< Marek 10 >
1 Ježíš opustil Kafarnaum a prošel Zajordáním do Judska. I zde ho obklopilo množství lidí a on je začal učit jako obvykle.
Yesu akaondoka huko, akavuka Mto Yordani, akaenda sehemu za Uyahudi. Umati mkubwa wa watu ukaenda kwake tena, naye kama ilivyokuwa desturi yake, akawafundisha.
2 Přišli však za ním farizejové a pokoušeli se ho nachytat: zeptali se ho, zda je dovolen rozvod.
Baadhi ya Mafarisayo wakaja ili kumjaribu kwa kumuuliza, “Je, ni halali mtu kumwacha mke wake?”
3 Místo odpovědi jim dal otázku: „Co řekl o rozvodu Mojžíš?“
Yesu akawajibu, “Je, Mose aliwaamuru nini?”
4 „K tomu, aby manželství bylo zrušeno, podle Mojžíše stačí, když muž napíše ženě rozlukový list.“
Wakajibu, “Mose aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
5 „To byl jen Mojžíšův ústupek tvrdosti lidského srdce, “řekl na to Ježíš. „Bůh si to tak nikdy nepřál.
Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
6 Hned na počátku stvořil člověka jako nerozlučnou dvojici, muže a ženu.
Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke.
7 Proto muž opustí své rodiče a připojí se ke své manželce;
Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.’
8 v tom spojení již nežijí jako dva jedinci, ale stávají se jednou bytostí.
Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena, bali mwili mmoja.
9 A proto člověk nemá právo rozdělit, co Bůh spojil.“
Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
10 Později se učedníci znovu k té otázce vrátili.
Walipokuwa tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza kuhusu jambo hili.
11 Vyložil jim to: „Kdo se rozvede se svou ženou a ožení se s jinou, hřeší stejně, jako by měl ženy dvě.
Akawajibu, “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kuoa mke mwingine, anazini naye.
12 A právě tak rozvede-li se žena se svým mužem a vdá se za jiného, dopouští se cizoložství.“
Naye mwanamke amwachaye mumewe na kuolewa na mume mwingine, anazini.”
13 Lidé nosili k Ježíšovi děti, aby jim žehnal. Učedníci jim domlouvali, aby ho neobtěžovali.
Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wake wakawakemea.
14 Když to Ježíš slyšel, zlobil se: „Neodhánějte ty děti a nebraňte jim, když chtějí ke mně. I jim přece patří Boží království.
Yesu alipoona yaliyokuwa yakitukia, akachukizwa. Akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa.
15 A říkám vám, že kdo nepřijde k Bohu s dětskou prostotou, nestane se občanem toho království.“
Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”
16 Bral děti do náruče, hladil je a žehnal jim.
Akawachukua watoto mikononi mwake, akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.
17 Když se zase vydali na cestu, dohonil je nějaký muž a padl před Ježíšem na kolena: „Dobrý učiteli, co mám dělat, abych získal věčný život?“ (aiōnios )
Yesu alipokuwa anaondoka, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake, akamuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios )
18 „Proč mi říkáš dobrý? Vždyť dobrý je jen Bůh, “odvětil Ježíš.
Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake.
19 „A k tvé otázce – přikázání přece znáš: nebudeš zabíjet, cizoložit, krást, lhát, podvádět, budeš si vážit svých rodičů.“
Unazijua amri: ‘Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, waheshimu baba yako na mama yako.’”
20 „Mistře, všechno jsem dodržoval od mládí.“
Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”
21 Ježíš ho objal pohledem: „A přece ti něco schází. Jdi a prodej všechno, co máš, peníze rozdej chudým a získáš tak poklad v nebi. Potom se vrať a staň se mým následovníkem.“
Yesu akamtazama na kumpenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho uwape maskini hizo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
22 Když to ten člověk vyslechl, zesmutněl a odešel s těžkým srdcem. Byl totiž velmi bohatý.
Yule mtu aliposikia hayo, akasikitika sana. Akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 Ježíš ho mlčky sledoval očima a pak se otočil k učedníkům: „Jak těžké je pro boháče vejít do Božího království!“
Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa wenye mali kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
24 To je zarazilo. Není snad majetek důkazem Boží přízně? „Přátelé, do Božího království se těžko dostanou ti, pro které jsou peníze a majetek smyslem života.
Wanafunzi wake wakashangazwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akawaambia tena, “Wanangu, tazama jinsi ilivyo vigumu kwa wale wanaotumainia mali kuingia katika Ufalme wa Mungu.
25 Snáze projde velbloud tou uzoučkou brankou, které říkáte jehelné ucho, než bohatý vejde do Božího království.“
Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajirikuingia katika Ufalme wa Mungu.”
26 To jim dodalo. „Má vůbec někdo naději, že se tam dostane?“říkali si mezi sebou.
Wanafunzi wake wakashangaa sana. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
27 Podíval se na ně. „Člověk na to nestačí, ale Bůh je všemocný.“
Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu sivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
28 Tu promluvil Petr: „Ale my jsme se všeho vzdali a šli za tebou.“
Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha kila kitu na kukufuata wewe!”
