< Zachariáš 14 >

1 Aj, den Hospodinův přichází, a rozděleny budou kořisti tvé u prostřed tebe.
Siku ya Bwana inakuja ambayo nyara zilizotekwa kwenu zitagawanywa miongoni mwenu.
2 Nebo shromáždím všecky národy proti Jeruzalému k boji, i bude dobyto město, a domové zloupeni, a ženy zhanobeny budou. A když vyjde díl města v zajetí, ostatek lidu nebude vyhlazeno z města.
Nitayakusanya mataifa yote huko Yerusalemu kupigana dhidi yake, mji utatekwa, nyumba zitavamiwa na kuporwa na wanawake watanajisiwa. Nusu ya mji watakwenda uhamishoni, lakini watakaobaki hawataondolewa kutoka mjini.
3 Nebo Hospodin vytáhna, bude bojovati proti těm národům, jakž bojuje v den potýkání.
Kisha Bwana atatoka na kupigana dhidi ya watu wa yale mataifa, kama apiganavyo siku ya vita.
4 I stanou nohy jeho v ten den na hoře Olivetské, kteráž jest naproti Jeruzalému od východu, a rozdvojí se hora Olivetská napoly k východu a k západu údolím velmi velikým, a odstoupí díl té hory na půlnoci, a díl její na poledne.
Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, mashariki mwa Yerusalemu, nao Mlima wa Mizeituni utagawanyika mara mbili kuanzia mashariki hadi magharibi, ukifanya bonde kubwa, nusu ya mlima ukisogea kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini.
5 I budete utíkati před údolím hor; nebo dosáhne údolí hor až k Azal. Budete, pravím, utíkati, jako jste utíkali před země třesením za dnů Uziáše krále Judského, když přijde Hospodin Bůh můj, a všickni svatí s ním.
Nanyi mtakimbia kupitia katika bonde hilo la mlima wangu kwa kuwa litaenea hadi Aseli. Mtakimbia kama mlivyokimbia tetemeko la ardhi katika siku za Uzia mfalme wa Yuda. Kisha Bwana Mungu wangu atakuja na watakatifu wote pamoja naye.
6 I stane se v ten den, že nebude světla drahého, ani tmy husté.
Siku hiyo hakutakuwepo nuru, baridi wala theluji.
7 A tak bude den jeden, kterýž jest znám Hospodinu, aniž bude den, ani noc; a však stane se, že v čas večera bude světlo.
Itakuwa siku ya kipekee, isiyo na mchana wala usiku, siku ijulikanayo na Bwana. Jioni inapofika nuru itakuwepo.
8 Stane se také v ten den, že vycházeti budou vody živé z Jeruzaléma, díl jich k moři východnímu, a díl jich k moři nejdalšímu. V létě i v zimě bude.
Siku hiyo, maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu, nusu kwenda kwenye bahari ya mashariki, na nusu kwenda kwenye bahari ya magharibi wakati wa kiangazi na wakati wa masika.
9 A bude Hospodin králem nade vší zemí; v ten den bude Hospodin jediný, a jméno jeho jedno.
Bwana atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo atakuwepo Bwana mmoja na jina lake litakuwa jina pekee.
10 A učiněna bude všecka tato země jako rovina od Gaba k Remmon na polední straně Jeruzalému, kterýž vyvýšen jsa, státi bude na místě svém, od brány Beniaminovy až k místu brány první, a až k bráně úhlové, a od věže Chananeel až k presu královskému.
Nchi yote kuanzia Geba, kaskazini mwa Yuda, hadi Rimoni, kusini mwa Yerusalemu, itakuwa kama Araba. Lakini Yerusalemu utainuliwa juu na kubaki mahali pake, toka Lango la Benyamini hadi mahali pa Lango la Kwanza, mpaka kwenye Lango la Pembeni na kutoka Mnara wa Hananeli hadi kwenye mashinikizo ya divai ya mfalme.
11 A budou bydliti v něm, a nebude více v prokletí; město Jeruzalém zajisté bezpečně seděti bude.
Utakaliwa na watu, kamwe hautaharibiwa tena, Yerusalemu utakaa salama.
