< Josua 21 >
1 Da gik Øversterne for Leviternes Fædrenehuse frem til Eleasar, Præsten, og til Josva, Nuns Søn, og til Øversterne for Fædrenehusene blandt Israels Børns Stammer,
Kisha wakuu wa koo za Walawi walimwendea Eliazari kuhani, na kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli.
2 og de talede til dem i Silo i Kanaans Land og sagde: Herren bød ved Mose, at man skulde give os Stæder at bo udi og deres Marker til vort Kvæg.
Waliwaambia, “Yahweh aliwaagizeni ninyi kwa mkono wa Musa kwamba mtupatieni miji ya kuishi yenye maeneo kwa ajili ya kuchungia ya mifugo.” waliyasema haya huko Shilo katika nchi ya Kanaani.
3 Da gave Israels Børn Leviterne af deres Arv, efter Herrens Mund, disse Stæder og deres Marker.
Hivyo, kwa agizo la Yahweh, watu wa Israeli waliwapa Walawi kutoka katika urithi wa wao miji ifuatayo pamoja na maeneo yao ya kuchungia.
4 Og Lodden kom ud for Kahathiternes Slægter; og Arons, Præstens Børn af Leviterne fik af Judas Stamme og Simeons Stamme og af Benjamins Stamme ved Lodkastningen tretten Stæder.
Upigaji wa kura kwa ajili ya koo za Wakohathi ulileta matokeo haya: makuhani ambao ni wazawa wa Haruni ambao walitokana na Walawi, walipokea miji kumi na mitatu waliopewa kutoka kwa kabila la Yuda, kutoka kabila la Simoni, na kutoka kabila la Benyamini.
5 Men de øvrige Kahaths Børn fik af Efraims Stammes Slægter og af Dans Stamme og af den halve Manasse Stamme ved Lodkastningen ti Stæder.
Koo zilizobaki za Wakohathi walipokea kwa kupiga kura kwa miji kumi kutoka katika kabila za Efraimu, Dani, na kutoka kwa nusu ya kabila la Manase.
6 Og Gersons Børn fik af Isaskars Stammes Slægter og af Asers Stamme og af Nafthali Stamme og af den halve Manasse Stamme i Basan ved Lodkastningen tretten Stæder.
Na watu wazawa wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kwa kupigiwa kura kutoka kwa koo za kabila la Isakari, Asheri, Nafutali, na nusu ya kabila la Manase katika Bashani.
7 Merari Børn efter deres Slægter fik af Rubens Stamme og af Gads Stamme og af Sebulons Stamme tolv Stæder.
Watu waliokuwa wazawa wa Merari walipokea miji kumi na miwili kutoka katika makabila ya Rubeni, Gadi na Zabuloni.
8 Saa gave Israels Børn Leviterne ved Lodkastning disse Stæder og deres Marker, ligesom Herren havde budet ved Mose.
Basi, watu wa Israeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yao ya kuchungia, kwa kupiga kura, kama vile Yahweh alivyokuwa ameagiza kwa mkono wa Musa.
9 Og de gave dem af Judas Børns Stamme og af Simeons Børns Stamme disse Stæder, som man nævnede ved Navn.
Kutoka kwa makabila la Yuda na Simoni, waliwapa nchi katika miji ifuatayo iliyoorodheshwa kwa majina.
10 Og Arons Børn af Kahathiternes Slægter, af Levi Børn, fik disse — thi den første Lod var deres —
Miji hii walipewa wazawa wa Haruni, ambao walikuwa miongoni mwa koo za Wakohathi, ambao walitoka katika kabila la Lawi. Kwa kuwa upigaji wa kura ya kwanza uliwaangukiwa wao.
11 og de gave ham Arba, Anoks Faders Stad, det er Hebron paa Judas Bjerg, og dens Agerland rundt omkring den.
Waisraeli waliwapatia Kiriathi Arba ( Arba alikuwa ni baba wa Anaki), eneo hilo liliitwa pia Hebroni, katika nchi ya milima ya Yuda, pamoja na maeneo ya kulishia mifugo yaliyouzunguka mji.
12 Og Stadens Mark og dens Landsbyer gave de Kaleb, Jefunne Søn, til hans Ejendom.
Lakini mashamba ya mji na vijiji vyake vilikuwa tayari ameshapewa Kalebu mwana Yefune, kama mali yake.
13 Og de gave Arons, Præstens Børn Tilflugtsstaden for Manddrabere Hebron og dens Marker og Libna og dens Marker
Na kwa wana wa Haruni kuhani, waliwapa Hebroni pamoja na eneo lake la kulishia mifugo ambao ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia na Libna pamoja na maeneo ya kulishia mifugo.
