< 2 Korinterne 10 >

1 Men jeg selv, Paulus, formaner eder ved Kristi Sagtmodighed og Mildhed, jeg, som, „naar I se derpaa, er ydmyg iblandt eder, men fraværende er modig over for eder”,
Basi, mimi Paulo ninawasihi kwa unyenyekevu na upole wa Kristo, mimi niliye “mwoga” ninapokuwa pamoja nanyi ana kwa ana, lakini mwenye ujasiri nikiwa mbali nanyi!
2 ja, jeg beder eder om ikke nærværende at skulle være modig med den Tillidsfuldhed, hvormed jeg agter at træde dristigt op imod nogle, som anse os for at vandre efter Kødet.
Nawaomba nitakapokuja kwenu nisiwe na ujasiri dhidi ya watu fulani, kama ninavyotazamia kwa wale wanaodhani kwamba tunaishi kwa kufuata namna ya ulimwengu huu.
3 Thi om vi end vandre i Kødet, saa stride vi dog ikke efter Kødet;
Ingawa tunaishi duniani, hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo.
4 thi vore Stridsvaaben ere ikke kødelige, men mægtige for Gud til Fæstningers Nedbrydelse,
Silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome,
5 idet vi nedbryde Tankebygninger og al Højhed, som rejser sig imod Erkendelsen af Gud, og tage enhver Tanke til Fange til Lydighed imod Kristus
tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu, na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo,
6 og ere rede til at straffe al Ulydighed, naar eders Lydighed er bleven fuldkommen.
tena tukiwa tayari kuadhibu kila tendo la kutotii, kutii kwenu kutakapokamilika.
7 Se I paa det udvortes? Dersom nogen trøster sig til selv at høre Kristus til, da slutte han igen fra sig selv, at ligesom han hører Kristus til, saaledes gøre vi det ogsaa.
Angalieni yale yaliyo machoni penu. Kama mtu yeyote anaamini kuwa yeye ni mali ya Kristo, basi kumbuka kuwa kama ulivyo wa Kristo, vivyo hivyo na sisi ndivyo tulivyo.
8 Ja, dersom jeg endog vilde rose mig noget mere af vor Magt, som Herren gav os til eders Opbyggelse og ikke til eders Nedbrydelse, skal jeg dog ikke blive til Skamme,
Basi hata kama nikijisifu zaidi kidogo kuhusu mamlaka tuliyo nayo, ambayo Bwana alitupa ili kuwajenga wala si kuwabomoa, mimi sitaionea haya.
9 for at jeg ikke skal synes at ville skræmme eder ved mine Breve;
Sitaki nionekane kama ninayejaribu kuwatisha kwa nyaraka zangu.
10 thi Brevene, siger man, ere vægtige og stærke, men hans legemlige Nærværelse er svag, og hans Tale intet værd.
Kwa maana wanasema, “Nyaraka zake ni nzito na zenye nguvu, lakini ana kwa ana ni dhaifu na kuzungumza kwake ni kwa kudharauliwa.”
11 En saadan betænke, at saaledes som vi fraværende ere med Ord ved Breve, saaledes ville vi ogsaa nærværende være i Gerning.
Watu kama hao wajue ya kuwa, yale tusemayo kwa barua tukiwa hatupo pamoja nanyi, ndivyo tulivyo na ndivyo tutakavyofanya tutakapokuwa pamoja nanyi.
12 Thi vi driste os ikke til at regne os iblandt eller sammenligne os med somme af dem, der anbefale sig selv; men selv indse de ikke, at de maale sig med sig selv og sammenligne sig med sig selv.
Hatuthubutu kujiweka kwenye kundi moja au kujilinganisha na hao wanaojitukuza wenyewe kuwa wao ni wa maana sana. Wanapojipima na kujilinganisha wenyewe kwa wenyewe, wanaonyesha ya kuwa hawana busara.
13 Vi derimod ville ikke rose os ud i det umaalelige, men efter Maalet af den Grænselinie, som Gud har tildelt os som Maal, at naa ogsaa til eder.
Lakini sisi hatujajivuna kupita kiasi, bali majivuno yetu yatakuwa katika mipaka ile Mungu aliyotuwekea, mipaka ambayo inawafikia hata ninyi.
14 Thi vi strække os ikke for vidt, som om vi ikke naaede til eder; vi ere jo komne ogsaa indtil eder i Kristi Evangelium,
Kwa maana hatukuwa tunavuka mipaka katika kujisifu kwetu, kama vile ambavyo ingekuwa kama hatukuwa tumekuja kwenu. Kwa maana sisi ndio tuliokuwa wa kwanza kuja kwenu na Injili ya Kristo.
15 saa vi ikke rose os ud i det umaalelige af andres Arbejder, men have det Haab, at, naar eders Tro vokser, ville vi hos eder blive store, efter vor Grænselinie, saa vi kunne komme langt videre
Wala hatuvuki mipaka kwa kujisifu kwetu kwa ajili ya kazi iliyofanywa na watu wengine. Tumaini letu ni kwamba imani yenu inavyozidi kukua, eneo letu la utendaji miongoni mwenu litapanuka zaidi,
16 og forkynde Evangeliet i Landene hinsides eder, men ikke rose os inden for en andens Grænselinie af det allerede fuldførte.
ili tuweze kuhubiri Injili sehemu zilizo mbali na maeneo yenu. Kwa maana hatutaki kujisifu kwa ajili ya kazi ambayo imekwisha kufanyika tayari katika eneo la mtu mwingine.
17 Men den, som roser sig, rose sig af Herren!
Lakini, “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”
18 Thi ikke den, der anbefaler sig selv, staar Prøve, men den, hvem Herren anbefaler.
Kwa maana si yeye ajisifuye mwenyewe akubaliwaye, bali yeye ambaye Bwana humsifu.

< 2 Korinterne 10 >