< 1 Samuel 2 >
1 Da bad Hanna og sagde: Mit Hjerte har frydet sig i Herren, mit Horn er ophøjet i Herren; min Mund er vidt opladt over mine Fjender, thi jeg har glædet mig i din Frelse.
Kisha Hana akaomba na kusema: “Moyo wangu wamshangilia Bwana, katika Bwana pembe yangu imeinuliwa juu. Kinywa changu chajisifu juu ya adui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
2 Der er ingen hellig som Herren; thi der er ingen foruden dig og ingen Klippe som vor Gud.
“Hakuna yeyote aliye mtakatifu kama Bwana, hakuna mwingine zaidi yako; hakuna Mwamba kama Mungu wetu.
3 Taler ikke saa mange Ord, saa saare høje Ting, lader ikke noget frækt udgaa af eders Mund; thi Herren er Vidskabs Gud, skulde hans Gerninger ikke være rette?
“Msiendelee kusema kwa kiburi hivyo wala msiache vinywa vyenu kunena kwa kiburi, kwa kuwa Bwana ndiye Mungu ajuaye, na kwa yeye matendo hupimwa.
4 De stærkes Bue er brudt, og de skrøbelige ere omgjordede med Styrke.
“Pinde za mashujaa zimevunjika, lakini wale wanaojikwaa wamevikwa nguvu.
5 De mætte lade sig leje for Brød, de hungrige hungre ej mere; ja, den ufrugtbare føder syv, men hun med de mange Sønner visner hen.
Wale waliokuwa na chakula tele wamejikodisha wenyewe ili kupata chakula, lakini wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Mwanamke yule aliyekuwa tasa amezaa watoto saba, lakini yule ambaye alikuwa na wana wengi amedhoofika.
6 Herren er den, som døder og gør levende, som nedfører til Dødsriget og fører op igen. (Sheol )
“Bwana huua na huleta uhai, hushusha chini mpaka kaburini na hufufua. (Sheol )
7 Herren er den, som gør fattig og gør rig, han er den, som nedtrykker, og den, som ophøjer;
Bwana humfanya mtu maskini naye hutajirisha, hushusha na hukweza.
8 han oprejser den ringe af Støvet, han ophøjer den fattige af Skarnet, for at sætte dem hos Fyrsterne og lade dem arve Ærens Trone; thi Jordens Grundvold hører Herren til, og han har sat Jorderige derpaa.
Humwinua maskini kutoka mavumbini na humwinua mhitaji kutoka lundo la majivu; huwaketisha pamoja na wakuu na kuwafanya warithi kiti cha enzi cha heshima. “Kwa kuwa misingi ya dunia ni ya Bwana; juu yake ameuweka ulimwengu.
9 Han skal bevare sine frommes Fødder, men ugudelige skulle vorde stumme i Mørket; thi en Mand bliver ikke vældig ved sin Kraft.
Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake, lakini waovu watanyamazishwa kwenye giza. “Si kwa nguvu mtu hushinda;
10 De, som trætte med Herren, skulle forskrækkes, han skal lade tordne i Himmelen over dem; Herren skal dømme Jorderiges Ender, og han skal give sin Konge Styrke og ophøje sin salvedes Horn.
wale wampingao Bwana wataharibiwa kabisa. Atapiga radi dhidi yao kutoka mbinguni; Bwana ataihukumu miisho ya dunia. “Atampa nguvu mfalme wake, na kuitukuza pembe ya mpakwa mafuta wake.”
11 Derefter gik Elkana til Rama, til sit Hus; men Drengen tjente Herren for Præsten Elis Ansigt.
Kisha Elikana akaenda nyumbani Rama, lakini mtoto akahudumu mbele za Bwana chini ya kuhani Eli.
12 Og Elis Sønner vare Belials Sønner; de kendte ikke Herren.
Wana wa Eli walikuwa watu wabaya kabisa, hawakumheshimu Bwana.
13 Thi det var Præsternes Vis med Folket: Naar nogen Mand ofrede et Offer, da kom Præstens Dreng, naar Kødet kogte, og havde en Madkrog med tre Grene i sin Haand.
Basi ilikuwa desturi ya makuhani pamoja na watu kwamba kila mara yeyote anapotoa dhabihu na huku nyama ikiwa inachemshwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na uma wenye meno matatu mkononi mwake.
14 Og han stak i Kedlen eller i Gryden eller i Panden eller i Potten; alt hvad Madkrogen drog op, det tog Præsten dermed; saaledes gjorde de mod al Israel, som kom derhen til Silo.
Angeutumbukiza huo uma kwenye sufuria au birika au sufuria kubwa au chungu, naye kuhani angalijichukulia mwenyewe chochote ambacho uma ungekileta. Hivi ndivyo walivyowatendea Waisraeli wote waliokuja Shilo.
