< Anden Krønikebog 9 >
1 Og Dronningen af Seba hørte Salomos Rygte og kom for at prøve Salomo med mørke Taler til Jerusalem med en saare stor Skare af Kameler, som bare vellugtende Urter og Guld i Mangfoldighed og dyrebare Stene; og hun kom til Salomo og talte med ham alt det, som var i hendes Hjerte.
Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
2 Og Salomo udtydede hende alle hendes Ord, og der var ikke et Ord skjult for Salomo, som han ej udtydede hende.
Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
3 Da Dronningen af Seba saa Salomos Visdom og det Hus, som han havde bygget,
Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
4 og Maden til hans Bord og hans Tjeneres Bolig, og hvordan de stode, som opvartede ham, og deres Klæder og hans Mundskænke og deres Klæder og hans Opgang, ad hvilken han gik op til Herrens Hus: Da var hun ude af sig selv.
chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
5 Og hun sagde til Kongen: Det Ord er sandt, som jeg har hørt i mit Land om dine Sager og om din Visdom;
Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
6 og jeg vilde ikke tro deres Ord, førend jeg kom, og mine Øjne have set det, og se, ikke Halvdelen er mig forkyndt af din megen Visdom; du har mere end efter Rygtet, som jeg har hørt.
Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
7 Salige ere dine Mænd, og salige ere disse dine Tjenere, som stedse staa for dit Ansigt, og som høre din Visdom!
Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
8 Lovet være Herren din Gud, som havde Lyst til dig, at sætte dig paa sin Trone til Konge for Herren, din Gud! Fordi din Gud elsker Israel og vil befæste det evindelig, derfor satte han dig til Konge over dem, til at gøre Ret og Retfærdighed.
Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
9 Og hun gav Kongen hundrede og tyve Centner Guld og saare mange vellugtende Urter og dyrebare Stene; der var ikke saadanne Urter som disse, hvilke Dronningen af Seba gav Kong Salomo.
Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
10 Dertil med havde Hurams Tjenere og Salomos Tjenere bragt Guld fra Ofir og bragt Hebentræ og dyrebare Stene.
(Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
11 Og af Hebentræet lod Kongen gøre Gange til Herrens Hus og til Kongens Hus, samt Harper og Psaltre til Sangerne; og der blev ikke tilforn set saadant som dette i Judas Land.
Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
12 Og Kong Salomo gav Dronningen af Seba alt det, hun havde Lyst til, som hun begærede, foruden Gaver for det, som hun havde medbragt til Kongen; og hun vendte om og drog til sit Land, hun og hendes Tjenere.
Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
13 Og Vægten paa det Guld, som kom til Salomo paa eet Aar, var seks Hundrede og seks og tresindstyve Centner Guld
Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
14 foruden det, som indkom fra Toldbetjentene, og det, som Købmændene bragte; og alle Kongerne af Arabia og Fyrsterne i Landet bragte Guld og Sølv til Salomo.
mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
15 Og Kong Salomo lod gøre to Hundrede Skjolde af drevet Guld; seks Hundrede Sekel drevet Guld lod han gaa paa hvert Skjold;
Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
16 og tre Hundrede smaa Skjolde af drevet Guld, tre Hundrede Sekel Guld lod han gaa paa hvert Skjold; og Kongen lagde dem i Libanons Skovhus.
Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
17 Og Kongen lod gøre en stor Trone af Elfenben og beslog den med purt Guld.
Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
18 Og Tronen havde seks Trin og en Skammel, som med Guld vare fastgjorte til Tronen, og der var Arme paa begge Sider omkring Sædets Sted, og to Løver stode ved Armene.
Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
19 Og der stod tolv Løver paa de seks Trin paa begge Sider; saadant er ikke gjort i noget Rige.
Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
20 Og alle Kong Salomos Drikkekar vare af Guld, og alle Karrene i Libanons Skovhus vare af fint Guld; Sølv agtedes ikke for noget i Salomos Dage.
Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
21 Thi Kongens Skibe fore til Tharsis med Hurams Tjenere; een Gang i tre Aar kom de Tharsis Skibe, som bragte Guld og Sølv, Elfenben, Aber og Paafugle.
Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
22 Og Kong Salomo blev større end alle Konger paa Jorden ved Rigdom og Visdom.
Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
23 Og alle Jordens Konger søgte Salomos Ansigt for at høre hans Visdom, som Gud havde givet i hans Hjerte.
Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
24 Og de førte hver sin Skænk: Sølvkar og Guldkar og Klæder, Rustninger og vellugtende Urter, Heste og Muler, hvilket skete aarligt.
Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
25 Og Salomo havde fire Tusinde Stalde til Heste og Vogne og tolv Tusinde Ryttere, og han lod dem blive i Vognstæderne og hos Kongen i Jerusalem.
Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
26 Og han herskede over alle Kongerne, fra Floden og indtil Filisternes Land og indtil Ægyptens Landemærke.
Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
27 Og Kongen gjorde Sølvet i Jerusalem som Stenene og gjorde Cedertræerne som Morbærtræerne, der ere i Lavlandet i Mangfoldighed.
Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
28 Og man udførte Heste til Salomo fra Ægypten og fra alle Landene.
Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
29 Men det øvrige af Salomos Handeler, de første og de sidste, ere de Ting ikke skrevne i Profeten Nathans Krønike og i Siloniten Ahias Profeti og i Seeren Jeddis Syn imod Jeroboam, Nebats Søn?
Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
30 Og Salomo regerede i Jerusalem over al Israel fyrretyve Aar.
Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
31 Og Salomo laa med sine Fædre, og de begrove ham i Davids, hans Faders, Stad; og Roboam, hans Søn, blev Konge i hans Sted.
Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.