< Anden Kongebog 23 >
1 Og Kongen sendte hen, og alle de Ældste i Juda og Jerusalem samlede sig om ham.
Kisha mfalme akawaita pamoja wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
2 Og Kongen gik op i Herrens Hus, og alle Judas Mænd og alle Jerusalems Indbyggere med ham og Præsterne og Profeterne og alt Folket, baade smaa og store, og han læste for deres Øren alle Ordene i Pagtens Bog, som var funden i Herrens Hus.
Akapanda kwenda hekaluni mwa Bwana pamoja na watu wa Yuda, watu wa Yerusalemu, makuhani na manabii, watu wote wakubwa kwa wadogo. Akasoma wakiwa wanasikia maneno yote ya Kitabu cha Agano, ambacho kilikuwa kimepatikana katika Hekalu la Bwana.
3 Og Kongen stod paa Forhøjningen og gjorde Pagten for Herrens Ansigt, at de skulde vandre efter Herren og holde hans Bud og hans Vidnesbyrd og hans Skikke af ganske Hjerte og af ganske Sjæl for at hævde denne Pagts Ord, som vare skrevne i denne Bog; og alt Folket indgik Pagten.
Mfalme akasimama karibu na nguzo, na kufanya upya agano mbele za Bwana: yaani kumfuata Bwana na kuzishika amri zake, maagizo na sheria kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, hivyo kuyathibitisha maneno ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Kisha watu wote wakajifunga wenyewe kwa kiapo katika agano.
4 Og Kongen bød Hilkia, Ypperstepræsten, og Præsterne af anden Rang og Dørvogterne, at de skulde udføre af Herrens Tempel alle de Redskaber, som vare gjorte til Baal og til Astarte og til al Himmelens Hær; og de opbrændte dem uden for Jerusalem paa Kedrons Marker, og Støvet af dem lod han bringe til Bethel.
Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani mkuu, makuhani waliomfuata kwa cheo, na mabawabu kuondoa kutoka kwenye Hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali na Ashera na jeshi lote la mianga ya angani! Akavichoma nje ya Yerusalemu katika mashamba ya Bonde la Kidroni, na kuyachukua hayo majivu mpaka Betheli.
5 Og han afsatte de afgudiske Præster, som Judas Konger havde indsat, og som havde gjort Røgelse paa Højene i Judas Stæder og i dem, som laa omkring Jerusalem, samt dem, som gjorde Røgelse for Baal, for Solen og for Maanen og for Himmeltegnene og for al Himmelens Hær.
Akawafukuza makuhani wa kipagani waliokuwa wameteuliwa na wafalme wa Yuda kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Yuda na ile iliyozunguka Yerusalemu, yaani wale waliofukiza uvumba kwa Baali, kwa jua na mwezi, kwa makundi ya nyota, na jeshi lote la angani.
6 Og han lod Astartebilledet føre ud af Herrens Hus uden for Jerusalem til Kedrons Bæk og opbrændte det ved Kedrons Bæk og stødte det smaat til Støv, og han kastede dets Støv paa Folkets Børns Grave.
Akaiondoa nguzo ya Ashera kutoka kwenye Hekalu la Bwana, na kuipeleka kwenye Bonde la Kidroni nje ya Yerusalemu, akaiteketeza huko. Akaisaga hadi ikawa unga na kusambaza hilo vumbi juu ya makaburi ya watu wa kawaida.
7 Og han nedbrød de Skørlevneres Huse, som vare ved Herrens Hus, i hvilke Kvinderne vævede Telte for Astarte.
Akabomoa pia nyumba za mahanithi wa mahali pa ibada za miungu, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana na mahali wanawake walipofuma kwa ajili ya Ashera.
8 Og han lod alle Præsterne komme fra Judas Stæder og vanhelligede Højene, hvor Præsterne havde gjort Røgelse, fra Geba indtil Beersaba; og han nedbrød Højene ved Portene, den, som var ved Indgangen til Josvas, Stadsfyrstens, Port, og den, som var til venstre, naar man gaar ind ad Stadens Port.
Yosia akawaleta makuhani wote wa Bwana kutoka miji yote ya Yuda, na kunajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, kuanzia Geba hadi Beer-Sheba, mahali pote ambapo hao makuhani wa miungu walifukiza uvumba. Akabomoa mahali pa kuwekea vitu vya ibada za miungu palipokuwa katika malango, kwenye ingilio la Lango la Yoshua, mtawala wa mji, lililoko upande wa kushoto wa lango la mji.