29 „Ujišťuji vás, “odpověděl Ježíš, „že každému, kdo se z lásky ke mně a pro šíření evangelia něčeho vzdá – ať už domova, života se sourozenci, rodiči, manželkou a dětmi, nebo majetku,
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna mtu yeyote aliyeacha nyumba, ndugu wa kiume au wa kike, au mama au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili,
30 se to vrátí stonásobně už zde na zemi (i když neujde pronásledování) a v budoucnosti ho čeká věčný život. (aiōn , aiōnios )
ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao. (aiōn , aiōnios )
31 Mnozí, kteří u lidí něco znamenají, budou poslední, a těm nejpohrdanějším se tam dostane čestných míst.“
Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
32 Když potom byli na cestě do Jeruzaléma, Ježíš šel vpředu a ostatní se drželi za ním. Co jim Ježíš řekl, to je znepokojilo a naplnilo obavami. Zavolal k sobě svých dvanáct učedníků a znovu je připravoval na to, co ho čeká:
Walikuwa njiani wakipanda kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa ametangulia. Wanafunzi wake walishangaa, nao watu waliowafuata walijawa na hofu. Yesu akawachukua tena wale wanafunzi wake kumi na wawili kando na kuwaambia yatakayompata.
33 „Musíme do Jeruzaléma a tam Syn člověka padne do rukou velekněží a učitelů zákona a ti ho odsoudí a vydají pohanům.
Akasema, “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atasalitiwa kwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Wao watamhukumu kifo na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa,
34 Budou se mu veřejně vysmívat, plivat na něj, zbičují a zabijí ho. Ale třetí den vstane z mrtvých.“
ambao watamdhihaki na kumtemea mate, watampiga na kumuua. Siku tatu baadaye atafufuka.”
35 Přihlásili se Zebedeovi synové Jakub a Jan: „Mistře, chtěli bychom tě o něco poprosit.“
Kisha Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie lolote tutakalokuomba.”
36 „Co si ode mne přejete?“vzhlédl Ježíš.
Naye akawaambia, “Je, mwataka niwafanyie jambo gani?”
37 „Až usedneš na trůn, chtěli bychom ti sedět nejblíže se všech, každý z jedné strany vedle tebe.“
Wakamwambia, “Tupe kukaa mmoja upande wako wa kuume na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wako.”
38 „Nevíte, oč prosíte. Můžete pít z kalicha hořkosti, ze kterého musím pít já, a projít křtem utrpení, který mě čeká?“
Lakini Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi?”
39 „Ale jistě, “přisvědčili. „Dobře, budete pít z mého kalicha a budete pokřtěni stejným křtem.
Wakajibu, “Tunaweza.” Kisha Yesu akawaambia, “Kikombe nikinyweacho mtakinywea na ubatizo nibatizwao mtabatizwa,
40 Ale není mou věcí určovat vám pořadí v Božím království. To už je stanoveno.“
lakini kuketi mkono wangu wa kuume au wa kushoto si juu yangu mimi kuwapa. Nafasi hizi ni kwa ajili ya wale walioandaliwa.”
41 Ostatních deset se zlobilo na Jakuba a Jana.
Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
42 Ale Ježíš je svolal dohromady a řekl jim: „Víte, že vládcové mají moc nad národy, a kdo vládne, obvykle druhé utlačuje.
Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao.
43 Ale mezi vámi to tak být nemá. Naopak, kdo z vás chce být velký, ať všem pokorně slouží.
Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu,
44 A kdo z vás chce být na předním místě, ať je pomocníkem všech.
na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumwa wa wote.
45 Vždyť já – Syn člověka – jsem nepřišel na svět proto, aby mi ostatní sloužili, ale abych já sloužil jim a abych položil život pro záchranu mnoha lidí.“
Kwa kuwa hata Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”
46 Procházeli také Jerichem, kde se k nim přidal velký zástup. U cesty seděl slepý žebrák Bartimeus – Timeův syn.
Kisha wakafika Yeriko. Yesu alipokuwa akiondoka mjini na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mmoja, jina lake Bartimayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando ya njia akiomba msaada.
47 Když uslyšel, že to jde Ježíš Nazaretský, křičel: „Ježíši z rodu krále Davida, slituj se nade mnou!“
Aliposikia kuwa ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita, akaanza kupaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
48 Lidé mu domlouvali, aby mlčel. Ale on volal tím hlasitěji: „Synu Davidův, slituj se nade mnou!“
Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya, lakini yeye akazidi kupaza sauti, akisema, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
49 Ježíš ho uslyšel, zastavil se a přikázal, aby slepce zavolali. Vrátili se tedy k Bartimeovi se vzkazem: „Máš štěstí, Ježíš tě volá – vstaň!“
Yesu akasimama na kusema, “Mwiteni.” Hivyo wakamwita yule mtu kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Inuka, anakuita.”
50 Slepec odhodil svůj starý kabát, vyskočil a klopýtal k Ježíšovi.
Akiwa analivua lile joho lake, alisimama na kumwendea Yesu.
51 „Co pro tebe mohu udělat?“dotkl se ho Ježíš. „Mistře, chci vidět!“
Yesu akamuuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona.”
52 „Staň se, tvá víra tě zachránila.“V té chvíli se slepci vrátil zrak a on se vydal také za Ježíšem.
Yesu akamwambia, “Nenda zako, imani yako imekuponya.” Mara akapata kuona, akamfuata Yesu njiani.