15 Ogsaa førend de gjorde Røgoffer af Fedtet, da kom Præstens Dreng og sagde til den Mand, som ofrede: Giv mig Kød til at stege til Præsten; thi han vil ikke tage kogt Kød af dig, men raat.
Lakini hata kabla mafuta ya mnyama hayajachomwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na kusema kwa mtu ambaye alikuwa akitoa dhabihu, “Mpe kuhani nyama akaoke, kwani hatapokea nyama iliyochemshwa kutoka kwako, ila iliyo mbichi tu.”
16 Naar Manden sagde til ham: Man skal gøre Røgoffer af Fedtet i Dag; tag dig siden, saaledes som dit Hjerte begærer; da sagde han til ham: Nu skal du dog give det, og hvis ikke, vil jeg tage det med Magt.
Kama mtu akimwambia, “Mafuta ya mnyama na yachomwe kwanza, ndipo uchukue chochote unachotaka,” mtumishi angalijibu, “Hapana, nipe sasa, kama huwezi nitaichukua kwa nguvu.”
17 Og de unge Mænds Synd var saare stor for Herrens Ansigt; thi Mændene foragtede Herrens Madoffer.
Hii Dhambi ya hawa vijana ilikuwa kubwa sana machoni pa Bwana, kwa kuwa waliitendea dhabihu ya Bwana kwa dharau.
18 Og Samuel tjente for Herrens Ansigt og var en Dreng, iført en linnet Livkjortel.
Lakini Samweli alikuwa akihudumu mbele za Bwana, kijana akivaa kisibau cha kitani.
19 Og hans Moder gjorde ham en liden Overkjortel og bragte ham den op fra Aar til Aar, naar hun gik op med sin Mand til at ofre det aarlige Offer.
Kila mwaka mama yake alimshonea joho dogo na kumchukulia wakati alipokwea pamoja na mumewe kutoa dhabihu ya mwaka.
20 Og Eli velsignede Elkana og hans Hustru og sagde: Herren give dig Sæd af denne Kvinde, i Stedet for ham, som begæredes for Herren, og de gik til deres Sted.
Eli alikuwa akiwabariki Elikana na mkewe, akisema, “Bwana na akupe watoto kwa mwanamke huyu ili kuchukua nafasi ya yule aliyekuwa amemwomba na akamtoa kwa Bwana.” Kisha wakawa wanakwenda nyumbani.
21 Men Herren besøgte Hanna, at hun undfangede og fødte tre Sønner og to Døtre; og Drengen Samuel blev stor hos Herren.
Bwana akawa mwenye neema kwa Hana, naye akapata mimba akazaa wana watatu na binti wawili. Wakati huo, kijana Samweli akaendelea kukua mbele za Bwana.
22 Og Eli var saare gammel, og han hørte alt det, hans Sønner gjorde mod al Israel, og at de laa hos de Kvinder, som kom i Hobetal for Forsamlingens Pauluns Dør.
Basi Eli, ambaye alikuwa mzee sana, alisikia kuhusu kila kitu ambacho wanawe walikuwa wakiwafanyia Israeli wote na jinsi walivyokutana kimwili na wanawake waliohudumu kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
23 Og han sagde til dem: Hvorfor gøre I disse Ting? thi jeg hører disse eders onde Handeler af alt dette Folk.
Hivyo akawaambia, “Kwa nini mmefanya mambo kama haya? Nimesikia kutoka kwa watu wote juu ya haya matendo yenu maovu.
24 Ikke saa, mine Sønner; thi det er ikke et godt Rygte, som jeg hører; I komme Herrens Folk til at begaa Overtrædelse.
Sivyo, wanangu, hii si habari nzuri ambayo ninasikia ikienea miongoni mwa watu wa Bwana.
25 Dersom en Mand synder mod en Mand, da skal Gud dømme ham; men dersom nogen synder mod Herren, hvo skal da bede for ham? Men de hørte ikke deres Faders Røst; thi Herren havde Villie til at slaa dem ihjel.
Kama mtu akifanya dhambi dhidi ya mtu mwenzake, mtu mwingine aweza kumwombea kwa Mungu, lakini kama mtu akimfanyia Mungu dhambi, ni nani atakayemwombea?” Hata hivyo wanawe hawakusikia maonyo ya baba yao, kwa sababu Bwana alitaka kuwaua.
26 Men Drengen Samuel tiltog i Alder og i Velbehagelighed, baade for Herren saa og for Menneskene.
Naye kijana Samweli akaendelea kukua katika kimo, akimpendeza Bwana na wanadamu.
