< Ezekiel 21 >

1 Og Herrens Ord kom til mig saaledes:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Du Menneskesøn! vend dit Ansigt imod Jerusalem, og lad Ordene falde som Draaber imod Helligdommene, og spaa imod Israels Land;
“Mwanadamu, uelekeze uso wako juu ya Yerusalemu na uhubiri dhidi ya mahali patakatifu. Tabiri dhidi ya nchi ya Israeli
3 og sig til Israels Land: Saa siger Herren: Se jeg kommer imod dig og uddrager mit Sværd af sin Skede, og jeg vil udrydde af dig den retfærdige med den ugudelige.
uiambie: ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Mimi niko kinyume nawe. Nitautoa upanga wangu kwenye ala yake na kumkatilia mbali mwenye haki na mwovu.
4 Efterdi jeg vil udrydde af dig den retfærdige med den ugudelige, derfor skal mit Sværd udfare af sin Skede: Imod alt Kød fra Sønden til Norden.
Kwa sababu nitamkatilia mbali mwenye haki na mwovu, upanga wangu utakuwa wazi dhidi ya kila mmoja kuanzia kusini mpaka kaskazini.
5 Og alt Kød skal fornemme, at jeg Herren, jeg har uddraget mit Sværd af sin Skede: Det skal ikke mere vende tilbage.
Ndipo watu wote watajua ya kuwa Mimi Bwana nimeutoa upanga wangu kwenye ala yake, nao hautarudi humo tena.’
6 Og du Menneskesøn, suk! saa det bryder i dine Lænder, og saa det er dig bittert, skal du sukke for deres Øjne.
“Kwa hiyo lia kwa uchungu, mwanadamu! Lia kwa uchungu mbele yao kwa moyo uliopondeka na kwa huzuni nyingi.
7 Og det skal ske, naar de sige til dig: Hvorfor sukker du? da skal du sige: For et Rygte; thi det kommer, og hvert Hjerte skal smelte, og alle Hænder skulle synke, og hver Aand skal blive sløv, og alle Knæ skulle ryste som Vand; se, det kommer, og det sker, siger den Herre, Herre.
Nao watakapokuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa uchungu?’ Utasema hivi, ‘Kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila moyo utayeyuka na kila mkono utalegea, kila roho itazimia na kila goti litalegea kama maji.’ Habari hizo zinakuja! Hakika zitatokea, asema Bwana Mwenyezi.”
8 Og Herrens Ord kom til mig saaledes:
Neno la Bwana likanijia, kusema:
9 Du Menneskesøn! spaa og sig: Saa siger Herren, sig: Et Sværd, et Sværd, det er gjort hvast og blankt tillige!
“Mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Upanga, upanga, ulionolewa na kusuguliwa:
10 For at udføre en Slagtning er det gjort hvast, og for at lyne er det gjort blankt; — eller skulle vi vel glæde os til, at min Søns Scepter vil lade haant om alt Træ?
umenolewa kwa ajili ya mauaji, umesuguliwa ili ungʼae kama umeme wa radi! “‘Je, tuifurahie fimbo ya utawala ya mwanangu Yuda? Upanga unaidharau kila fimbo ya namna hiyo.
11 Man gav det hen at gøres blankt for at tage det i Haand; Sværdet er gjort hvast, og det er gjort blankt for at give det i Morderens Haand.
“‘Upanga umewekwa tayari ili kusuguliwa, ili upate kushikwa mkononi, umenolewa na kusuguliwa, umewekwa tayari kwa mkono wa muuaji.
12 Raab og hyl, du Menneskesøn! thi det skal komme over mit Folk, ja, over alle Fyrster i Israel; de ere overgivne til Sværdet tillige med mit Folk; derfor slaa paa Hoften!
Piga kelele na uomboleze, ee mwanadamu, kwa kuwa upanga u dhidi ya watu wangu; u dhidi ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa wauawe kwa upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo pigapiga kifua chako.
