< Første Kongebog 3 >

1 Og Salomo besvogrede sig med Farao, Kongen af Ægypten, og tog Faraos Datter og førte hende ind i Davids Stad, indtil han havde fuldendt at bygge sit Hus og Herrens Hus og Jerusalems Mur trindt omkring;
Sulemani akawa na ushirikiano wa kindoa na Farao mfalme wa Misri. Alimwoa binti wa Farao na kumleta katika mji wa Daudi mpaka alipomaliza kujenga nyumba yake, nyumba ya BWANA, na ukuta wa Yerusalemu.
2 ikkun at Folket ofrede paa Højene; thi der var ikke bygget et Hus til Herrens Navn indtil disse Dage.
Watu walikuw wakitoa sadaka kwenye maeneo ya juu, kwa sababu hapakuwa bado na nyumba iliyokuwa imejengwa kwa jina la BWANA.
3 Men Salomo elskede Herren og vandrede efter Davids sin Faders Skikke, kun at han ofrede og gjorde Røgelse paa Højene.
Sulemani alionyesha upendo wake kwa BWANA kwa kutembea katika maagizo ya Daudi baba yake, isipokuwa tu alitoa dhabihu na kuchoma uvumba mahali pa juu.
4 Og Kongen gik til Gibeon for at ofre der, thi der var den store Høj, og Salomo ofrede tusinde Brændofre paa dette Alter.
Mfalme akaenda Gibioni kutoa sadaka kule, kwa kuwa hilo ndilo lilikuwa eneo kuu la juu. Sulemani katoa sadaka maelfu katika madhabu hiyo.
5 Herren aabenbarede sig for Salomo i Gibeon om Natten i en Drøm, og Gud sagde: Begær, hvad jeg skal give dig.
BWANA akaonekana kwa Sulemani huko Gibioni katika ndoto ya usiku; akasema, “Omba! uanataka nikupe nini?”
6 Og Salomo sagde: Du har gjort stor Miskundhed imod din Tjener David, min Fader, ligesom han og vandrede for dit Ansigt i Sandhed og i Retfærdighed og i Hjertets Oprigtighed imod dig; og du har bevaret ham denne store Miskundhed og har givet ham en Søn, som sidder paa hans Trone, som det ses paa denne Dag.
Kwa hiyo Sulemani akasema, “umeonyesha uaminifu wa agano mkuu kwa mtumishi wako, Daudi baba yangu, kwa sababu alitembea mbele yako kwa ukweli na uaminifu, katika haki ya moyo na katika unyofu wa moyo. Umetunza kwa ajili yake hili agano kuu kwa uaminifu na umempa mwana wake kuketi kwenye kiti chake cha enzi leo.
7 Og nu, Herre, min Gud! du har gjort din Tjener til Konge i min Fader Davids Sted; men jeg er et ungt Menneske, og jeg forstaar ikke at gaa ud eller ind;
Na sasa, BWANA, Mungu wangu, umemfanya mtumishi wako kuwa mfalme katika nafasi ya Daudi baba yangu, japo mimi ni mtoto mdogo. Sijui namna ya kuiingia na kutoka.
8 og din Tjener er midt iblandt dit Folk, som du har udvalgt, et stort Folk, saa det ikke kan tælles eller beregnes for Mangfoldigheds Skyld:
Mtumishi wako yuko katikati ya watu wako uliowachagua, kundi kubwa, watu wangi wasiohesabika.
9 Saa giv din Tjener et forstandigt Hjerte til at dømme dit Folk og til med Forstand at skelne imellem godt og ondt; thi hvo kan dømme dette dit mægtige Folk?
Kwa hiyo umpe mtumishi wako moyo wa uelewa wa kuwahukumu watu wako. Kwani ni nani awezaye kuwahukumu watu wako hawa walio wengi?”
10 Og det Ord var godt for Herrens Øjne, at Salomo begærede denne Ting.
Ombi hili la Sulemani likampendeza Bwana.
11 Og Gud sagde til ham: Efterdi du har begæret denne Ting og ikke har begæret dig et langt Liv og ikke har begæret dig Rigdom og ikke har begæret dine Fjenders Sjæl, men har begæret dig Forstand til at holde Dom:
Kwa hiyo Mungu akamwambia. “Kwa sababu umeomba jambo hili na haujajiombea maisha marefu au utajiri au uhai wa maadui wako, lakini umeomba ufahamu wa kutambua hukumu ya haki,
12 Se, saa har jeg gjort efter dit Ord, se, jeg har givet dig et viist og forstandigt Hjerte, at der ikke har været nogen som du før dig; ej heller nogen som du skal opstaa efter dig.
Tazama sasa nitafanya yote uliyoniomba wakati uliponipa ombi lako. Ninakupa moyo wa hekima na ufahamu, kwa kuwa hapajawahi kuwa na mtu wa kuwa kama wewe kabla yako, na hakuna wa kuwa kama wewe atakayeinuka baada yako.
13 Og jeg har endog givet dig det, som du ikke har begæret, baade Rigdom og Ære, saa at der ikke har været nogen som du iblandt Kongerne i alle dine Dage.
Pia ninakupa hata ambayo hujaomba, vyote heshima na utajiri, ili kwamba pasije pakawa na mfalme wa kuwa kama wewe katika siku zako zote.
14 Og dersom du vandrer i mine Veje, at holde mine Skikke og mine Bud, saaledes som David din Fader har vandret, da vil jeg forlænge dine Dage.
Kama utatembea katika njia zangu na kuyatunza maagizo yangu na maagizo yangu, kama alivyofanya baba yako Daudi, ndipo nitakapoziongeza siku zako.”