27 Og en Guds Mand kom til Eli, og han sagde til ham: Saaledes siger Herren: Har jeg ikke aabenbaret mig for din Faders Hus, der de vare i Ægypten i Faraos Hus?
Basi mtu wa Mungu akaja kwa Eli na kumwambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Je, sikujifunua waziwazi kwa nyumba ya baba yako wakati walikuwa huko Misri chini ya Farao?
28 Og jeg har udvalgt ham af alle Israels Stammer mig til en Præst, til at ofre paa mit Alter, til at røge med Røgelse, til at bære Livkjortlen for mit Ansigt, og jeg har givet din Faders Hus alle Israels Børns Ildofre.
Nilimchagua baba yako kati ya makabila yote ya Israeli kuwa kuhani wangu, kukwea kwenye madhabahu yangu, kufukiza uvumba na kuvaa kisibau mbele yangu. Pia niliwapa nyumba ya baba yako sadaka zote zilizotolewa kwa moto na Waisraeli.
29 Hvorfor vanære I mit Slagtoffer og mit Madoner, som jeg bød at ofre i Boligen? og du ærer dine Sønner mere end mig, idet I fede eder med det bedste af alt mit Folks Israels Madofre!
Kwa nini unadharau dhabihu zangu na sadaka zile nilizoziamuru kwa ajili ya makao yangu? Kwa nini unawaheshimu wanao kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu zilizo bora za kila sadaka zinazotolewa na watu wangu wa Israeli?’
30 Derfor siger Herren, Israels Gud: Vistnok har jeg sagt: Dit Hus og din Faders Hus skulle vandre for mit Ansigt til evig Tid; men nu siger Herren: Det være langt fra mig; thi dem, som ære mig, vil jeg ære, og de, som foragte mig, skulle ringeagtes.
“Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli asema: ‘Niliahidi kuwa nyumba yako na nyumba ya baba yako wangehudumu mbele zangu milele.’ Lakini sasa Bwana anasema: ‘Jambo hili na liwe mbali nami! Wale wanaoniheshimu nitawaheshimu, wale wanaonidharau mimi watadharauliwa.
31 Se, de Dage komme, at jeg vil afhugge din Arm og din Faders Huses Arm, at der ikke skal være en gammel i dit Hus.
Wakati unakuja nitakapozipunguza nguvu zenu na nguvu ya nyumba ya baba yenu, ili pasiwepo mtu katika mbari yenu atakayeishi kuuona uzee
32 Og du skal se Trængsel for Boligen i alt, hvori det skulde gaaet Israel vel; og der skal ingen gammel være i dit Hus nogen Sinde.
nanyi mtaona huzuni katika makao yangu. Ingawa Israeli watafanyiwa mema, katika mbari yenu kamwe hapatakuwepo mtu atakayeishi hadi kuwa mzee.
33 Og jeg vil ikke udrydde hver Mand af dig fra mit Alter til at fortære dine Øjne og at bedrøve din Sjæl; dog skal hele dit Huses Mangfoldighed dø som Mænd.
Kila mmoja wenu ambaye sitamkatilia mbali kutoka madhabahuni pangu atabakizwa tu kupofusha macho yenu kwa machozi na kuihuzunisha mioyo yenu, nao wazao wenu wote watakufa watakapokuwa wamefikia umri wa kustawi.
34 Og dette skal være dig et Tegn, som skal komme over dine to Sønner, over Hofni og Pinehas: Paa een Dag skulle de begge dø.
“‘Kile kitakachotokea kwa wanao wawili, Hofni na Finehasi, kitakuwa ishara kwako. Wote wawili watakufa katika siku moja.
35 Og jeg vil oprejse mig en trofast Præst, han skal gøre, ligesom det er i mit Hjerte og i min Sjæl; og jeg vil bygge ham et bestandigt Hus, og han skal vandre for min salvedes Ansigt alle Dage.
Mimi mwenyewe nitajiinulia kuhani mwaminifu, ambaye atafanya sawasawa na kile kilichoko moyoni mwangu na akilini mwangu. Nitaifanya nyumba yake kuwa imara, naye atahudumu mbele ya mpakwa mafuta wangu daima.
36 Og det skal ske, hver den, som bliver tilovers i dit Hus, skal komme at nedbøje sig for ham for en Sølvpenning og for et Stykke Brød; og han skal sige: Kære, lad mig komme til een af Præstetjenesterne at æde en Mundfuld Brød.
Kisha kila mmoja aliyeachwa katika mbari yenu atakuja na kusujudu mbele yake kwa ajili ya kipande cha fedha na ganda la mkate akisema, “Niteue katika baadhi ya ofisi ya ukuhani ili niweze kupata chakula.”’”