< 2 Samuel 21 >
1 Og der var en Hungersnød i Davids Dage tre Aar, Aar efter Aar, og David søgte Herrens Ansigt, og Herren sagde: Det er for Sauls Skyld og for Blodhusets Skyld, fordi han ihjelslog Gibeoniterne.
Wakati wa utawala wa Daudi kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, “Ni kwa sababu ya Sauli na nyumba yake iliyotiwa madoa ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
2 Da lod Kongen kalde ad Gibeoniterne og sagde til dem: (Men Gibeoniterne vare ikke af Israels Børn, men af de overblevne Amoriter, og Israels Børn havde tilsvoret dem, men Saul søgte efter at slaa dem ihjel, fordi han var nidkær for Israels og Judas Børn)
Mfalme akawaita Wagibeoni na kuzumgumza nao. (Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, ila walikuwa mabaki ya Waamori. Waisraeli walikuwa wameapa kuwaacha hai, lakini Sauli katika wivu wake kwa ajili ya Israeli na Yuda, alikuwa amejaribu kuwaangamiza.)
3 og David sagde til Gibeoniterne: Hvad skal jeg gøre for eder? og hvormed skal jeg sone det, at I ville velsigne Herrens Arv?
Daudi akawauliza Wagibeoni, “Niwatendee nini? Nitawaridhishaje ili mbariki urithi wa Bwana?”
4 Og Gibeoniterne sagde til ham: Det er os ikke om Sølv eller Guld at gøre hos Saul og hos hans Hus, og det er os ikke om at gøre at ihjelslaa nogen i Israel; da sagde han: Hvad I sige, vil jeg gøre for eder.
Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
5 Og de sagde til Kongen: Den Mand, som udryddede os, og som tænkte det imod os, at vi skulde ødelægges, at vi ikke skulde bestaa inden al Israels Landemærke:
Wakamjibu mfalme, “Kwa habari ya mtu aliyetuangamiza na kufanya hila mbaya dhidi yetu ili kwamba tuangamizwe na tusiwe na yeyote katika Israeli,
6 Af hans Sønner lad der gives os syv Mænd, at vi kunne hænge dem op for Herren i Sauls Gibea, den Herrens udvalgtes; og Kongen sagde: Jeg vil give eder dem.
tupatieni wazao wake saba wa kiume tuwaue hadharani mbele za Bwana huko Gibea ya Sauli, aliyekuwa amechaguliwa na Bwana.” Basi mfalme akasema, “Nitawakabidhi kwenu.”
7 Men Kongen sparede Mefiboseth, en Søn af Sauls Søn Jonathan, for Herrens Eds Skyld, som var imellem dem, imellem David og Jonathan, Sauls Søn.
Mfalme akamhifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa sababu ya kile kiapo mbele za Bwana kati ya Daudi na Yonathani.
8 Og Kongen tog de to Sønner af Rizpa, Ajas Datter, hvilke hun havde født Saul, nemlig: Armoni og Mefiboseth, og Mikals, Sauls Datters, fem Sønner, hvilke hun havde født Adriel, Meholathiteren Barsillajs Søn;
Lakini mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili wa Rispa binti Aiya, ambao alikuwa amemzalia Sauli, pamoja na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliokuwa amemzalia Adrieli mwana wa Barzilai, Mmeholathi.
9 og han gav dem i Gibeoniternes Haand, og de hængte dem op paa Bjerget for Herrens Ansigt, og de faldt alle syv, og de bleve dræbte i Høstens første Dage, i Byghøstens Begyndelse.
Akawakabidhi kwa Wagibeoni, ambao waliwaua na kuwaweka wazi juu ya kilima mbele za Bwana. Wote saba walianguka kwa pamoja; waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mara tu uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.
10 Da tog Rizpa, Ajas Datter, Sørgeklædet og udbredte det paa Klippen, fra Høstens Begyndelse, indtil der faldt Vand fra Himmelen over dem; og hun tilstedte ikke Himmelens Fugle at hvile paa dem om Dagen og ej heller Markens Dyr om Natten.
