< Hebræerne 2 >

1 Derfor bør vi des mere agte paa det, vi have hørt, for at vi ikke skulle rives bort.
Kwa sababu hiyo tunapaswa kuzingatia kwa makini zaidi yote tuliyosikia, ili tusije tukapotoshwa.
2 Thi naar det Ord, som taltes ved Engle, blev urokket, og hver Overtrædelse og Ulydighed fik velforskyldt Løn,
Ujumbe ule waliopewa wazee wetu na malaika ulionyeshwa kuwa kweli, hata mtu yeyote ambaye hakuufuata au hakuutii aliadhibiwa kama alivyostahili.
3 hvorledes skulle da vi undfly, naar vi ikke bryde os om saa stor en Frelse, som jo efter først at være bleven forkyndt ved Herren er bleven stadfæstet for os af dem, som havde hørt ham,
Basi, sisi tutaokokaje kama hatuujali wokovu mkuu kama huu? Kwanza Bwana mwenyewe aliutangaza wokovu huu, na wale waliomsikia walituthibitishia kwamba ni kweli.
4 idet Gud vidnede med baade ved Tegn og Undere og mange Haande kraftige Gerninger og ved Meddelelse af den Helligaand efter sin Villie.
Mungu pia aliongeza hapo ushahidi wake kwa kufanya kila namna ya miujiza na maajabu, na kwa kuwagawia watu vipaji vya Roho Mtakatifu kadiri ya mapenzi yake.
5 Thi det var ikke Engle, han underlagde den kommende Verden, om hvilken vi tale.
Mungu hakuwaweka malaika wautawale ulimwengu ujao, yaani ulimwengu ule tunaoongea habari zake.
6 Men en har vidnet et Sted og sagt: „Hvad er et Menneske, at du kommer ham i Hu? eller en Menneskesøn, at du ser til ham?
Tena yasemwa mahali fulani katika Maandiko: “Mtu ni nini ee Mungu, hata umfikirie; mwanaadamu ni nini hata umjali?
7 Du gjorde ham en kort Tid ringere end Engle; med Herlighed og Ære kronede du ham;
Ulimfanya kwa kitambo kidogo kuwa chini zaidi kuliko malaika; ukamvika taji ya utukufu na heshima,
8 alle Ting lagde du under hans Fødder.” — Idet han nemlig underlagde ham alle Ting, undtog han intet fra at være ham underlagt. Nu se vi imidlertid endnu ikke alle Ting underlagte ham;
ukaweka kila kitu chini ya miguu yake, avitawale.” Yasemwa kwamba Mungu alimweka mtu kuwa mtawala wa vitu vyote yaani bila kuacha hata kimoja. Hata hivyo, hatuoni bado mtu akivitawala vitu vyote sasa.
9 men ham, som en kort Tid var bleven gjort ringere end Engle, Jesus, se vi paa Grund af Dødens Lidelse kronet med Herlighed og Ære, for at han ved Guds Naade maa have smagt Døden for alle.
Lakini twamwona Yesu ambaye alifanywa kwa kitambo kidogo kuwa chini zaidi kuliko malaika, ili kwa neema ya Mungu afe kwa ajili ya watu wote. Sasa tunamwona ametawazwa kwa utukufu na heshima kwa sababu ya kifo alichoteseka.
10 Thi det sømmede sig ham, for hvis Skyld alle Ting ere, og ved hvem alle Ting ere, naar han førte mange Sønner til Herlighed, da at fuldkomme deres Frelses Ophavsmand igennem Lidelser.
Ilikuwa haki tupu kwamba Mungu, ambaye huumba na kutegemeza vitu vyote, alimfanya Yesu kuwa mkamilifu kabisa kwa njia ya mateso, ili awalete watoto wengi waushiriki utukufu wake. Maana Yesu ndiye anayewaongoza kwenye wokovu.
11 Thi baade den, som helliger, og de, som helliges, ere alle af een; hvorfor han ikke skammer sig ved at kalde dem Brødre,
Yeye anawatakasa watu dhambi zao, naye pamoja na wale waliotakaswa, wote wanaye Baba mmoja. Ndiyo maana Yesu haoni aibu kuwaita hao ndugu zake;
12 naar han siger: „Jeg vil forkynde dit Navn for mine Brødre, midt i en Menighed vil jeg lovsynge dig.”
kama asemavyo: “Ee Mungu, nitawatangazia ndugu zangu matendo yako. Nitakusifu katika kusanyiko lao.”
13 Og fremdeles: „Jeg vil forlade mig paa ham.” Og fremdeles: „Se, her er jeg og de Børn, som Gud har givet mig.”
Tena asema: “Nitamwekea Mungu tumaini langu.” Na tena: “Mimi niko hapa pamoja na watoto alionipa Mungu.”
14 Efterdi da Børnene ere delagtige i Blod og Kød, blev ogsaa han i lige Maade delagtig deri, for at han ved Døden skulde gøre den magtesløs, som har Dødens Vælde, det er Djævelen,
Basi, kwa vile watoto hao, kama awaitavyo, ni watu wenye mwili na damu, Yesu mwenyewe akawa kama wao na kushiriki ubinadamu wao. Alifanya hivyo ili kwa njia ya kifo chake amwangamize Ibilisi, ambaye ana mamlaka juu ya kifo,
15 og befri alle dem, som paa Grund af Dødsfrygt vare under Trældom al deres Livs Tid.
na hivyo awaokoe wale waliokuwa watumwa maisha yao yote kwa sababu ya hofu yao ya kifo.
16 Thi det er jo dog ikke Engle, han tager sig af, men Abrahams Sæd tager han sig af.
Maana ni wazi kwamba yeye hakuja kwa ajili ya kuwasaidia malaika, bali kama yasemavyo Maandiko; “Anawasaidia wazawa wa Abrahamu.”
17 Derfor maatte han blive sine Brødre lig i alle Ting, for”at han kunde blive en barmhjertig og trofast Ypperstepræst over for Gud til at sone Folkets Synder.
Ndiyo maana ilimbidi awe kama ndugu zake kwa kila namna, ili awe Kuhani Mkuu wao aliye mwaminifu na mwenye huruma katika kumtumikia Mungu, ili dhambi za watu ziondolewe.
18 Thi idet han har lidt, kan han som den, der selv er fristet, komme dem til Hjælp, som fristes.
Na, anaweza sasa kuwasaidia wale wanaojaribiwa na kuteswa.

< Hebræerne 2 >