< 3 Mosebog 23 >
1 Og Herren talede til Mose og sagde:
Yahweh akamwambia Musa:
2 Tal til Israels Børn og sig til dem: Hvad angaar Herrens bestemte Tider, som I skulle udraabe som hellige Sammenkaldelser, da ere disse mine bestemte Tider.
“Zungumza na watu wa Israeli, na uwaambie, 'Hizi ndizo sikukuu zilizoamriwa kwa ajili ya Yahweh, ambazo ni lazima mzitangaze kuwa makusanyiko matakatifu, ni sikukuu zangu za mara kwa mara.
3 Seks Dage skal al Gerning gøres, men paa den syvende Dag er en Hviles Sabbat, en hellig Sammenkaldelse, da skulle I ingen Gerning gøre, den er for Herren en Sabbat i alle eders Boliger.
Mnaweza kufanya kazi kwa siku sita, lakini siku ya saba ni Sabato ya kupumzika kabisa. Usifanye kazi kwa sababu ni Sabato kwa ajili ya Yahweh mahali pote mnaposhi.
4 Disse ere Herrens bestemte Tider, de hellige Sammenkaldelser, som I skulle udraabe til deres bestemte Tider.
Hizi ndizo sikukuu za Yahweh zilizoamriwa, Makusanyiko matakatifu mtakayoyatangaza kwa nyakati zilioamriwa:
5 I den første Maaned, paa den fjortende Dag i Maaneden, mellem de tvende Aftener, da er det Paaske for Herren.
Katika mwenzi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi kwenye mwanga hafifu wa machweo ya jua, ni Pasaka ya Yahweh.
6 Og paa den femtende Dag i denne Maaned er de usyrede Brøds Højtid for Herren; I skulle æde usyrede Brød i syv Dage.
Siku ya kumi na tano ya mwezi ule ule ni sikukuu ya mikate isiotiwa hamira kwa ajili ya Yahweh. Kwa muda wa siku saba mtakula mikate isiotiwa hamira.
7 Paa den første Dag skal være eder en hellig Sammenkaldelse, da skulle I ingen Arbejdsgerning gøre.
Siku ya kwanza ni lazima mjitenge kwa pamoja, hamtafanya kazi ya kawaida.
8 Og I skulle ofre Ildofre for Herren i syv Dage; paa den syvende Dag skal være en hellig Sammenkaldelse, I skulle ikke gøre nogen Arbejdsgerning.
Kwa siku saba mtamletea Yahweh matoleo ya chakula. Siku ya saba ni ya kusanyiko takatifu lililotengwa kwa ajili ya Yahweh, nanyi katika siku hiyo hamtafanya kazi yoyote ya kawaida.”
9 Og Herren talede til Mose og sagde:
Yahweh akamwambia Musa, akisema,
10 Tal til Israels Børn og sig til dem: Naar I komme ind i det Land, som jeg vil give eder, og I høste dets Høst, da skulle I fremføre et Neg af det første af eders Høst til Præsten.
“Sema na watu wa Israeli uwaambie, 'mtakapika kwenye nchi nitakayowapa nyinyi, na mtakapovuna mazao yake, nanyi yawapasa kumletea kuhani fungu la masuke ya nafaka ya matunda yake ya kwanza.
11 Og han skal røre Neget for Herrens Ansigt, for eder til en Behagelighed; den anden Dag efter Sabbaten skal Præsten røre det.
Naye ataliinua hilo fungu la masuke ya nafaka mbele za Yahweh na kulileta kwake, kwa kuwa litakubalika kwa niaba yenu. Nalo litaletwa siku baada ya Sabato ili kwamba kuhani ataliinua na kulileta kwangu.
12 Og I skulle gøre Offer paa den samme Dag, naar I røre Neget, et Lam uden Lyde, aargammelt, til et Brændoffer for Herren,
Siku ile mtakapoliinua lile fungu la masuke ya nafaka na kulileta kwangu, itawabidi kutoa mwana—kondoo dume wa mwaka mmoja na asiye na dosari awe sadaka ya kuteketezwa kwa Yahweh.
