< Job 36 >
1 Og Elihu blev ved og sagde:
Elihu akaendelea kusema:
2 Bi mig lidt, og jeg vil belære dig, thi her er endnu noget at tale for Gud.
“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
3 Jeg vil hente min Kundskab langt borte fra og skaffe den, som har skabt mig, Ret.
Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
4 Thi sandelig, mine Taler ere ikke Løgn; een, som er oprigtig i hvad han ved, er hos dig.
Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
5 Se, Gud er mægtig, og han vil ikke forkaste nogen, han er mægtig i Forstandens Styrke.
“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
6 Han lader ikke en ugudelig leve, men skaffer de elendige Ret.
Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
7 Han drager ikke sine Øjne bort fra de retfærdige, hos Konger paa Tronen, der sætter han dem evindelig, og de skulle ophøjes.
Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
8 Og om de blive bundne i Lænker, blive fangne med Elendigheds Snore,
Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
9 da forkynder han dem deres Gerninger og deres Overtrædelser, at de vare overmodige;
huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
10 da aabner han deres Øren for Formaningen og siger, at de skulle omvende sig fra Uretfærdighed.
Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
11 Dersom de da ville høre og tjene ham, da skulle de ende deres Dage i det gode og deres Aar i Liflighed;
Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
12 men dersom de ikke ville høre, da skulle de omkomme ved Sværdet op opgive Aanden i Uforstand.
Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
13 Og de vanhellige af Hjerte nære Vrede, de raabe ej til ham, naar han binder dem.
“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
14 Deres Sjæl dør hen i Ungdommen og deres Liv som Skørlevneres.
Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
15 Han frier en elendig ved hans Elendighed og aabner deres Øre ved Trængsel.
Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
16 Ogsaa dig leder han ud af Trængselens Strube til det vide Rum, hvor der ikke er snævert; og hvad, som sættes paa dit Bord, er fuldt af Fedme.
“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
17 Men har du fuldt op af den uretfærdiges Sag, skal Sag og Dom følges ad.
Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
18 Thi lad ej Vreden forlede dig til Spot og lad ej den store Løsesum forføre dig!
Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
19 Mon han skulde agte din Rigdom? nej, hverken det skønne Guld eller nogen Magts Styrke!
Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
20 Du skal ikke hige efter Natten, da Folk borttages fra deres Sted.
Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
21 Forsvar dig, at du ikke vender dit Ansigt til Uret; thi denne har du foretrukket fremfor det at lide.
Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
22 Se, Gud er ophøjet ved sin Kraft; hvo er en Lærer som han?
“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Hvo har foreskrevet ham hans Vej? og hvo tør sige: Du har gjort Uret?
Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
24 Kom i Hu, at du ophøjer hans Gerning, hvilken Folk have besunget;
Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
25 hvilken alle Mennesker have set, hvilken Mennesket skuer langtfra.
Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
26 Se, Gud er stor, og vi kunne ikke kende ham, og man kan ikke udgrunde Tallet paa hans Aar.
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27 Thi han drager Vandets Draaber til sig; gennem hans Dunstkreds beredes de til Regn,
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
28 hvilken Skyerne lade nedflyde, lade neddryppe over mange Mennesker.
mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
29 Mon ogsaa nogen forstaa hans Skyers Udspænding, hans Hyttes Bragen?
Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
30 Se, han udbreder sit Lys om sig og skjuler Havets Rødder.
Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
31 Thi derved dømmer han Folkene, giver dem Spise i Overflødighed.
Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
32 Over sine Hænder dækker han med Lyset, og han giver det Befaling imod den, det skal ramme.
Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
33 Om ham forkynder hans Torden, ja om ham Kvæget, naar han drager op.
Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.