9 Dog ofrede ikke Højenes Præster paa Herrens Alter i Jerusalem, endskønt de aad usyrede Brød midt iblandt deres Brødre.
Ingawa makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu hawakuhudumu katika madhabahu ya Bwana katika Yerusalemu, walikula mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
10 Og han vanhelligede Tofet, som var i Hinnoms Børns Dal, for at ikke nogen skulde lade sin Søn eller sin Datter gaa igennem Ilden til Molek.
Kisha mfalme akanajisi Tofethi, palipokuwa katika Bonde la Ben-Hinomu, ili mtu yeyote asiweze kupatumia kumtoa kafara mwanawe au binti yake katika moto kwa mungu Moleki.
11 Og han afskaffede de Heste, som Judas Konger havde indviet til Solen, foran Indgangen til Herrens Hus, ved Hofbetjenten Nethan-Meleks Kammer, hvilket var paa Parvarim, og han opbrændte Solens Vogne med Ild.
Akaondoa kutoka kwenye ingilio la Hekalu la Bwana wale farasi ambao wafalme wa Yuda walikuwa wamewaweka wakfu kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye ua karibu na chumba cha afisa aliyeitwa Nathan-Meleki. Basi Yosia akayachoma moto yale magari yaliyokuwa yamewekwa wakfu kwa jua.
12 Og de Altre, som vare paa Akas's Sals Tag, og som Judas Konger havde opført, og de Altre, som Manasse havde opført i de to Herrens Huses Forgaarde, nedbrød Kongen, og han skyndte sig derfra og lod deres Støv kaste i Kedrons Bæk.
Alizivunja madhabahu ambazo wafalme wa Yuda walikuwa wamezijenga kwenye paa la ghorofa ya Ahazi, pia madhabahu alizokuwa amezijenga Manase katika nyua mbili za Hekalu la Bwana. Akaziondoa huko, akazivunja vipande vipande, na kutupa hicho kifusi katika Bonde la Kidroni.
13 Og de Høje, som vare lige for Jerusalem, som vare paa den højre Haand af Mashiths Bjerg, hvilke Salomo, Israels Konge, havde bygget for Astarte, Zidoniernes Vederstyggelighed, og for Kamos, Moabiternes Vederstyggelighed, og for Milkom, Ammons Børns Vederstyggelighed, vanhelligede Kongen.
Mfalme pia akanajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, palipokuwa mashariki ya Yerusalemu upande wa kusini wa Kilima cha Uharibifu, pale ambapo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amejenga kwa ajili ya Ashtorethi mungu mke chukizo la Wasidoni, kwa ajili ya Kemoshi mungu chukizo la Wamoabu, na kwa ajili ya Moleki mungu chukizo la watu wa Amoni.
14 Og han sønderslog Støtterne og udryddede Astartebillederne og opfyldte deres Sted med Menneskeben.
Yosia akapasua yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Ashera. Kisha akafunika hayo maeneo kwa mifupa ya wanadamu.
15 Ja ogsaa det Alter, som var i Bethel, og Højen, som Jeroboam, Nebats Søn, som kom Israel til at synde, havde gjort, ja det Alter og Højen nedbrød han, og han opbrændte Højen og gjorde den til fint Støv og opbrændte Astartebilledet.
Hata madhabahu yaliyokuwa huko Betheli, mahali pa juu pa kuabudia miungu palipokuwa pamejengwa na Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye aliwafanya Israeli watende dhambi, alibomoa hata hayo madhabahu na mahali pa juu pa kuabudia miungu. Alipateketeza kwa moto hapo mahali pa juu pa kuabudia miungu na kupasaga hadi pakawa vumbi, na kuichoma hiyo nguzo ya Ashera pia.
16 Og Josias vendte sig og saa de Grave, som vare der paa Bjerget, og han sendte hen og lod tage Benene af Gravene og opbrændte dem paa Alteret og vanhelligede det efter Herrens Ord, som den Guds Mand havde udraabt, han som udraabte disse Ord.