13 og dets Madoffer, to Tiendeparter Mel blandet med Olie til et Ildoffer for Herren, til en behagelig Lugt; og dets Drikoffer af Vin, en Fjerdepart af en Hin.
Matoleo ya nafaka yatakuwa sehemu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta, uwe matoleo yaliyofanywa kwa moto kwa Yahweh, ili kutoa harufu nzuri ya kupendeza, pamoja na hiyo kutakuwa na matoleo ya kinywaji ya divai, moja ya nne ya hini.
14 Og I skulle ikke æde Brød eller ristede Aks eller Korn indtil den Dag, indtil I føre eders Guds Offer frem; dette skal være hos eders Efterkommere en evig Skik i alle eders Boliger.
Hamtakula mkate, wala nafaka iliyokaangwa au nafaka mpya hata siku ile mliyoleta matoleo haya kwa Mungu wenu. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu, popote pale mnapoishi.
15 Og I skulle tælle eder fra anden Dagen efter den Sabbat, fra den Dag I bære Rørelsens Neg frem; syv hele Uger skulle de være;
Tangu siku iliyofuata baada ya Sabato—hiyo ilikuwa siku mlipolileta lie fungu la nafaka la matoleo ya kutikiswa—hesabuni majuma saba kamili.
16 til Dagen efter den syvende Uge skulle I tælle halvtredsindstyve Dage: Saa skulle I ofre nyt Madoffer for Herren.
Mtahesabu siku hamsini, ambazo zingekuwa siku baada ya Sabato ya saba. Kisha mtaleta matoleo ya nafaka mpya kwa Yahweh.
17 Af eders Boliger skulle I frembære Rørelsens Brød, der skal være to Brød af to Tiendeparter Mel, med Surdejg skulle de bages; de ere en Førstegrøde for Herren.
Mtaleta kutoka nyumbani mwenu mikate miwili iliyotengenezwa kutokana na mbili za kumi za efa. Ni lazima ifanywe kwa unga laini na uliochanganywa na hamira; zitakuwa matoleo ya kutikiswa ya malimbuko ya kwanza kwa Yahweh.
18 Og I skulle ofre tillige med Brødet syv Lam uden Lyde, aargamle, og en Tyrekalv og to Vædre; de skulle være et Brændoffer for Herren, tillige med deres Madoffer og deres Drikoffer, det er en behagelig Lugts Ildoffer for Herren.
Mtaileta hiyo mikate pamoja na wana—kondoo saba wa mwaka mmoja na wasiokuwa na dosari, fahali mmoja mchanga na dume wa kondoo wawili. Watakuwa matoleo ya kuteketezwa kwa moto kwa Yahweh, pamoja na matoleo yao ya nafaka na matoleo ya kinywaji, matoleo yaliyofanywa kwa moto na kutoa harufu nzuri ya kupendeza kwa Yahweh.
19 Og I skulle lave een Gedebuk til Syndoffer, og to Lam, aargamle, til Takoffer.
Ni lazima mtowe mbuzi dume mmoja kwa ajili ya matoleo ya dhambi, na wana—kondoo dume wawili wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu, wawe matoleo ya ushirika.
20 Og Præsten skal røre dem tillige med Førstegrødens Brød med en Rørelse for Herrens Ansigt, tillige de to Lam; de skulle være helligede Herren og tilhøre Præsten.
Ni lazima kuhani azitikise pamoja na mkate wa malimbuko ya kwanza mbele za Yahweh na kuzileta kwake kuwa matoleo pamoja na kondoo dume wawili. Watakuwa sadaka takatifu kwa Yahweh kwa ajili ya kuhani.
21 Og I skulle kalde sammen paa den Dag, det skal være eder en hellig Sammenkaldelse, I skulle ingen Arbejdsgerning gøre; det skal være en evig Skik i alle eders Boliger hos eders Efterkommere,
Mtatoa tangazo siku iyo hiyo. Kutakuwa na kusanyiko takatifu, na hamtafanya kazi za kawaida. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vya watu wenu mahali pote mnapoishi.