14 og Jathir og dens Marker og Esthemoa og dens Marker
Na Yatiri pamoaja na maeno yake ya kuchungia, na Eshitemoa pamoja na maeneo yake ya malisho.
15 og Holon og dens Marker og Debir og dens Marker
Lakini pia waliwapa Holoni pamoja na maeneo yake ya malisho, Debiri pamoja na maeneo yake ya malisho,
16 og Ajin og dens Marker og Jutta og dens Marker og Beth-Semes og dens Marker, ni Stæder af disse to Stammer;
Aini pampoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho. Ilikuwa ni miji kumi na tisa ambayo walipewa kutoka katika makabila haya mawilil.
17 men af Benjamins Stamme: Gibeon og dens Marker, Geba og dens Marker,
Kutoka katika kabilala Benyamini walipewa Gibea pamoja na maeneo yake ya malisho, na Geba pamoja na maeneo yake ya malisho,
18 Anathoth og dens Marker og Almon og dens Marker, fire Stæder.
na Anathothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na amoni pamoja na vitongoji vyake vinne.
19 Alle Præsternes, Arons Børns, Stæder vare tretten Stæder og deres Marker.
Miji waliyopewa makuhani, wana wa Haruni, ilikuwa ni miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumlisha na maeneo yake ya malisho.
20 Men Kahaths Børns Slægter, af Leviterne, de andre af Kahaths Børn, fik de Stæder, som hørte til deres Lod, af Efraims Stamme.
Na kwa ajili ya sehemu ya familia ya Kohathi iliyosalia, wale Walawi walio wa familia ya Kohathi, walipewa miji kutoka katika kabila la Efraimu kwa kupiga kura.
21 Og de gave dem Tilflugtsstaden for Manddrabere Sikem og dens Marker, paa Efraims Bjerg, og Geser og dens Marker
Walipewa Shekemu pamoja na maeneo yake ya malisho katika nchi ya milima ya Efraimu - mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia, na Gezeri pamoja na maeneo yake ya malisho,
22 og Kibzaim og dens Marker og Beth-Horon og dens Marker, fire Stæder;
na Kibzaimu pamoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Horoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa miji minne kwa ujumla wake.
23 og af Dans Stamme: Eltheke og dens Marker, Gibbethon og dens Marker,
Kutoka katika kabila la Dani, ukoo wa Kohathi ulipewa Elteke pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gibethoni pamoja na maeneo yake ya malisho, na
24 Ajalon og dens Marker, Gath-Rimmon og dens Marker, fire Stæder;
Aijaloni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gathrimoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake.
25 og af den halve Manasse Stamme: Thaanak og dens Marker og Gath-Rimmon og dens Marker, to Stæder.
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, ukoo wa Kohathi walipewa miji miwili - Taanaki pamoja na maeneo yake ya malisho na Gathirimoni pamoja na maeneo yake ya malisho.
26 Alle Stæder vare ti og deres Marker for de andre Kahaths Børns Slægter.
Kulikuwa na miji kumi kwa ujumla wake kwa ajili ya koo zilizosalia za Wakohathi, pamoja na maeneo yao ya malisho.
27 Og Gersons Børn af Leviternes Slægter gave de af den halve Manasse Stamme: Tilflugtsstaden for Manddrabere Golan i Basan og dens Marker og Beesthera og dens Marker, to Stæder;
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, jamaa za Gershoni, ambazo hizi zilikuwa ni koo zingine za Walawi, zilipewa Golani katika Bashani pamoja na maeneo yao ya malisho, ni mji wa makimbilio kwa ajili ya mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia, sambamba na Beeshitera pamoja na maeneo yake ya malisho - ilikuwa miji miwili kwa ujumla.
28 og af Isaskars Stamme: Kisjon og dens Marker, Dabrath og dens Marker,
Koo za Gershoni zilipewa pia miji minne kutoka kwa kabila la Isakari - Kishoni sambamba na maeneo yake ya malisho, Daberathi pamoja na maeneo yake ya malisho,
29 Jarmuth og dens Marker, En-Gannim og dens Marker, fire Stæder;
Yarmuthi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Engnimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
30 og af Asers Stamme: Miseal og dens Marker, Abdon og dens Marker,
Kutoka katika kabila la Asheri, walipewa miji minne kwa ujumla - Mishali pamoja na maeneo yake ya malisho, Abdoni pamoja na maeneo yake ya malisho,
31 Helkath og dens Marker, og Rehob og dens Marker, fire Stæder;
Helikathi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Rehobu pamoja na maeneo yake ya malisho.
