< Anden Kongebog 15 >

1 Idet syv og tyvende Jeroboams, Israels Konges, Aar blev Asaria, Amazias, Judas Konges, Søn, Konge.
Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Han var seksten Aar gammel, der han blev Konge, og regerede to og halvtredsindstyve Aar i Jerusalem, og hans Moders Navn var Jekolia fra Jerusalem.
Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
3 Og han gjorde det, som var ret for Herrens Øjne, efter alt det, som hans Fader Amazia gjorde.
Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
4 Dog kom Højene ikke bort; Folket ofrede endnu og gjorde Ragelse paa Højene.
Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
5 Og Herren slog Kongen, at han blev spedalsk indtil sin Dødsdag og boede udi et særskilt Hus; men Jotham, Kongens Søn, var over Huset og dømte Folket i Landet.
Bwana akampiga mfalme kwa ukoma mpaka siku aliyokufa, naye aliishi katika nyumba iliyotengwa peke yake. Yothamu mwana wa mfalme akawa msimamizi wa jumba la mfalme, na akawatawala watu wa nchi.
6 Men det øvrige af Asarias Handeler og alt, hvad han gjorde, er det ikke skrevet i Judas Kongers Krønikers Bog?
Matukio mengine ya utawala wa Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
7 Og Asaria laa med sine Fædre, og de begavede ham hos hans Fædre i Davids Stad, og Jotham, hans Søn, blev Konge i hans Sted.
Azaria akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika Mji wa Daudi, na Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
8 Og i det otte og tredivte Asarias, Judas Konges, Aar blev Sakaria, Jeroboams Søn, Konge over Israel i Samaria seks Maaneder.
Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, naye akatawala miezi sita.
9 Og han gjorde det, som var ondt for Herrens Øjne, ligesom hans Fædre gjorde, han veg ikke fra Jeroboams, Nebats Søns, Synder, som han kom Israel til at synde med.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama baba zake walivyofanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
10 Og Sallum, Jabes's Søn, gjorde et Forbund imod ham og slog ham i Folkets Paasyn og dræbte ham og blev Konge i hans Sted.
Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya shauri baya dhidi ya Zekaria. Akamshambulia mbele ya watu, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
11 Men det øvrige af Sakarias Handeler, se, de Ting ere skrevne i Israels Kongers Krønikers Bog.
Matukio mengine ya utawala wa Zekaria yameandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
12 Dette er Herrens Ord, som han talte til Jehu, sigende: Dine Sønner i det fjerde Led skulle sidde paa Israels Trone; og det skete saa.
Kwa hiyo neno la Bwana lililonenwa kwa Yehu likatimia, kwamba, “Wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
13 Sallum, Jabes's Søn, blev Konge i det ni og tredivte Usias, Judas Konges, Aar, og regerede en Maaneds Tid i Samaria.
Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa thelathini na tisa wa Uzia mfalme wa Yuda, naye akatawala katika Samaria kwa mwezi mmoja.
14 Og Menahem, Gadis Søn, drog op fra Thirza og kom til Samaria og slog Sallum, Jabes's Søn, i Samaria og dræbte ham og blev Konge i hans Sted.
Kisha Menahemu mwana wa Gadi akaenda kutoka Tirsa mpaka Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi huko Samaria, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
15 Men det øvrige af Sallums Handeler og hans Forbund, som han indgik, se, de Ting ere skrevne i Israels Kongers Krønikers Bog.
Matukio mengine ya utawala wa Shalumu, na mauaji aliyoyafanya, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
16 Da slog Menahem Thipsa og alle, som vare deri, og dens Landemærke, da han drog ud fra Thirza; fordi man ikke havde villet indlade ham, derfor slog han dem; alle de frugtsommelige derudi søndersled han.
Wakati ule, akianzia Tirsa, Menahemu alishambulia Tifsa na kila mtu ndani yake, na wale waliokuwa maeneo jirani, kwa sababu walikataa kufungua malango yao. Akaiangamiza Tifsa yote, na kuwapasua matumbo wanawake wote wenye mimba.
17 Og i det ni og tredivte Asarias, Judas Konges, Aar blev Menahem, Gadis Søn, Konge over Israel, ti Aar i Samaria.
Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, akatawala huko Samaria kwa miaka kumi.
18 Og han gjorde det, som var ondt for Herrens Øjne, han veg ikke fra Jeroboams, Nebats Søns, Synder, som han kom Israel til at synde med, alle sine Dage.
Akatenda maovu machoni pa Bwana. Katika wakati wa utawala wake wote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
19 Ful, Kongen af Assyrien, kom over Landet, og Menahem gav Ful tusinde Centner Sølv, at han skulde holde med ham og befæste Riget i hans Haand.
Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaishambulia Israeli. Menahemu mfalme wa Israeli akampa talanta elfu moja za fedha ili amsaidie na kumwezesha katika utawala wake.
20 Og Menahem indkrævede det Sølv af Israel, af alle de formuende, til at give Kongen af Assyrien, nemlig halvtredsindstyve Sekel Sølv for hver Mand; saa drog Kongen af Assyrien tilbage og blev ikke der i Landet.