22 Og naar I høste eders Lands Høst, da skal du ikke skære det yderste aldeles op paa din Ager, haar du høster, og ej sanke nøje i din Høst; du skal lade det blive til den fattige og til den fremmede; jeg er Herren eders Gud.
Mtakapovuna mazao ya nchi yenu, Msivune kabisa kabisa pembeni mwa mashamba yenu, wala msivune mazazo ya mavuno yenu. Inawapasa kuyaacha kwa ajili ya masikini na mgeni. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.”
23 Og Herren talede: til Mose og sagde:
Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
24 Tal til Israels Børn og sig: I den syvende Maaned, paa den første Dag i Maaneden, skal der være eder en Hvile, en Basunklang til Ihukommelse, en hellig Sammenkaldelse.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza itakuwa siku ya pumzika makini kwa ajili yenu, kumbukumbu pamoja na kupigwa kwa tarumbeta na kusanyiko takatifu,
25 Og I skulle ingen Arbejdsgerning gøre, og I skulle ofre Ildoffer for Herren.
Hamtafanya kazi ya kawaida, na ni lazima mtoe dhabihu inayofanywa kwa moto kwa Yahweh.”
26 Og Herren talede til Mose og sagde:
Kisha Yahweh akamwambia Musa, akisema,
27 Fremdeles paa den tiende Dag i denne syvende Maaned er det Forligelsens Dag; den skal være eder en hellig Sammenkaldelse, og I skulle ydmyge eders Sjæle, og I skulle ofre Ildoffer for Herren.
“Sasa, siku ya kumi ya mwezi huu wa saba, ni Siku ya Upatanisho. Kutakuwa na kusanyiko takatifu, na ni lazima mjinyenyekeze na kuleta kwa Yahweh matoleo kwa moto.
28 Og I skulle ingen Gerning gøre paa den Dag; thi den er Forligelsens Dag, til at gøre Forligelse for eder, for Herren, eders Guds Ansigt.
Hamtafanya kazi katika siku hiyo kwa sababu ni Siku ya Upatanisho, ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu mbele za Yahweh Mungu wenu.
29 Thi hver Sjæl, som ikke ydmyger sig paa den samme Dag, den skal udryddes fra sit Folk.
Yeyote asiyejinyenyekeza siku hiyo lazima akatiliwe mbali na watu wake.
30 Og hver Sjæl, som gør noget Arbejde paa denne samme Dag, den Sjæl vil jeg ødelægge af hans Folks Midte.
Yeye afanyaye kazi yoyote katika siku hiyo, Mimi, Yahweh, nitamwangamiza atoke miongoni mwa watu wake.
31 I skulle intet Arbejde gøre; det skal være en evig Skik hos eders Efterkommere i alle eders Boliger.
Msifanye kazi ya aina yoyote katika siku hiyo. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu mahali pote mnapoishi.
32 Denne er eder en Hviles Sabbat, at I skulle ydmyge eders Sjæle; paa den niende Dag i Maaneden om Aftenen, fra den ene Aften til anden skulle I hvile paa eders Sabbat.
Siku hii itakuwa Sabato ya pumziko lenye utlivu, na ni lzima siku ya tisa ya mwezi mjinyenyekeze katika majira ya jioni. Tangu jioni hata jioni mtaishika Sabato yenu.”
33 Og Herren talede til Mose og sagde:
Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
34 Tal til Israels Børn og sig: Paa den femtende Dag i denne syvende Maaned er Løvsalernes Højtid i syv Dage for Herren.
“Zungumza na watu ISraeli, uwaambie 'Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba kutakuwa na Sikukuu ya vibanda kwa Yahweh. nayo itadumu siku saba.
35 Paa den første Dag skal være en hellig Sammenkaldelse; I skulle ingen Arbejdsgerning gøre.
Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu. Hamtafanya kazi ya kawaida.