32 og af Nafthali Stamme: Tilflugtsstaden for Manddrabere Kedes i Galilæa og dens Marker og Hamoth-Dor og dens Marker og Karthan og dens Marker, tre Stæder;
Kutoka kwa kabila la Nafutali, nasaba za Gershoni walipewa miji mitatu kwa ujumla - Kedeshi katika Galilaya pamoja na maeneo yake ya malisho, ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia; na Hamothidori pamoja na maeneo yake ya malisho, na Kartani pamoja na maeneo yake ya malisho.
33 alle Gersoniternes Stæder efter deres Slægter vare tretten Stæder og deres Marker.
Kulikuwa na miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumuisha na maeneo yake ya malisho, kwa ajili ya koo za Gershoni.
34 Men til Merari Børns Slægter, som vare de øvrige af Leviterne, gave de af Sebulons Stamme: Jokneam og dens Marker, Kartha og dens Marker,
Na kwa Walawi waliosalia, koo za Merari waliokuwa wamepewa kutoka katika kabila la Zabuloni: Yokneamu pamoa na maeneo yake ya marisho, Karta pamoja na maeneo yake ya malisho,
35 Dimna og dens Marker, Nahalal og dens Marker, fire Stæder;
Dimna pamoja na maeneo yake ya malisho, na Nahalali pamoja na maeneo yake ya malisho- ilikuwa ni miji minne kwa ujumla.
36 og af Rubens Stamme: Bezer og dens Marker og Jahza og dens Marker,
Kwa mbari za Merari walipewa miji minne kutoka katika kabila la Rubeni: Bezeri pamoja na maeneo yake ya malisho, Yahazi pamoja na maene yake ya malisho,
37 Kedemoth og dens Marker og Mefaath og dens Marker, fire Stæder;
na Kedemothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
38 og af Gads Stamme: Tilflugtsstaden for Manddrabere Ramoth i Gilead og dens Marker og Mahanajim og dens Marker,
Kutoka katika kabila la Gadi walipewa miji ya Ramothi katika Gileadi pamoja na sehemu zake za malisho - huu ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu mwenzake bila kukusudia - na Mahanaimu pamoja na sehemu zake za malisho.
39 Hesbon og dens Marker, Jaeser og dens Marker; alle de Stæder vare fire.
Koo za Merari zilipewa pia Heshiboni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Yazeri pamoja na malisho yake.
40 Alle disse vare Merari Børns Stæder efter deres Slægter, de øvrige af Leviternes Slægter, og deres Lod var tolv Stæder.
Hii ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake. Hii yote ilikuwa ni miji ya koo kadhaa za Merari, ambao walitoka katika kabila la Lawi, miji kumi na miwili walipewa wao kwa kupiga kura.
41 Alle Leviternes Stæder midt i Israels Børns Ejendom, vare otte og fyrretyve Stæder og deres Marker.
Miji waliyopewa Walawi kutoka katikati ya nchi iliyomilikiwa na watu wa Israeli ilikuwa miji arobaini na nane, kujumuisha na sehemu za malisho yao.
42 Disse Stæder laa hver for sig, med deres Marker trindt omkring; saaledes havde det sig med alle disse.
Miji hii kila mmoja ulikuwa na maeneo yake ya malisho kwa kuuzunguka mji. Miji hii yote ilikuwa hivyo.
43 Og Herren gav Israel alt det Land, som han havde svoret at give deres Fædre, og de toge det i Eje og boede derudi.
Basi Yahweh aliwapa Israeli nchi yote ambayo aliwaapia baba zao kuwa atawapa. Waisraeli waliimiliki nchi na wakakaa humo.
44 Og Herren gav dem Rolighed trindt omkring, efter alt det, som han havde svoret deres Fædre; og ingen bestod for deres Ansigt af alle deres Fjender; Herren gav alle deres Fjender i deres Haand.
Kisha Yahweh akawapa pumziko kwa kila upande, kama tu alivyowaahidia baba zao. Hakuna hata adui mmoja atakayeweza kuwashinda. Yawhew aliwatia maadui wao wote mikononi mwao.
45 Der blev ikke et Ord til intet af alle de gode Ord, som Herren havde talet til Israels Hus, det opfyldtes alt sammen.
Hakuna hata kitu kimoja miongoni kwa ahadi nzuri ambazo Yahweh alizisema kwa nyumba ya Israeli ambazo hazikutimia. Ahadi zote zilitimia.