Menahemu akatoza fedha hizi kwa nguvu kutoka kwa Israeli. Kila mtu tajiri alilazimika kuchanga shekeli hamsini za fedha ambazo alipewa mfalme wa Ashuru. Basi mfalme wa Ashuru akajiondoa na hakuendelea kuikalia nchi.
21 Men det øvrige af Menahems Handeler og alt det, han gjorde, er det ikke skrevet i Israels Kongers Krønikers Bog?
Matukio mengine ya utawala wa Menahemu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
22 Og Menahem laa med sine Fædre, og Pekaja, hans Søn, blev Konge i hans Sted.
Menahemu akalala pamoja na baba zake. Naye Pekahia mwanawe akawa mfalme baada yake.
23 I det halvtredsindstyvende Asarias, Judas Konges, Aar blev Pekaja, Menahems Søn, Konge over Israel i Samaria i to Aar.
Katika mwaka wa hamsini wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, akatawala miaka miwili.
24 Og han gjorde det, som var ondt for Herrens Øjne, han veg ikke fra Jeroboams, Nebats Søns, Synder, som han kom Israel til at synde med.
Pekahia akafanya uovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
25 Og Peka, Remalias Søn, hans Høvedsmand, gjorde et Forbund imod ham og ihjelslog i Samaria, i Kongens Hus's Palads, ham og Argob og Arje; og han havde med sig halvtredsindstyve Mænd af Gileaditernes Børn og dræbte ham og blev Konge i hans Sted.
Mmoja wa maafisa wake wakuu, Peka mwana wa Remalia, akafanya shauri baya dhidi yake. Akachukua watu hamsini wa Gileadi pamoja naye, akamuua Pekahia, pamoja na Argobu na Aria, katika ngome ya jumba la kifalme huko Samaria. Kwa hiyo Peka akamuua Pekahia, naye akaingia mahali pake kuwa mfalme.
26 Men det øvrige af Pekajas Handeler og alt det, han gjorde, se, de Ting ere skrevne i Israels Kongers Krønikers Bog.
Matukio mengine ya utawala wa Pekahia na yote aliyoyafanya yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
27 I det to og halvtredsindstyvende Asarias, Judas Konges, Aar blev Peka, Remalias Søn, Konge over Israel i Samaria i tyve Aar.
Katika mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala miaka ishirini.
28 Og han gjorde det, som var ondt for Herrens Øjne, han veg ikke fra Jeroboams, Nebats Søns, Synder, som han kom Israel til at synde med.
Akafanya maovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
29 I Pekas, Israels Konges, Dage kom Thiglath-Pileser, Kongen af Assyrien, og tog Ijon og Abel-Beth-Maaka og Ianoa og Kedes og Hasor og Gilead og Galilæa, alt Nafthalis Land, og han bortførte dem til Assyrien.
Wakati wa utawala wa Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alikuja na kuteka Iyoni, Abel-Beth-Maaka, Yanoa, Kedeshi na Hazori. Akateka miji ya Gileadi na Galilaya, pamoja na nchi yote ya Naftali, na kuwahamishia watu wote Ashuru.
30 Og Hosea, Elas Søn, gjorde et Forbund imod Peka, Remalias Søn, og slog ham og dræbte ham og blev Konge i hans Sted, i det tyvende Jothams, Ussias Søns, Aar.
Kisha Hoshea mwana wa Ela akafanya shauri baya dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akamshambulia na kumuua, kisha akaingia mahali pake kuwa mfalme katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
31 Men det øvrige af Pekas Handeler og alt det, han gjorde, se, de Ting ere skrevne i Israels Kongers Krønikers Bog.
Matukio mengine ya utawala wa Peka na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
32 I det andet Pekas, Remalias Søns, Israels Konges, Aar blev Jotham, en Søn af Judas Konge Ussia, Konge.
Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Uzia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
33 Han var fem og tyve Aar gammel, der han blev Konge, og han regerede seksten Aar i Jerusalem, og hans Moders Navn var Jerusa, Zadoks Datter.
Alikuwa na miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
34 Og han gjorde det, som var ret for Herrens Øjne, efter alt det, som Ussia, hans Fader, gjorde.
Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya.
35 Dog blev Højene ikke borttagne, Folket ofrede endnu og gjorde Røgelse paa Højene; han byggede den øverste Port paa Herrens Hus.
Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko. Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana.
36 Men det øvrige af Jothams Handeler og alt det, han gjorde, ere de Ting ikke skrevne i Judas Kongers Krønikers Bog?
Matukio mengine ya utawala wa Yothamu na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
37 I de Dage begyndte Herren at sende Rezin, Kongen af Syrien, og Peka, Remalias Søn, mod Juda.
(Katika siku hizo, Bwana akaanza kuwatuma Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia dhidi ya Yuda.)
38 Og Jotham laa med sine Fædre og blev begraven hos sine Fædre i Davids, sin Faders, Stad, og Akas, hans Søn, blev Konge i hans Sted.
Yothamu akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi, mji wa baba zake. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.

< Anden Kongebog 15 >