< 5 Mosebog 34 >
1 Og Mose gik op fra Moabs slette Marker paa Nebo Bjerg, paa Pisgas Top, som er lige over for Jeriko; og Herren lod ham se hele Landet: Gilead indtil Dan
Musa aliondoka kutoka nyanda za Moabu mpaka mlima wa Nebo, hadi kilele cha Pisga, kilicho mkabala na Yericho. Huko Yahwe alimwonyesha nchi yote ya Gileadi kutoka umbali wa Dani,
2 og hele Nafthali og Efraims og Manasse Land og hele Judas Land indtil det yderste Hav
na Naftali yote, na nchi ya Efraimu na Manase, na nchi yote ya Yuda, mpaka bahari ya magharibi,
3 og Sydlandet og Sletten, Dalen ved Jeriko, Palmestaden, indtil Zoar.
na Negevi, na uwanda wa bonde la Yericho, mji wa mitende, mpaka umbali wa Soari.
4 Og Herren sagde til ham: Dette er det Land, som jeg har tilsvoret Abraham, Isak og Jakob og sagt: Din Sæd vil jeg give det; jeg har ladet dig se det med dine Øjne, men du skal ikke drage derover.
Yahwe alimwambia, “Hii ni nchi niliyoapa kwa Abrahamu, kwa Isaka, na kwa Yakobo, na kusema, “Nitawapatia uzao wako.” Nimekuruhusu uitazame kwa macho yako, lakini hautakwenda kule.”
5 Og Mose, Herrens Tjener, døde der i Moabs Land, efter Herrens Mund.
Basi Musa mtumishi wa Yahwe, alikufa pale katika nchi ya Moabu, kama neno la Yahwe lilivyoahidi.
6 Og han begrov ham i Dalen i Moabiternes Land, tværs over for Beth-Peor; og ingen ved hans Grav indtil denne Dag.
Yahwe alimzika katika bonde katika nchi ya Moabu mkabala na Beth-peori, lakini hakuna ajuaye kaburi lake lilipo hadi leo hii.
7 Og Mose var hundrede og tyve Aar gammel, der han døde; hans Øje var ikke sløvet, og hans Kraft var ikke veget fra ham.
Musa alikuwa na umri wa miaka mia moja na ishirini alipokufa; macho yake hayakufifia, wala nguvu asili zake hazikupungua.
8 Og Israels Børn begræd Mose paa Moabiternes slette Marker tredive Dage; og Graadens Dage endtes, Sorgen over Mose.
Watu wa Israeli walimuomboleza Musa katika nyanda za Moabu kwa siku thelathini, hapo ndipo siku za maombolezo ya Musa zilipotimia.
9 Og Josva, Nuns Søn, blev fyldt med Visdomsaand, thi Mose havde lagt sine Hænder paa ham; og Israels Børn hørte ham og gjorde, som Herren havde befalet Mose.
Yoshua mwana wa Nuni alikuwa amejawa na roho ya hekima, kwa maana Musa alimwekea mkono juu yake. Watu wa Israeli walimsikiliza na kufanya yale ambayo Yahwe alimuamuru Musa.
10 Men der opstod ikke en Profet ydermere i Israel som Mose, hvem Herren kendte Ansigt til Ansigt,
Tangu hapo hakujatokea nabii katika Israeli kama Musa, ambaye Yahwe alimjua uso kwa uso.
11 naar man ser hen til alle de Tegn og de underlige Ting, som Herren sendte ham til at gøre i Ægyptens Land, paa Farao og paa alle hans Tjenere og paa alt hans Land,
Hakujawahi kuwa na nabii yeyote kama yeye kwa ishara na miujiza ambayo Yahwe alimtuma kufanya katika nchi ya Misri, kwa Farao, na kwa watumishi wake, na kwa nchi yake yote.
12 og til den vældige Haand og til alle de forfærdelige og store Gerninger, som Mose gjorde for al Israels Øjne.
Hakujawahi kuwa na nabii yeyote kama yeye kwa mambo yote makubwa, ya kutisha ambayo Musa aliyafanya machoni pa Israeli yote.