13 Thi Prøven er sket! og hvad, dersom endog det haanende Scepter ikke holder Stand? siger den Herre, Herre.
“‘Kwa maana upanga huu umejaribiwa na kuhakikishwa, itakuwaje basi fimbo ya ufalme ya Yuda inayoudharau kama haitakuwepo tena, bali itakuwa imeondolewa kabisa? asema Bwana Mwenyezi.’
14 Og du Menneskesøn! spaa og slaa Haand i Haand; og Sværdet skal blive dobbelt, ja tredobbelt; det er et Sværd, for hvilket der skal ligge ihjelslagne; det er et Sværd, for hvilket den store skal ligge ihjelslagen; det er imod dem fra alle Sider.
“Hivyo basi, mwanadamu, tabiri na ukapige makofi. Upanga wako na upige mara mbili, naam, hata mara tatu. Ni upanga wa kuchinja, upanga wa mauaji makuu, ukiwashambulia kutoka kila upande.
15 Paa det at Hjertet maa smelte, og der maa blive mange Anstød, har jeg sat det blinkende Sværd imod alle deres Porte; ak! det er gjort til at lyne, det er draget til at slagte.
Ili mioyo ipate kuyeyuka na wanaouawa wawe wengi, nimeweka upanga wa kuchinja kwenye malango yao yote. Lo! Umetengenezwa umetemete kama umeme wa radi, umeshikwa kwa ajili ya kuua.
16 Tag dig sammen til højre! vend dig til venstre! hvorhen din Æg er beskikket.
Ee upanga, kata upande wa kuume, kisha upande wa kushoto, mahali popote makali yako yatakapoelekezwa.
17 Ogsaa jeg vil slaa min Haand i min Haand og stille min Harme; jeg Herren, jeg har talt det.
Mimi nami nitapiga makofi, nayo ghadhabu yangu itapungua. Mimi Bwana nimesema.”
18 Og Herrens Ord kom til mig saalunde:
Neno la Bwana likanijia kusema:
19 Og du Menneskesøn! afsæt dig to Veje, ad hvilke Kongen af Babels Sværd skal komme, de skulle begge udgaa fra eet Land, og tegn en Haand, tegn den, hvor Vejen til hver Stad begynder.
“Mwanadamu, weka alama njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babeli utapitia, njia hizo zikianzia katika nchi hiyo hiyo. Weka kibao pale ambapo njia zinagawanyika kuelekea mjini.
20 Du skal afsætte en Vej, ad hvilken Sværdet kan komme til Ammons Børns Rabba og til Juda ind i den faste Stad Jerusalem.
Weka alama njia moja kwa ajili ya upanga upate kuja dhidi ya Raba ya Waamoni na nyingine upate kuja dhidi ya Yuda na Yerusalemu iliyozungushiwa ngome.
21 Thi Kongen af Babel staar paa Vejskellet, hvor de to Veje begynde, for at lade sig spaa; han kaster med Pilene, han spørger Husguderne, han ser paa Leveren.
Kwa kuwa mfalme wa Babeli sasa amesimama katika njia panda, katika makutano ya njia mbili, akipiga ramli: anapiga kura kwa kutumia mishale, anataka shauri kwa sanamu zake, anachunguza maini ya wanyama.
22 I hans højre Haand er Spaadommen „Jerusalem” falden, at han skal opstille Murbrækkere, at han skal oplade Munden med Mord og opløfte Røsten med Krigsskrig, opstille Murbrækkere imod Portene, opkaste en Belejringsvold, bygge Vagttaarne.
Upande wake wa kuume inakuja kura ya Yerusalemu, ambapo ataweka vyombo vya kuvunjia boma, ili kuamrisha mauaji, kupiga ukelele wa vita, kuweka vyombo vya kuvunjia boma kwenye malango, kuweka jeshi kuzunguka na kufanya uzingiraji.