Kisha Yosia akatazama huku na huko, naye alipoona makaburi yaliyokuwa huko kwenye kilima, akaamuru mifupa itolewe humo na akaichoma juu ya madhabahu ya Betheli ili kupanajisi. Hili lilitokea kulingana na neno la Bwana lililosemwa na mtu wa Mungu ambaye alitangulia kusema mambo haya.
17 Og han sagde: Hvad er det for et Gravmæle, som jeg ser? og Mændene i Staden sagde til ham: Det er den Guds Mands Grav, som kom fra Juda og raabte disse Ting, som du har gjort imod Alteret i Bethel.
Mfalme akauliza, “Lile kaburi lenye mnara wa ukumbusho ninaloliona ni kwa ajili gani?” Watu wa mji wakasema, “Hii ni alama ya kaburi la mtu wa Mungu aliyekuja kutoka Yuda, naye akanena dhidi ya hii madhabahu ya Betheli mambo yale yale uliyoifanyia leo.”
18 Og han sagde: Lader ham hvile, ingen flytte hans Ben; og de reddede hans Ben tillige med den Profets Ben, som kom fra Samaria.
Akasema, “Liacheni, msiliguse. Msimruhusu mtu yeyote kuiondoa mifupa yake.” Basi wakaiacha mifupa yake pamoja na ile ya yule nabii ambaye alikuwa amekuja kutoka Samaria.
19 Ja ogsaa alle Højenes Huse, som vare i Samarias Stæder, og som Israels Konger havde opført til at opirre Gud, borttog Josias og gjorde ved dem ganske paa samme Maade, som han havde gjort i Bethel.
Kama alivyokuwa amefanya huko Betheli, Yosia akabomoa na kunajisi mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu ambapo wafalme wa Israeli walikuwa wamejenga ndani ya miji ya Samaria, ambayo ilikuwa imemghadhibisha Bwana.
20 Og han slagtede alle Højenes Præster, som der vare, paa Altrene, og opbrændte Menneskeben paa dem; og han kom tilbage til Jerusalem.
Yosia akawachinja makuhani wote wa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika madhabahu zao wenyewe, na kuchoma mifupa ya wanadamu juu yake. Kisha akarudi Yerusalemu.
21 Og Kongen bød alt Folket og sagde: Holder Paaske for Herren eders Gud, saaledes som der er skrevet i denne Pagts Bog.
Mfalme akatoa agizo hili kwa watu wote: “Adhimisheni Pasaka kwa Bwana Mungu wenu, kama ilivyoandikwa katika Kitabu hiki cha Agano.”
22 Thi der var ikke holdt en Paaske som denne fra Dommernes Dage af, som dømte Israel, og gennem alle Israels Kongers og Judas Kongers Dage.
Hapakuwahi kuwepo na adhimisho lingine la Pasaka kama hilo tangu nyakati za Waamuzi walioongoza Israeli, wala katika nyakati zote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.
23 Men i Kong Josias's attende Aar blev denne Paaske holdt for Herren i Jerusalem.
Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia, Pasaka hii iliadhimishwa kwa Bwana huko Yerusalemu.
24 Men ogsaa Spaakvinderne og Tegnsudlæggerne og Husguderne og de stygge Afguder og alle de Vederstyggeligheder, som bleve sete i Judas Land og i Jerusalem, borttog Josias, for at holde Lovens Ord, som vare skrevne i Bogen, som Hilkia, Præsten, havde fundet i Herrens Hus.
Zaidi ya hayo, Yosia akawaondoa waaguzi, wanaoabudu mizimu, sanamu za kuagulia, sanamu za kuabudiwa, na vitu vingine vyote vya machukizo vilivyoonekana huko Yuda na Yerusalemu. Aliyafanya haya ili kutimiza matakwa ya sheria iliyoandikwa ndani ya kile kitabu ambacho Hilkia kuhani alikipata ndani ya Hekalu la Bwana.
25 Og der var ingen Konge som han før ham, der omvendte sig til Herren af sit ganske Hjerte og af sin ganske Sjæl og af al sin Formue efter al Moses Lov, og der opstod ej nogen efter ham som han.
Kabla wala baada ya Mfalme Yosia hapakuwepo na mfalme mwingine yeyote ambaye alimpenda Bwana kwa moyo wake wote, kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na Sheria yote ya Mose.
