< Første Krønikebog 26 >
1 Hvad Portnernes Skifter angaar, saa var der af Koriterne Meselemia, Kores Søn, af Asafs Børn.
Huu ulikuwa mgawanyiko wa walinzi wa lango: Kutoka kwa Wakora, Meshelemia mwana wa Kore, wa uzao wa Asafu.
2 Og Meselemia havde Sønner: Sakaria den førstefødte, Jedial den anden, Sebadja den tredje, Jathniel den fjerde,
Meshelemia alikuwa na wana wa kiume: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wapili, Zebadia watatu, Yathinieli wanne,
3 Elam den femte, Johanan den sjette, Eljoenaj den syvende.
Elamu watano, Yehohanani wasita, Eliehoenai wasaba.
4 Og Obed-Edom havde Sønner: Semaja den førstefødte, Josabad den anden, Joa den tredje og Sakar den fjerde og Nethaneel den femte,
Obedi alikuwa na wana wa kiume: Shemaia wa kwanza, Yehozabadi wapili, Yoa watatu, na Sakari wanne, na Nethanieli watano,
5 Ammiel den sjette, Isaskar den syvende, Peulthaj den ottende; thi Gud havde velsignet ham.
Amieli wasita, Isakari wasaba, Peulethai wanane, kwa kuwa Mungu alimbariki Obedi Edomu.
6 Og for hans Søn Semaja bleve Sønner fødte, som herskede i deres Fædres Hus; thi de vare vældige i Styrke.
Kwa Shemaia mwanae walizawa wana walio tawala familia zao; walikuwa wanaume wenye uwezo mbali mbali.
7 Semajas Sønner vare: Othni og Refael og Obed, Elsabad, hans Brødre, duelige Folk, Elihu og Semakja.
Wana wa Shemaia walikuwa Othini, Refaeli, Obedi, na Elizabadi. Ndugu zake Elihu na Semakia walikuwa wanaume wenye uwezo mbali mbali.
8 Alle disse vare af Obed-Edoms Sønner, de med deres Sønner og deres Brødre, duelige Mænd og stærke til Tjenesten; der var to og tresindstyve af Obed-Edom.
Hawa wote walikuwa uzao wa Obedi Edomu. Wao na wanao na ndugu zao walikuwa wanaume wenye uwezo wa kufanya wajibu wao katika huduma ya hema la kuabudia. Palikuwa na sitini na mbili walio kuwa na undugu na Obedi Edomu.
9 Og Meselemias Sønner og Brødre, duelige Folk, vare atten.
Meshelemia alikuwa na wana na ndugu, wanaume wenye uwezo, jumla ya kumi na nane.
10 Og Hosa af Meraris Børn havde Sønner: Simri var den første, enddog han ikke var den førstefødte, men hans Fader havde sat ham til at være den første;
Hosa, mzao wa Merari, alikuwa na wana: Shimiri kiongozi (japo hakuwa mzaliwa wa kwanza, baba yake alimfanya kiongozi),
11 Hilkia den anden, Tebalia den tredje, Sakaria den fjerde; alle Hosas Sønner og Brødre vare tretten.
Hilikia wapili, Tebalia watatu, Zekaria wanne. Wote wa wana wa Hosa na ndugu walikuwa kumi na tatu kwa idadi.
12 Efter disse, nemlig Mændenes Øverster, faldt Portnernes Skifter til Vagterne, i Forening med deres Brødre, for at gøre Tjeneste i Herrens Hus.
Huu mgawanyiko wa walinzi wa lango, sambamba na viongozi, ulikuwa na majukumu, kama ndugu zao, kutumika katika nyumba ya Yahweh.
13 Og de kastede Lod, saavel for den yngste som for den ældste, efter deres Fædres Hus, til hver Port.
Walirusha kura, wadogo kwa wakubwa, kulingana na familia zao, kwa kila lango.
14 Og Lodden imod Østen faldt for Selemia; og de kastede Lod for hans Søn Sakaria, en klog Raadgiver, og hans Lod faldt ud imod Norden.
Kura ilipo rushwa kwa lango la mashariki, ilimuangukia Shelemia. Kisha wakarusha kura kwa Zekaria mwana wake, mshauri makini, na kura yake ikatokea lango la kaskazini.
15 For Obed-Edom faldt Lodden imod Sønden, og for hans Sønner imod Skatkamrenes Hus.
Kwa Obedi Edomu kulipangiwa lango la kusini, na wanae walipangiwa nyumba za ghala.
16 For Suppim og for Hosa faldt Lodden imod Vesten ved Skalleket Port, paa Vejen, som gaar op ad; der var Vagt over for Vagt.
Shufimu na Hosa walipangiwa lango la magharibi pamoja na lango la Shalekethi, kwa barabara ya juu. Lindo lilikabiidhiwa kwa kila familia.
17 Imod Østen vare seks af Leviterne, imod Norden vare fire hver Dag, imod Sønden fire hver Dag og ved Skatkamrene to og to.
Kwa mashariki walikuwa Walawi sita, kaskazini kwa siku moja, kusini kwa siku moja, na nyumba za ghala wawili.
18 Ved Parbar imod Vesten: Fire var der paa Vejen, to hen imod Parbar.
Katika ua kuelekea magharibi wanne walipangwa, wanne barabarani, na wawili katika ua.