15 Og Salomo vaagnede, og se, det var en Drøm; og han kom til Jerusalem og stod foran Herrens Pagts Ark og ofrede Brændofre og gjorde Takofre og gjorde alle sine Tjenere et Gæstebud.
Kisha Sulemani alipoamka, na tazama, ilikuwa ndoto. Akaja Yerusalemu na akasimama mbele ya sanduku na agano la Bwana. Akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, na akawafanyia sherehe watumishi wake wote.
16 Da kom to Kvinder, som vare Skøger, til Kongen, og de stode for hans Ansigt.
Kisha wanawake wawili waliokuwa makahaba wakaja mbele ya mfalme wakasimama mbele yake.
17 Og den ene Kvinde sagde: Hør mig, min Herre! jeg og denne Kvinde boede i eet Hus, og jeg fødte hos hende i Huset.
Mwanamke mmoja akasema, “Aa, bwana wangu, mwanamke huyu na mimi tunaishi katika nyumba moja, Nilizaa mtoto tukiwa pamoj na yeye katika nyumba yetu.
18 Og det skete paa den tredje Dag, efter at jeg havde født, da fødte ogsaa denne Kvinde; og vi vare sammen, der var ingen fremmed hos os i Huset, uden vi to i Huset.
Ikatokea siku ya tatu baada ya kujifungua na yeye akajifungua. Tulikuwa sisi tu. Hapakuwepo na mtu mwingine yeyote katika nyumba yetu, ila sisi tu wawili katika hiyo nyumba.
19 Og denne Kvindes Søn døde om Natten, thi hun laa paa ham.
Kisha mtoto wa mwanamke huyu akafa wakati wa usiku, kwa sababu alimlalia.
20 Og hun stod op midt om Natten og tog min Søn fra min Side, der din Tjenestekvinde sov, og hun lagde ham i sin Arm, og lagde sin døde Søn i min Arm.
kwa hiyo akamka wakati huo wa usiku wa manane akamchukua mwanangu toka pembeni yangu, wakati mimi mtumishi wako nilipokuwa usingizini, na akamlaza kwenye kifua chake, na akamlaza mtoto wake aliyekufa juu ya kifua changu.
21 Og jeg stod op om Morgenen, at give min Søn at die, se, da var han død; men om Morgenen gav jeg nøje Agt paa ham, se, da var det ikke min Søn, som jeg havde født.
Asubuhi nilipoamka ili kumhudumia mwanangu, nikaona kuwa alikuwa amekufa. Lakini nilipomwangalia kwa makini wakati huo wa asubuhi, nikagundua kuwa hakuwa yule mwanangu niliyezaa,”
22 Og den anden Kvinde sagde: Det er ikke saa; thi den levende er min Søn, men den døde er din Søn; og denne sagde: Det er ikke saa; thi den døde er din Søn, men den levende er min Søn; og de talede saa for Kongens Ansigt.
Yule mwanamke mwingine akasema, “Hapana, Huyu aliye hai ndiye wangu. Na yule aliyekufa ndiye wako.” Yule mwanamke wa kwanza akasema, “Hapana, Yule mtoto aliyekufa ndiye mwanao, na huyu aliye hai ndiye wangu.” Hivi ndivyo walivyoongea mbele ya mfalme.
23 Da sagde Kongen: Denne siger: Denne er min Søn, den levende, og den døde er din Søn; og denne siger: Det er ikke saa; thi den døde er din Søn, men den levende er min Søn.
Kisha mfalme akasema, “Mmoja wenu anasema, 'huyu aliye hai ni wangu, na kumbe mwanao ndiye aliye kufa,'na mwingine naye anasema, 'Hapana, mwanao ni yule aliyekufa, na mwanangu ni huyu aliye hai.'”
24 Og Kongen sagde: Henter mig et Sværd; og de bragte Sværdet ind for Kongens Ansigt.
Mfalme akasema, ''Nileteeni upanga.” Kwa hiyo wakaleta upanga kwa mfalme.
25 Da sagde Kongen: Deler det levende Barn i to Dele, og giver den ene Halvdelen og den anden Halvdelen.
Kisha mfalme akasema, “Mgawe mtoto aliye hai katika vipande viwili, na huyu mwanamke apewe nusu na yule mwingine naye apewe nusu.”
26 Da sagde Kvinden, hvis Søn den levende var, til Kongen (thi hendes inderste brændte for hendes Søn), ja hun sagde: Hør mig, min Herre! giver hende det levende Barn, og slaar det dog ikke ihjel; men hin sagde: Det skal hverken være mit eller dit, deler det.
Yule mwanamke mwenye mtoto aliyekuwa hai akamwambia mfalme, kwa kuwa moyo wake ulikuwa na huruma sana kwa mwanae, akasema, “Aa, bwana wangu, mpatie huyu mtoto aliye hai, na usimwue kamwe.” Lakini yule mwanamke mwingine akasema, “Hatakuwa wangu wala wako. Mgawe.”
27 Og Kongen svarede og sagde: Giver denne det levende Barn, og slaar det ikke ihjel; hun er Moder til det.
Ndipo mfalme aliposema, “Mpe yule mwanamke wa kwanza mtoto aliye hai, na kamwe usimwue. Yeye ndiye mama wa mtoto huyu.”
28 Og al Israel hørte Dommen, som Kongen havde dømt, og de frygtede for Kongens Ansigt; thi de saa, at Guds Visdom var i ham til at holde Dom.
Israeli wote waliposikia hukumu ambayo mafalme ametoa, walimwogopa mfalme, kwa sababu waliona kuwa hekima ya Mungu ilikuwa ndani yake kwa ajili ya kutoa kuhukumu.

< Første Kongebog 3 >