26 Dog vendte Herren ikke om fra sin store Vredes Ild, hvormed hans Vrede var optændt imod Juda, for alle de Opirrelser, som Manasse havde opirret ham med.
Hata hivyo, Bwana hakuacha ghadhabu yake iliyowaka dhidi ya Yuda kwa sababu ya yale yote ambayo Manase alikuwa amefanya kumghadhibisha.
27 Og Herren sagde: Jeg vil ogsaa bortkaste Juda fra mit Ansigt, ligesom jeg bortkastede Israel, og jeg vil forkaste denne Stad, som jeg udvalgte, Jerusalem, og det Hus, om hvilket jeg sagde: Mit Navn skal være der.
Hivyo Bwana akasema, “Nitamwondoa Yuda mbele zangu kama nilivyomwondoa Israeli, nami nitaukataa Yerusalemu, mji niliouchagua, na Hekalu hili, ambalo nilisema, ‘Jina langu litakaa humo.’”
28 Men det øvrige af Josias's Handeler og alt, hvad han gjorde, ere de Ting ikke skrevne i Judas Kongers Krønikers Bog?
Matukio mengine ya utawala wa Yosia na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
29 I hans Dage drog Farao Neko, Kongen af Ægypten, op imod Kongen af Assyrien til Floden Frat, og Kong Josias drog imod ham; men denne dræbte ham i Megiddo, der han havde set ham.
Yosia alipokuwa mfalme, Farao Neko mfalme wa Misri akapanda mpaka Mto Frati kumsaidia mfalme wa Ashuru. Mfalme Yosia akatoka kwenda kupigana naye, lakini Neko akamkabili na kumuua huko Megido.
30 Og hans Tjenere førte ham død fra Megiddo og førte ham til Jerusalem og begravede ham i hans Grav; og Folket i Landet tog Joakas, Josias's Søn, og salvede ham og gjorde ham til Konge i hans Faders Sted.
Watumishi wa Yosia wakauleta mwili wake katika gari la vita kutoka Megido hadi Yerusalemu, wakamzika kwenye kaburi lake mwenyewe. Nao watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta na kumfanya mfalme mahali pa baba yake.
31 Joakas var tre og tyve Aar gammel, der han blev Konge, og regerede tre Maaneder i Jerusalem, og hans Moders Navn var Hamutal, Jeremias's Datter fra Libna.
Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia kutoka Libna.
32 Og han gjorde det, som var ondt for Herrens Øjne, efter alt det, som hans Fædre gjorde.
Akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyofanya.
33 Og Farao Neko lod ham lægge i Lænker i Ribla udi Hamaths Land, at han ikke skulde regere i Jerusalem, og han lagde en Straf paa Landet, hundrede Centner Sølv og et Centner Guld.
Farao Neko akamfunga kwa minyororo huko Ribla katika nchi ya Hamathi ili asiweze kutawala huko Yerusalemu, naye akatoza kodi ya talanta mia moja za fedha, na talanta moja ya dhahabu katika Yuda.
34 Og Farao Neko gjorde Eliakim, Josias's Søn, til Konge i hans Faders, Josias's Sted, og omvendte hans Navn til Jojakim; men Joakas tog han med, og denne kom til Ægypten og døde der.
Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme mahali pa baba yake Yosia, na kulibadilisha jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri, naye akafia huko.
35 Og Jojakim gav Farao Sølvet og Guldet, men han lignede en Skat paa Landet for at kunne give Pengene efter Faraos Befaling; eftersom Skatten var lignet paa hver især, inddrev han Sølvet og Guldet af Folket i Landet for at give det til Farao Neko.
Yehoyakimu akamlipa Farao Neko ile fedha na dhahabu aliyodai. Ili kuweza kufanya hivyo, Yehoyakimu akatoza nchi kodi na kulipiza fedha na dhahabu kutoka kwa watu wa nchi kulingana na makadrio ya mapato yao.
36 Jojakim var fem og tyve Aar gammel, der han blev Konge, og regerede elleve Aar i Jerusalem, og hans Moders Navn var Sebuda, Pedajas Datter fra Ruma.
Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Zebida binti Pedaya kutoka Ruma.
37 Og han gjorde det, som var ondt for Herrens Øjne, efter alt det, som hans Fædre havde gjort.
Naye akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyokuwa wamefanya.