12 Tato pak bude rána, kterouž raní Hospodin všecky národy, kteříž by bojovali proti Jeruzalému: Usuší tělo jednoho každého, stojícího na nohách svých, a oči jednoho každého usvadnou v děrách svých, a jazyk jednoho každého usvadne v ústech jejich.
Hii ndiyo tauni ambayo Bwana atapiga nayo mataifa yote ambayo yalipigana dhidi ya Yerusalemu: Nyama ya miili yao itaoza wangali wamesimama kwa miguu yao, macho yao yataoza kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza vinywani mwao.
13 I stane se v ten den, že bude znepokojení Hospodinovo veliké mezi nimi, tak že uchopí jeden druhého ruku, a vztažena bude ruka jednoho na ruku druhého.
Katika siku hiyo Bwana atawatia wanaume hofu kuu. Kila mwanaume atakamata mkono wa mwenzake nao watashambuliana.
14 Také i ty, Judo, bojovati budeš v Jeruzalémě, a shromážděno bude zboží všech národů vůkol, zlato a stříbro, i roucha velmi mnoho.
Yuda pia atapigana katika Yerusalemu. Utajiri wa mataifa yote yanayoizunguka Yerusalemu utakusanywa, wingi wa dhahabu, fedha na nguo.
15 A podobná bude rána koní, mezků, velbloudů a oslů i všech hovad, kteráž budou v tom ležení, podobná ráně té.
Tauni ya aina iyo hiyo itapiga farasi na nyumbu, ngamia na punda, nao wanyama wote walioko kwenye kambi za adui.
16 I stane se, že kdožkoli pozůstane ze všech národů, kteříž by přitáhli proti Jeruzalému, přicházeti budou z rok do roka klaněti se králi Hospodinu zástupů a slaviti slavnost stánků.
Kisha walionusurika katika mataifa yote ambayo yaliushambulia Yerusalemu watakuwa wakipanda Yerusalemu kila mwaka kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote na kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
17 I stane se, kdo z čeledí země nebude přicházeti do Jeruzaléma klaněti se králi Hospodinu zástupů, že nebude na ně pršeti déšt.
Ikiwa taifa lolote la dunia hawatakwenda Yerusalemu kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote, mvua haitanyesha kwao.
18 A jestliže čeled Egyptská nevstoupí, ani přijde, jakkoli na ně nepršívá, přijde však táž rána, kterouž raní Hospodin národy, kteříž by nepřicházeli k slavení slavnosti stánků.
Ikiwa watu wa Misri nao hawatakwenda kushiriki, hawatapata mvua. Bwana ataleta juu yao tauni ile ambayo itawapiga mataifa yale ambayo hayatakwenda kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
19 Tať bude pokuta pro hřích Egyptských a pokuta pro hřích všech národů, kteříž by nechodili k slavení slavnosti stánků.
Hii itakuwa adhabu ya Misri na adhabu ya mataifa yote yale ambayo hayatakwenda Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
20 V ten den bude na zvoncích koňských: Svatost Hospodinu; a bude hrnců v domě Hospodinově jako číší před oltářem.
Katika siku hiyo, kengele zilizofungwa kwenye farasi zitaandikwa maneno haya: Takatifu kwa Bwana, navyo vyungu vya kupikia katika nyumba ya Bwana vitakuwa kama bakuli takatifu mbele ya madhabahu.
21 Nýbrž bude všeliký hrnec v Jeruzalémě a v Judstvu svatost Hospodinu zástupů; a přicházejíce všickni, kteříž obětovati mají, budou je bráti a vařiti v nich. Aniž bude Kananejský více v domě Hospodina zástupů v ten den.
Kila chungu kilichoko Yerusalemu na Yuda kitakuwa kitakatifu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote na wote wanaokuja kutoa dhabihu watachukua baadhi ya vyungu hivyo na kupikia. Katika siku hiyo hatakuwepo tena mfanyabiashara katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote.

< Zachariáš 14 >