< Kolossensern 3 >

1 Naar I altsaa ere blevne oprejste med Kristus, da søger det, som er oventil, hvor Kristus sidder ved Guds højre Haand.
Ikiwa tena Mungu amewafufua pamoja na Kristo, yatafuteni mambo ya juu ambako Kristo anakaa mkono wa kuume wa Mungu.
2 Tragter efter det, som er oventil, ikke efter det, som er paa Jorden.
Fikirini kuhusu mambo ya juu, sio kuhusu mambo ya duniani.
3 Thi I ere døde, og eders Liv er skjult med Kristus i Gud.
Kwa kuwa mmekufa, na maisha yenu yamefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
4 Naar Kristus, vort Liv, aabenbares, da skulle ogsaa I aabenbares med ham i Herlighed.
Wakati Kristo atakapoonekana, ambaye ni maisha yenu, ndipo nanyi pia mtaonekana naye katika utukufu.
5 Saa døder da de jordiske Lemmer, Utugt, Urenhed, Brynde, ondt Begær og Havesygen, som jo er Afgudsdyrkelse;
Kwa hiyo yafisheni mambo yaliyo katika nchi yaani, zinaa, uchafu, shauku mbaya, nia mbaya, na tamaa, ambayo ni ibada ya sanamu.
6 for disse Tings Skyld kommer Guds Vrede.
Ni kwa ajili ya mambo haya ghadhabu ya Mungu inakuja juu ya wana wasio tii.
7 I dem vandrede ogsaa I fordum, da I levede deri.
Ni kwa ajili ya mambo haya ninyi pia mlitembea kwayo mlipoishi kati yao.
8 Men nu skulle ogsaa I aflægge det alt sammen, Vrede, Hidsighed, Ondskab, Forhaanelse, slem Snak af eders Mund.
Lakini sasa ni lazima myaondoe mambo haya yote. Yaani, ghadhabu, hasira, nia mbaya, matusi, na maneno machafu yatokayo vinywani mwenu.
9 Lyver ikke for hverandre, da I have afført eder det gamle Menneske med dets Gerninger
Msidanganyane ninyi kwa ninyi, kwa kuwa mmeuvua utu wenu wa kale na matendo yake.
10 og iført eder det nye, som fornyes til Erkendelse efter hans Billede, der skabte det;
Mmevaa utu mpya, ambao unafanywa upya katika maarifa kutokana mfano wa yule aliye muumba.
11 hvor der ikke er Græker og Jøde, Omskærelse og Forhud, Barbar, Skyther, Træl, fri, men Kristus er alt og i alle.
Katika maarifa haya, hakuna Myunani na Myahudi, kutahiriwa na kutokutahiriwa, msomi, asiye msomi, mtumwa, asiye mtumwa, lakini badala yake Kristo ni mambo yote katika yote.
12 Saa ifører eder da som Guds udvalgte, hellige og elskede inderlig Barmhjertighed, Godhed, Ydmyghed, Sagtmodighed, Langmodighed,
Kama wateule wa Mungu, watakatifu na wapendwao, jivikeni utu wema, ukarimu, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
13 saa I bære over med hverandre og tilgive hverandre, dersom nogen har Klagemaal imod nogen; ligesom Kristus tilgav eder, saaledes ogsaa I!
Chukulianeni ninyi kwa ninyi. Hurumianeni kila mtu na mwenzake. Kama mtu analalamiko dhidi ya mwingine, amsamehe kwa jinsi ilele ambayo Bwana alivyo wasamehe ninyi.
14 Men over alt dette skulle I iføre eder Kærligheden, hvilket er Fuldkommenhedens Baand.
Zaidi ya mambo haya yote, muwe na upendo, ambao ndio kigezo cha ukamilifu.
15 Og Kristi Fred raade i eders Hjerter, til hvilken I ogsaa bleve kaldede i eet Legeme; og vorder taknemmelige!
Amani ya Kristo na iwaongoze mioyoni mwenu. Ilikuwa ni kwa ajili ya amani hii kwamba mliitiwa katika mwili mmoja. Iweni na shukrani.
16 Lad Kristi Ord bo rigeligt iblandt eder, saa I med al Visdom lære og paaminde hverandre med Psalmer, Lovsange og aandelige Viser, idet I synge med Ynde i eders Hjerter for Gud.
Na Neno la Kristo likae ndani yenu kwa utajiri. Kwa hekima yote, fundishaneni na kushauriana ninyi kwa ninyi kwa Zaburi, nyimbo, na nyimbo za rohoni. Imbeni kwa shukrani mioyo yenu kwa Mungu.
17 Og alt, hvad I gøre i Ord eller i Handling, det gører alt i den Herres Jesu Navn, takkende Gud Fader ved ham.
Na chochote mfanyacho, katika maneno au katika matendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu. Mpeni shukrani Mungu baba kupitia Yeye.
18 I Hustruer! underordner eder under eders Mænd, som det sømmer sig i Herren.
Wake, wanyenyekeeni waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana.
19 I Mænd! elsker eders Hustruer, og værer ikke bitre imod dem!
Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali dhidi yao.
20 I Børn! adlyder i alle Ting eders Forældre, thi dette er velbehageligt i Herren.
Watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, maana ndivyo impendezavyo Bwana.
21 I Fædre! opirrer ikke eders Børn, for at de ikke skulle tabe Modet.
Akina baba msiwachokoze watoto wenu, ili kwamba wasije wakakata tamaa.
22 I Trælle! adlyder i alle Ting eders Herrer efter Kødet, ikke med Øjentjeneste som de, der ville tækkes Mennesker, men i Hjertets Enfold, frygtende Herren.
Watumwa, watiini mabwana zenu katika mwili kwa mambo yote, sio kwa huduma ya macho kama watu wa kufurahisha tu, bali kwa moyo wa kweli. Mwogopeni Mungu.
23 Hvad I end foretage eder, saa gører det af Hjertet, som for Herren og ikke for Mennesker,
Chochote mfanyacho, fanyeni kutoka nafsini mwenu kama kwa Bwana na si kama kwa wanadamu.
24 da I vide, at I af Herren skulle faa Arven til Vederlag; det er den Herre Kristus, I tjene.
Mnajua ya kwamba mtapokea tuzo ya umilkaji kutoka kwa Bwana. Ni Kristo Bwana mnayemtumikia.
25 Thi den, som gør Uret, skal faa igen, hvad Uret han gjorde, og der er ikke Persons Anseelse.
Kwa sababu yeyote atendaye yasiyo haki atapokea hukumu kwa matendo yasiyo haki aliyoyafanya, na hakuna upendeleo.

< Kolossensern 3 >