Rispa binti Aiya akachukua nguo ya gunia, akajitandikia juu ya mwamba. Kuanzia mwanzo wa mavuno mpaka mvua ziliponyesha juu ya miili ya hao waliouawa, Rispa hakuruhusu ndege wa angani kuwagusa wakati wa mchana, wala wanyama wa mwitu wakati wa usiku.
11 Og det blev David tilkendegivet, det, som Rizpa, Ajas Datter, Sauls Medhustru, havde gjort.
Daudi alipoambiwa kile Rispa binti Aiya, suria wa Sauli, alichokuwa amekifanya,
12 Og David gik hen og tog fra Mændene i Jabes udi Gilead Sauls Ben og hans Søns, Jonathans, Ben, som de havde stjaalet fra Torvet i Bethsan, hvor Filisterne havde hængt dem paa den Dag, Filisterne havde slaget Saul paa Gilboa,
alikwenda akachukua mifupa ya Sauli na mwanawe Yonathani kutoka kwa watu wa Yabeshi-Gileadi. (Walikuwa wameichukua kwa siri kutoka uwanja wa watu wote huko Beth-Shani, mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika baada ya kumuua Sauli huko Gilboa.)
13 og han førte Sauls Ben og Jonathans, hans Søns, Ben op derfra, og de samlede Benene af dem, som vare hængte.
Daudi akaileta mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani kutoka huko, pia mifupa ya wale waliokuwa wameuawa na kutupwa ilikusanywa.
14 Og de begrove Sauls og hans Søn Jonathans Ben i Benjamins Land, i Zela, udi Kis's, hans Faders, Grav, og de gjorde alt det, som Kongen havde befalet; saa bønhørte Gud derefter Landet.
Wakazika mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani katika kaburi la Kishi, babaye Sauli, huko Sela katika nchi ya Benyamini, nao wakafanya kila kitu mfalme alichoagiza. Baada ya hayo, Mungu akajibu maombi kwa ajili ya nchi.
15 Og Filisterne havde endnu en Krig imod Israel, og David drog ned, og hans Tjenere med ham, og stred imod Filisterne, og David blev træt.
Kwa mara nyingine tena kulikuwa na vita kati ya Wafilisti na Israeli. Daudi akashuka pamoja na watu wake ili kupigana dhidi ya Wafilisti, naye akawa amechoka sana.
16 Og Jisbi-Benob, som var en af Rafas Børn, havde et Spyd, hvis Vægt var en Vægt af tre Hundrede Sekel Kobber, og han var ombunden med et nyt Sværd, han tænkte paa at slaa David ihjel.
Naye Ishbi-Benobu, mmoja wa wazao wa Warefai, ambaye mkuki wake ulikuwa na uzito wa shekeli 300 za shaba, alikuwa amejifunga upanga mpya, naye alisema angemuua Daudi.
17 Men Abisaj, Zerujas Søn, hjalp denne og slog Filisteren og dræbte ham; da besvore Davids Mænd ham og sagde: Du skal ikke ydermere drage ud med os i Krigen, at du ikke skal udslukke Israels Lampe.
Lakini Abishai mwana wa Seruya akaja kumwokoa Daudi; akampiga huyo Mfilisti, akamwangusha chini na kumuua. Ndipo watu wakamwapia Daudi, wakisema, “Kamwe hutakwenda tena nasi vitani, ili kwamba taa ya Israeli isije ikazimwa.”
18 Og det skete derefter, at der var endnu Krig i Gob med Filisterne, da slog Husathiteren Sibkaj Saf, som var af Rafas Børn.
Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.
19 Og der var endnu en Krig i Gob med Filisterne, og El-Hanan, Jaare-Orgims Søn, slog Beth-Lahemi, Githiteren Goliath, hvis Spydstage var som en Væverstang.
Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
20 Og der var endnu en Krig i Gath; og der var en høj Mand, som havde seks Fingre paa hver af sine Hænder, og seks Tæer paa hver af sine Fødder, det er fire og tyve i Tallet, og han var ogsaa født for Rafa.
Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
21 Og der han forhaanede Israel, da slog Jonathan, Davids Broder Simeas Søn, ham.
Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
22 Disse fire vare fødte for Rafa i Gath, og de faldt ved Davids Haand og ved hans Tjeneres Haand.
Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.