der hvor Fuglene bygge Rede; Storkens Bo er paa Fyrretræerne.
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 De høje Bjerge ere for Stengederne, Klipperne ere en Tilflugt for Kaninerne.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 Han gjorde Maanen til at bestemme Tiderne, Solen ved sin Nedgang.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 Du gør Mørke, og der bliver Nat, i den krybe alle Skovens Dyr frem.
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 De unge Løver brøle efter Rov og komme for at kræve deres Føde af Gud.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 Solen gaar op, saa trække de sig tilbage og lægge sig i deres Huler.
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 Da gaar Mennesket ud til sin Gerning og til sit Arbejde indtil Aftenen.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 Hvor mange ere dine Gerninger, Herre! du gjorde dem alle viselig; Jorden er fuld af dine Ejendomme.
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 Her er Havet stort og vidt til begge Sider; der er Vrimmel uden Tal, der er Dyr, de smaa med de store.
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 Der gaa Skibene; der er Leviathan, som du dannede til at lege derudi.
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 De vente alle paa dig, at du skal give dem deres Føde i rette Tid.
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 Giver du dem, da sanke de; oplader du din Haand, da mættes de med godt.
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 Skjuler du dit Ansigt, da forfærdes de; tager du Aanden tilbage fra dem, da dø de og vende tilbage til deres Støv.
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 Udsender du din Aand, skabes de, og du fornyer Jordens Skikkelse.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 Herrens Ære blive evindelig, Herren glæde sig over sine Gerninger!
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 Han ser til Jorden, og den bæver; han rører ved Bjergene, og de ryge.
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 Jeg vil synge for Herren, medens jeg lever, jeg vil lovsynge min Gud, medens jeg er til.
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 Maatte min Tale behage ham; jeg vil glædes i Herren.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 Maatte dog Syndere udryddes af Jorden, og ugudelige ikke være ydermere! Min Sjæl, lov Herren! Halleluja.
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.