23 Men det skal vorde dem som en Forfængelighedsspaadom i deres Øjne, de have Ed paa Ed; men han skal bringe Misgerningen i Erindring, og de skulle gribes.
Itakuwa kama kupiga ramli kwa uongo kwa wale watu ambao wameapa kumtii yeye. Lakini mfalme wa Babeli atawakumbusha juu ya uovu wao na kuwachukua mateka.
24 Derfor, saa siger den Herre, Herre: Fordi I bringe eders Misgerning i Erindring, idet eders Overtrædelser blottes, saa at eders Synder ses i alle eders Gerninger, ja, fordi I bringes i Erindring, skulle I gribes med Haanden.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu enyi watu mmekumbusha uovu wenu kwa kuasi waziwazi, mkidhihirisha dhambi zenu katika yale yote mfanyayo, kwa kuwa mmefanya jambo hili, mtachukuliwa mateka.
25 Og du gennemborede, du ugudelige, du Israels Fyrste, hvis Dag kommer til den Tid, naar Misgerningen medfører Enden!
“‘Ee mtawala kafiri na mwovu wa Israeli, ambaye siku yako imewadia, ambaye wakati wako wa adhabu umefikia kilele chake,
26 Saa siger den Herre, Herre: Ypperstepræstehuen skal borttages, og Kongekronen bortføres; hvad der er, skal ikke være mere, det nedtrykte skal ophøjes og det høje nedtrykkes.
hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Vua kilemba, ondoa taji. Kwa kuwa mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa. Aliye mnyonge atakwezwa na aliyekwezwa atashushwa.
27 Omvæltning, Omvæltning, Omvæltning vil jeg gøre det til; heller ikke denne skal vare ved — indtil han kommer, hvem Retten hører til, og jeg giver ham den.
Mahame! Mahame! Nitaufanya mji kuwa mahame! Hautajengwa upya mpaka aje yule ambaye ndiye mwenye haki nao; yeye ndiye nitakayempa.’
28 Og du Menneskesøn! spaa og sig: Saa siger den Herre, Herre om Ammons Børn og om deres Haan, ja, sig: Et Sværd, et Sværd er draget til Slagtning, det er gjort fuldkomment blankt til at lyne,
“Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu Waamoni na matukano yao. “‘Upanga, upanga, umefutwa kwa ajili ya kuua, umesuguliwa ili kuangamiza na unametameta kama umeme wa radi!
29 idet man bringer dig forfængelige Syner, idet man spaar dig Løgn for at lægge dig ved de ihjelslagne ugudeliges Halse, hvis Dag kom til den Tid, da Misgerningen medførte Enden.
Wakati wakitoa maono ya uongo kwa ajili yako, wanapobashiri uongo kwa ajili yako, wanakuweka wewe kwenye shingo za watu wapotovu, wale walio waovu, wale ambao siku yao imewadia, wakati wa adhabu yao ya mwisho.
30 Stik Sværd i Skeden! paa det Sted, hvor du er skabt, i det Land, hvor du er født, vil jeg dømme dig.
Urudishe upanga kwenye ala yake! Katika mahali ulipoumbiwa, katika nchi ya baba zako, huko nitakuhukumu.
31 Og jeg vil udøse min Vrede over dig, min Fortørnelses Ild vil jeg oppuste imod dig, og jeg vil give dig i grumme Mænds Hænder, som ere Mestre til at ødelægge.
Nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako; nitakutia mikononi mwa watu wakatili, watu stadi katika kuangamiza.
32 Du skal være Ilden til Næring, dit Blod skal blive midt i Landet, du skal ikke ihukommes; thi jeg Herren, jeg har talt det.
Mtakuwa kuni za kuwashia moto, damu yenu itamwagwa katika nchi yenu, wala hamtakumbukwa tena; kwa maana Mimi Bwana nimesema.’”

< Ezekiel 21 >