< Ezekiel 27 >
1 Og Herrens Ord kom til mig saaledes:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Og du Menneskesøn! opløft et Klagemaal over Tyrus,
“Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Tiro.
3 og sig til Tyrus, som bor ved Havets Havne, og som handler med Folkene paa mange Øer: Saa siger den Herre, Herre: O Tyrus! du sagde: Jeg er fuldkommen i Skønhed.
Umwambie Tiro, ulioko kwenye lango la bahari, ufanyao biashara na mataifa mengi ya pwani, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ee Tiro, wewe umesema, “Mimi ni mkamilifu katika uzuri.”
4 Dine Landemærker ere midt i Havet, dine Bygningsmænd have gjort din Skønhed fuldendt.
Mipaka yako ilikuwa katika moyo wa bahari, wajenzi wako walikamilisha uzuri wako.
5 De byggede dig hele Opklædningen af Fyrretræ fra Senir; de hentede Geder fra Libanon til at gøre en Mast paa dig.
Walizifanya mbao zako zote kwa misunobari itokayo Seniri; walichukua mierezi kutoka Lebanoni kukutengenezea mlingoti.
6 De gjorde dine Aarer af Eg fra Basan; dit Dæk gjorde de af Elfenben, indlagt i Buksbom fra Kithims Øer.
Walichukua mialoni toka Bashani wakakutengenezea makasia yako; kwa miti ya msanduku kutoka pwani ya Kitimu wakatengeneza sitaha yako na kuipamba kwa pembe za ndovu.
7 Dit Sejl var af hvidt Linned med stukket Arbejde fra Ægypten, for at det skulde være dig til Mærke; af blaat Purpur og rødt Purpur fra Elisas Øer var dit Solsejl.
Kitani safi kilichotariziwa kutoka Misri kilikuwa tanga lako, nacho kilikuwa bendera yako; chandarua chako kilikuwa cha rangi ya buluu na ya zambarau kutoka visiwa vya Elisha.
8 Indbyggerne i Zidon og Arvad vare dine Rorkarle; dine vise, o Tyrus! som vare i dig, de vare dine Styrmænd.
Watu kutoka Sidoni na Arvadi walikuwa wapiga makasia yako; watu wako wenye ustadi, ee Tiro, walikuwa ndio mabaharia wako.
9 Gebals Ældste og dens vise vare hos dig for at stoppe din Læk; alle Skibe i Havet og deres Skibsfolk vare hos dig for at drive Handel med dig.
Wazee wa Gebali pamoja na mafundi stadi walikuwa mafundi wako melini. Meli zote za baharini na mabaharia wao walikuja kwako ili kubadilishana bidhaa zako.
10 Folk fra Persien og Lydien og fra Put vare i din Hær som dine Krigsfolk, de ophængte Skjold og Hjelm i dig, de gave dig Glans.
“‘Watu wa Uajemi, Ludi na Putu walikuwa askari katika jeshi lako. Walitundika ngao zao na chapeo zao kwenye kuta zako, wakileta fahari yako.
11 Arvads Børn og din Hær vare paa dine Mure trindt omkring, og tapre Mænd vare paa dine Taarne; de hængte deres Skjolde paa dine Mure trindt omkring, de gjorde din Skønhed fuldendt.
Watu wa Arvadi na wa Heleki walikuwa juu ya kuta zako pande zote; watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walitundika ngao zao kuzizunguka kuta zako; wakaukamilisha uzuri wako.
12 Tharsis handlede med dig, fordi du havde Mangfoldighed af alle Haande Gods; med Sølv, Jern, Tin og, Bly betalte de dine Varer.
“‘Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mkubwa wa bidhaa, walibadilisha fedha, chuma, bati na risasi kwa mali zako.
13 Javan, Tubal og Mesek, de vare dine Kræmmere; Menneskesjæle og Kobberkar gave de dig i Tusk.
“‘Uyunani, Tubali na Mesheki, walifanya biashara nawe, walibadilisha watumwa na vyombo vya shaba kwa bidhaa zako.
14 De af Thogarmas Hus betalte dine Varer med Køreheste og Rideheste og Mulæsler.
“‘Watu wa Beth-Togarma walibadilisha farasi wa mizigo, farasi wa vita na nyumbu kwa mali zako.
15 Dedans Børn vare dine Kræmmere; mange Kyster stode i Handelsforhold med dig; de gave dig Elfenben og Ebentræ til Betaling.
“‘Watu wa Dedani walifanya biashara nawe, watu wengi wa nchi za pwani walikuwa wachuuzi wako, walikulipa kwa pembe za ndovu na mpingo.
16 Syrien handlede med dig, fordi du havde en Mangfoldighed af Arbejder; med Karbunkel, Purpur og stukket Arbejde jog hvidt Linned og Koraller og Rubiner betalte de dine Varer.
“‘Watu wa Aramu walifanya biashara nawe kwa ajili ya wingi wa kazi za mikono yako, wakibadilishana kwa almasi, vitambaa vya rangi ya zambarau, vitambaa vilivyotariziwa, kitani safi, matumbawe na akiki nyekundu.
17 Judas og Israels Lande, de vare dine Kræmmere; Hvede fra Minnit og søde Sager og Honning og Olie og Balsam gave de dig i Tusk.
“‘Yuda na Israeli walifanya biashara nawe, walibadilishana kwa ngano kutoka Minithi, mtama, asali, mafuta na zeri ya kuponyeshea.
18 Damaskus handlede med dig, fordi du havde en Mangfoldighed af Arbejder, for Mangfoldigheden af alle Haande Gods, med Vin af Helbon og hvid Uld.