19 Disse vare Portnernes Skifter af Koriternes Børn og af Meraris Børn.
Haya yalikuwa magawanyiko ya walinzi wa lango. Palijazwa na uzao wa Kora na Merari.
20 Men af Leviterne var Ahia over Guds Hus's Skatte og de hellige Tings Skatte.
Miongoni mwa Walawi, Ahija alikuwa kiongozi wa hazina ya nyumba ya Mungu, na hazina ya vitu vya Yahweh.
21 Ladans Sønner, nemlig Gersonitens Sønner af Ladan, Øversterne for Gersoniten Ladans Fædrenehuse, var Jehieli.
Wazao wa Ladani, walitoka kwa Gerishoni kupitia kwake na walio kuwa viongozi wa familia za Ladani Mgerishoni, walikuwa Yehieli na wanae,
22 Jehielis Sønner vare Setham og Joel, hans Broder, som vare over Herrens Hus's Skatte.
Zethamu, na Yoeli kaka yake, aliyesimamia ghala za nyumba ya Yahweh.
23 Af Amramiterne, af Jizehariterne, af Hebroniterne, af Ussieliterne,
Kulikuwa na askari walio chukuliwa kwa koo za Amramu, Izhari, Hebroni, na uzieli.
24 var Sebuel en Søn af Gersom, Moses Søn, Opsynsmand over Skattene.
Shebueli mwana wa Gerishomu mwana wa Musa, alikuwa msimamizi wa nyumba za ghala.
25 Men hvad angaar hans Brødre, dem af Elieser, saa var dennes Søn Rehabia og dennes Søn Jesaja og dennes Søn Joram og dennes Søn Sikri og dennes Søn Selomoth.
Ndugu zake wa ukoo wa Eliezeri walikuwa Rehabia mwanae, mwana wa Rehabia Yeshaia, mwana wa Yeshaia Yoramu, mwana wa Yoramu Zikiri, na mwana wa Zikiri Shelomothi.
26 Denne Selomoth og hans Brødre vare over alle Skattene af de hellige Ting, som Kong David samt Øversterne for Fædrenehusene, Høvedsmændene over tusinde, over hundrede og Stridshøvedsmændene havde helliget.
Shelomothi na ndugu zake walikuwa wasimamizi wa nyumba zote za ghala zinazo hifadhi vitu vyote vya Yahweh, ambavyo Daudi mfalme, viongozi wa familia, wakuu wa maelfu na mamia, na wakuu wa jeshi walivyo vitenga.
27 Fra Krigene og af Byttet havde de helliget det til at udbedre Herrens Hus med.
Walitenga vitu walivyo vichukuwa kwenye mapambano kwa ajili ya kutunza nyumba ya Yahweh.
28 Og alt hvad Samuel, Seeren og Saul, Kis's Søn, og Abner, Ners Søn, og Joab, Zerujas Søn, havde helliget, alt hvad hver havde helliget, det var under Selomiths og hans Brødres Haand.
Pia walikuwa wahusika wa kila kitu kilicho tengwa kwa ajili ya Yahweh na Samweli nabii, Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Zeruia. Kila kitu kilicho tengwa kwa ajili ya Yahweh kilikuwa chini ya ulinzi wa shelomothi na ndugu zake.
29 Af Jizehariterne vare Kenanja og hans Sønner beskikkede over Israel, til den udvortes Gerning, som Fogeder og som Dommere.
Wa uzao wa Izhari, Kenania na wana wake walikuwa wahusika wa mambo ya ndani ya Israeli. Walikuwa maafisa na waamuzi.
30 Af Hebroniterne vare Hasabia og hans Brødre, duelige Folk, tusinde og syv Hundrede, beskikkede over Embederne i Israel paa denne Side Jordanen imod Vesten, til alle Haande Herrens Gerning og til Kongens Tjeneste.
Wa uzao wa Hebroni, Hashabia na kaka zake, wanaume wenye uwezo 1, 700, walikuwa wahusika wa kazi ya Yahweh na kazi ya mfalme. Walikuwa upande wa mgharibi mwa Yordani.
31 Af Hebroniterne var Jerija den Øverste for Hebroniterne efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse; i det fyrretyvende Aar af Davids Regering blev der søgt og fundet iblandt dem vældige Helte i Jaeser i Gilead.
Kutoka uzao wa Hebroni, Yeriya alikuwa kiongozi wa uzao wake, walihesabiwa kutoka orodha za familia zao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi walitathimini kumbukumbu na kugundua miongoni mwao wanaume wa uwezo katika Yazeri ya Gileadi.
32 Og hans Brødre vare duelige Mænd, to Tusinde og syv Hundrede, Øverster for Fædrenehuse; og Kong David satte dem over Rubeniterne og Gaditerne og den halve Manasses Stamme i alle Guds Sager og alle Kongens Sager.
Yerija alikuwa na ndugu 2, 700, walio kuwa viongozi wenye uwezo katika familia. Daudi aliwafanya waangalizi wa makabila ya Rubeni na Gadi, na nusu kabila la Manase, kwa kila jambo linalo muhusu Mungu, na kwa mambo ya mfalme.