< Josua 13 >
1 Og Josva var gammel, han var kommen til Aars, og Herren sagde til ham: Du er gammel, du er kommen til Aars, og der er saare meget af Landet blevet tilovers at indtage.
Yoshua alipokuwa mzee na umri wake ukiwa umesogea sana, Bwana akamwambia, “Wewe ni mzee sana, na bado kumesalia sehemu kubwa sana za nchi ambazo ni za kutwaliwa.
2 Dette er Landet, som er blevet tilovers: Alle Filisternes Landskaber og alle Gesuriter:
“Nchi iliyosalia ni hii: maeneo yote ya Wafilisti na Wageshuri:
3 Fra Sihon, som flyder foran Ægypten og indtil Ekrons Landemærke mod Norden, som regnes til Kananiterne; de fem Filisters Fyrster: Den Gaziter og den Asdoditer, den Askloniter, den Gathiter og den Ekroniter, og Aviterne;
kutoka Mto Shihori ulioko mashariki mwa Misri, kuelekea kaskazini kwenye eneo la Ekroni, ambayo yote ilihesabika kama ya Wakanaani (maeneo yale matano ya watawala wa Kifilisti, ambayo ni Gaza, Ashdodi, Ashkeloni, Gathi na Ekroni: ndiyo nchi ya Waavi);
4 mod Sønden alt Kananiternes Land og Meara, som hører Zidonierne til, indtil Afek, indtil Amoriternes Landemærke;
kuanzia kusini, nchi yote ya Wakanaani, kuanzia Ara ambayo ni ya Wasidoni, ikienea hadi Afeki, na eneo la Waamori,
5 og Gibliternes Land og det hele Libanon mod Solens Opgang fra Baal-Gad neden for Hermons Bjerg, indtil man kommer til Hamath;
eneo la Wagebali; Lebanoni yote kuelekea mashariki, kuanzia Baal-Gadi chini ya Mlima Hermoni hadi Lebo-Hamathi.
6 alle de, som bo paa Bjergene, fra Libanon indtil de hede Kilder, alle Zidonier; jeg vil fordrive dem fra Israels Børns Ansigt; lad det ikkun falde Israel til Arv, som jeg befalede dig.
“Na kuhusu wakaaji wote katika maeneo ya milima, kuanzia Lebanoni hadi Misrefoth-Maimu, pamoja na eneo lote la Wasidoni, mimi mwenyewe nitawafukuza watoke mbele ya Waisraeli. Hakikisha umegawa nchi hii kwa Israeli kuwa urithi, kama nilivyokuagiza,
7 Saa del nu dette Land til Arv iblandt de ni Stammer og den halve Del af Manasse Stamme;
sasa basi, ligawanye eneo hili kwa yale makabila tisa na ile nusu ya kabila la Manase kuwa urithi.”
8 med hvem Rubeniterne og Gaditerne have taget deres Arv, som Mose gav dem paa hin Side Jordanen mod Østen, ligesom Mose, Herrens Tjener, gav dem den,
Ile nusu nyingine ya Manase, Wareubeni na Wagadi, walishapokea urithi Mose aliokuwa amewapa mashariki mwa Yordani, sawasawa na mtumishi wa Bwana alivyowagawia.
9 fra Aroer, som ligger ved Bredden af Arnons Bæk, og fra den Stad, som er midt i Dalen, og alt det jævne Land ved Medba indtil Dibon,
Eneo lao lilienea toka Aroeri, iliyoko ukingoni mwa Bonde la Arnoni kuanzia mji ulio katikati ya bonde, likijumlisha nchi ya uwanda wa juu wote wa Medeba mpaka Diboni,
10 og alle Stæder, som tilhørte Sihon, Amoriternes Konge, som regerede i Hesbon, indtil Ammons Børns Landemærke;
nayo miji yote ya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala Heshboni, hadi mpakani mwa Waamoni.
11 og Gilead og Gesuriternes og Maakathiternes Landemærke og hele Hermons Bjerg og al Basan indtil Salka,
Vilevile ilijumlisha Gileadi, eneo la Wageshuri na Wamaaka, mlima wote wa Hermoni na Bashani yote ikienea hadi Saleka:
12 hele Ogs Rige i Basan, han som regerede i Astharoth og i Edrei og var een af de overblevne Kæmper. Og Mose slog dem og fordrev dem;
yaani ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyekuwa ametawala katika Ashtarothi na Edrei, na ndiye pekee alisalia kwa Warefai. Mose alikuwa amewashinda na kuteka nchi yao.
13 men Israels Børn fordreve ikke Gesuriterne og Maakathiterne; men Gesur og Maakath boede iblandt Israel indtil denne Dag.
Lakini Waisraeli hawakuwafukuza watu wa Geshuri na wa Maaka, kwa hiyo wanaendelea kuishi miongoni mwa Waisraeli mpaka leo hii.
14 Alene Levi Stamme gav han ikke Arv; Herrens, Israels Guds Ildofre, de ere hans Arv, som han havde sagt til dem.
Lakini kwa kabila la Lawi, Mose hakupeana urithi, kwa kuwa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizotolewa kwa Bwana, Mungu wa Israeli, ndizo zilizokuwa urithi wao, kama alivyowaahidi.