“‘Dameski, kwa sababu ya wingi wa kazi za mikono yako na ukuu wa utajiri wa mali, walifanya biashara nawe wakibadilishana mvinyo kutoka Helboni na sufu kutoka Zahari.
19 Vedan og Javan gave Sager fra Uzzal for dine Varer; skinnende Jern, Kasia og Kalmus gaves dig i Tusk.
“‘Wadani na Wayunani kutoka Uzali, walikuletea mali za biashara, nao wakabadilishana nawe chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai.
20 Dedan handlede med dig med Dækkener til at ride paa.
“‘Dedani alifanya biashara nawe kwa matandiko ya farasi.
21 Arabien og alle Kedars Fyrster, de stode i Handelsforhold med dig; med Lam og Vædre og Bukke, med dem handlede de med dig.
“‘Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wanunuzi wako waliobadilishana bidhaa zako na wana-kondoo, kondoo dume na mbuzi.
22 Kræmmere fra Seba og Raema, de vare dine Kræmmere; med det ypperste af alle Haande Urter og med alje Haande kostbare Stene og Guld betalte de dine Varer.
“‘Wafanyabiashara wa Sheba na wa Raama walifanya biashara nawe, wakabadilishana bidhaa zako na aina zote za vikolezi, vito vya thamani na dhahabu.
23 Haran og Karma og Eden, Kræmmere fra Seba, Assur og Kilmad handlede med dig.
“‘Harani, Kane na Edeni na wafanyabiashara wa Sheba, Ashuru na Kilmadi walifanya biashara nawe.
24 De vare dine Kræmmere med Kostbarheder, bestaaende i Kapper af blaat Purpur og stukket Arbejde, og med værdifuldt Garn, i tvundne og faste Snore, paa dit Marked.
Kwenye soko lako, walifanya biashara nawe kwa mavazi mazuri, vitambaa vya buluu, nguo za kutariziwa na mazulia ya rangi mbalimbali yenye kamba zilizosokotwa na kuwekwa mafundo imara.
25 Tharsis's Skibe droge omkring for dig, de dreve din Handel, og du blev fyldt og saare rig midt i Havet.
“‘Merikebu za Tarshishi ndizo zinazokusafirishia bidhaa zako. Umejazwa shehena kubwa katika moyo wa bahari.
26 Dine Rorkarle førte dig paa de store Vande, Østenvejret sønderslog dig midt i Havet.
Wapiga makasia wako wanakupeleka mpaka kwenye maji makavu. Lakini upepo wa mashariki umekuvunja vipande vipande katika moyo wa bahari.
27 Dit Gods og dine Varer, hvad du handlede med, dine Skibsfolk og dine Styrmænd, de, som stoppede din Læk, og de, som dreve din Handel, og alle dine Krigsmænd, som vare i dig, med hele din Skare, som var i din Midte, faldt midt i Havet paa dit Falds Dag.
Utajiri wako, bidhaa zako na mali zako, mabaharia wako, manahodha wako, mafundi wako wa meli, wafanyabiashara wako na askari wako wote, na kila mmoja aliyeko melini atazama kwenye moyo wa bahari siku ile ya kuvunjika kwa meli yako.
28 Ved Lyden af dine Styrmænds Skrig bæve Strandmarkerne.
Nchi za pwani zitatetemeka wakati mabaharia wako watakapopiga kelele.
29 Og alle de, som føre Aarer, stige ud af deres Skibe; Skibsfolk, alle Styrmænd paa Havet, de træde i Land.
Wote wapigao makasia wataacha meli zao, mabaharia wote na wanamaji wote watasimama pwani.
30 Og de lade deres Røst høre over dig og raabe bitterlig; og de kaste Støv paa deres Hoved, de vælte sig i Asken.
Watapaza sauti zao na kulia sana kwa ajili yako; watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao na kujivingirisha kwenye majivu.
31 Og de rage sig helt skaldede for din Skyld og iføre sig Sæk; og de græde over dig i Sjælens Bitterhed med en bitter Sorg.
Watanyoa nywele zao kwa ajili yako, nao watavaa nguo za magunia. Watakulilia kwa uchungu wa moyo na kwa maombolezo makuu.
32 Og de opløfte et Klagemaal over dig i deres Jamren og beklage dig: „Hvo er som Tyrus, som den, der er bleven tavs midt paa Havet?”
Watakapokuwa wanalia na kuomboleza juu yako, watafanya maombolezo kukuhusu wakisema: “Ni nani aliyepata kuangamizwa kama Tiro, katika moyo wa bahari?”
33 Der dine Varer kom frem af Havene, mættede du mange Folk; med Mangfoldigheden af dit Gods, og hvad du handlede med, gjorde du Konger rige paa Jorden.
Wakati bidhaa zako zilipotoka baharini, ulitosheleza mataifa mengi; kwa wingi wa utajiri wako na bidhaa zako ulitajirisha wafalme wa dunia.
34 Nu, da du knust er forsvunden af Havene i de dybe Vandeler din Handel og hele din Skare midt i dig falden.
Sasa umevunjavunjwa na bahari, katika vilindi vya maji, bidhaa zako na kundi lako lote vimezama pamoja nawe.
35 Alle Øernes Indbyggere gyse over dig, og deres Konger forfærdes saare, de se bedrøvelige ud i Ansigtet.
Wote waishio katika nchi za pwani wanakustaajabia; wafalme wao wanatetemeka kwa hofu kuu, nazo nyuso zao zimekunjamana kwa woga.
36 Købmændene iblandt Folkene pibe ad dig; du er bleven til Gru og er til evig Tid ikke mere.
Wafanyabiashara miongoni mwa mataifa wanakucheka; umefikia mwisho wa kutisha nawe hutakuwepo tena.’”