36 I skulle ofre Ildoffer for Herren syv Dage; paa den ottende Dag skal der være eder en hellig Sammenkaldelse, og I skulle ofre Herren Ildoffer, det er Slutningshøjtid, I skulle ingen Arbejdsgerning gøre.
Kwa muda wa siku saba mtatoa dhabihu iliyofanywa kwa moto kwa Yahweh. Siku ya nane kutakuwa na kusanyiko takatifu, nanyi mtato dhabihu iliyofanywa kwa moto kwa Yahweh. Hili ni kusanyiko lenye utulivu, nanyi msifanye kazi yoyote ya kawaida.
37 Disse ere Herrens bestemte Tider, som I skulle udraabe som hellige Sammenkaldelser, at ofre for Herren Ildoffer, Brændoffer og Madoffer, Slagtoffer og Drikoffer, hver Dags Gerning paa sin Dag;
Hizi ndizo sikukuu zilizoamriwa kwa ajili ya Yahweh, ambazo mnapaswa kuzitangaza kuwa ni makusanyiko matakatifu ya kutoa dhabihu kwa moto kwa Yahweh, matoleo ya kuteketezwa na matoleo ya nafaka, dhabihu na matoleo ya vinywaji, kila moja kwa siku yake.
38 foruden Herrens Sabbater og foruden eders Gaver og foruden alle eders Løfter og foruden alle eders frivillige Ofre, som I skulle give Herren.
Sikukuu hizi zitakuwa nyongeza kwa Sabato za Yahweh na zawadi zenu, viapo vyenu vyote, na sadaka zenu zote za hiari mzitoazo kwa Yahweh.
39 Men paa den femtende Dag i den syvende Maaned, naar I samle Jordens Grøde, skulle I højtidelig holde Herrens Højtid syv Dage; paa den første Dag skal være en Hvile og paa den ottende Dag skal være en Hvile.
Kuhusu Sikukuu ya vibanda, siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakapokuwa mmeyakusanya ndani matunda ya nchi, ni lazima muitunze sikukuu hii ya Yehweh kwa muda wa siku saba. Siku ya kwanza itakuwa ya pumziko lenye utulivu, na siku ya nane pia itakuwa ya pumziko lenye utulivu.
40 Og I skulle tage eder paa den første Dag Frugt af skønne Træer, Palmekviste og Grene af løvrige Træer og Vidier ved Bække, og I skulle være glade for Herren eders Guds Ansigt syv Dage.
Siku ya kwanza mtachuma tunda lililobora kutoka kwenye miti, mtakata makuti ya mtende, na matawi ya miti minene yenye majani mengi, na majani ya mierebi kutoka chemchemi za maji, nanyi mtashangilia mbele za Yahweh Mungu wenu kwa siku saba.
41 Og I skulle højtidelig holde denne Højtid for Herren syv Dage om Aaret; til en evig Skik hos eders Efterkommere, i den syvende Maaned skulle I højtidelig holde den.
Kwa muda wa siku saba kila mwaka, mtaisherehekea sikukuu hii kwa Yahweh. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu mahali potepote mtakapoishi. Mtaisherehekea sikukuu hii katika mwezi wa saba.
42 Syv Dage skulle I bo i Hytter, hver indfødt i Israel skal bo i Hytter,
Mtaishi kwenye vibanda vidogovidogo kwa siku saba. Waisraeli wenyeji wa kuzaliwa wote itawapasa kuishi katika vibanda vidogovidogo kwa siku saba,
43 paa det eders Efterkommere skulle vide, at jeg lod Israels Børn bo i Hytter, der jeg udførte dem af Ægyptens Land; jeg er Herren eders Gud.
ili kwamba wazao wenu, kizazi baada ya kizazi, waweze kujifunza nilivyowafanya wana wa Israeli kuishi kwenye vibanda kama hivi nilipowaongoza kutoka katika nchi ya Misri. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.'”
44 Og Mose talede om Herrens bestemte Tider til Israels Børn.
Katika njia hii Musa akazitangaza kwa watu wa ISraeli sikukuu zilizoamria kwa ajili ya Yahweh.