15 Men Mose havde givet Rubens Børns Stamme Arv efter deres Slægter;
Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Reubeni ukoo kwa ukoo:
16 og deres Landemærke var fra Aroer, som ligger ved Bredden af Arnons Bæk, og fra den Stad, som er midt i Dalen, og alt det jævne Land ved Medba,
Eneo la Aroeri lililo ukingoni mwa Bonde la Arnoni, na kuanzia mji ulio katikati ya bonde, pia uwanda wote wa juu kupita Medeba
17 Hesbon og alle dens Stæder, som ligger paa det jævne Land, Dibon og Bamoth-Baal og Beth-Baal-Meon
hadi Heshboni na miji yake yote kwenye uwanda wa juu, ikijumlishwa miji ya Diboni, Bamoth-Baali, Beth-Baal-Meoni,
18 og Jahza og Kedemoth og Mefaath
Yahasa, Kedemothi, Mefaathi,
19 og Kirjathaim og Sibma og Zereth-Sahar paa Dalens Bjerg
Kiriathaimu, Sibma, Sereth-Shahari juu ya kilima kilicho katika bonde,
20 og Beth-Peor og Asdoth-Pisga og Beth-Jesimoth
Beth-Peori, materemko ya Pisga na Beth-Yeshimothi:
21 og alle Stæderne paa det jævne Land og hele Sihons, den amoritiske Konges Rige, han, som regerede i Hesbon, hvilken Mose slog, tillige med Fyrsterne af Midian, nemlig Evi og Rekem og Zur og Hur og Reba, Sihons ypperste Mænd, som boede i Landet.
miji yote ya uwanda wa juu na eneo lote la utawala wa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala katika Heshboni. Mose alikuwa amemshinda Sihoni, pia watawala wakuu wa Wamidiani, ambao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba, waliokuwa wameungana na Sihoni, ambao waliishi katika nchi ile.
22 Og Bileam, Beors Søn, Spaamanden, slog Israels Børn ihjel med Sværd, tillige med de andre ihjelslagne.
Pamoja na wale waliouawa katika vita, Waisraeli walikuwa wamemuua kwa upanga Balaamu mwana wa Beori aliyekuwa mchawi.
23 Og Rubens Børns Landemærke vare Jordanen og Landemærket derhos; denne er Rubens Børns Arv efter deres Slægter, Stæderne og deres Landsbyer.
Mpaka wa Wareubeni ulikuwa ni ukingo wa Mto Yordani. Miji hii na vijiji vyake ndiyo iliyokuwa urithi wa Wareubeni ukoo kwa ukoo.
24 Og Mose havde givet Gads Stamme, Gads Børn, Arv efter deres Slægter.
Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
25 Og Jaeser og alle Stæderne i Gilead vare deres Landemærke og Halvdelen af Ammons Børns Land, indtil Aroer, som ligger lige over for Rabbah,
Nchi ya Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Amoni iliyoenea hadi Aroeri, karibu na Raba;
26 og fra Hesbon indtil Ramath-Mizpe og Bethonim og fra Mahanaim indtil Debirs Landemærke;
na kuanzia Heshboni mpaka Ramath-Mispa na Betonimu, na kutoka Mahanaimu hadi eneo la Debiri;
27 og i Dalen: Beth-Haram og Beth-Nimra og Sukoth og Zafon, som var bleven tilovers af Sihons, Hesbons Konges, Rige, Jordanen og Landemærket derhos, indtil Enden af Kinnereths Hav, paa hin Side Jordanen mod Østen.
na katika bonde, Beth-Haramu, Beth-Nimra, Sukothi na Safoni na sehemu iliyobaki ya eneo la utawala wa Sihoni mfalme wa Heshboni (upande wa mashariki mwa Mto Yordani, eneo inayoishia kwenye Bahari ya Kinerethi).
28 Denne er Gads Børns Arv efter deres Slægter, Stæderne og deres Landsbyer.
Miji hii na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Gadi ukoo kwa ukoo.
29 Og Mose havde givet den halve Manasse Stamme Arv, og den hørte den halve Manasse Børns Stamme til efter deres Slægter.
Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa hiyo nusu ya kabila la Manase, yaani kwa nusu ya jamaa ya uzao wa Manase, ukoo kwa ukoo:
30 Og deres Landemærke var fra Mahanaim, hele Basan, hele Ogs, Kongen af Basans Rige, og alle Jairs Byer, som ligge i Basan, tresindstyve Stæder.
Eneo lililoenea kuanzia Mahanaimu, na kujumlisha Bashani yote, ufalme wote wa Ogu mfalme wa Bashani, makazi yote ya Yairi huko Bashani, miji sitini,
31 Og Halvdelen af Gilead og Astaroth og Edrei, Ogs Riges Stæder i Basan, gav han Makirs, Manasse Søns, Børn, Halvdelen nemlig af Makirs Børn efter deres Slægter.
nusu ya Gileadi, na Ashtarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Hii ilikuwa kwa ajili ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, kwa ajili ya nusu ya wana wa Makiri, ukoo kwa ukoo.
32 Dette er det, som Mose uddelte til Arv paa Moabs slette Marker, paa hin Side Jordanen ved Jeriko mod Østen.
Huu ndio urithi alioupeana Mose wakati alipokuwa katika tambarare za Moabu, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
33 Men Levi Stamme havde Mose ikke givet Arv; Herren, Israels Gud, han er deres Arv, som han havde tilsagt dem.
Lakini kwa kabila la Walawi, Mose hakuwapa urithi; Bwana Mungu, Mungu wa Israeli ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.